Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,340
- 51,900
Kwema Wakuu,
Ukishakuwa Chawa katika siasa jihesabie upo kundi la wanyonge. Utawala unaanzia kwenye nafsi ya mtu. Ukifuatilia watawala wakubwa wa ngazi za juu hasa ufalme au Urais wanafanana tabia moja, kutokuwa Chawa.
Ni rahisi sana mtu asiyechawa kuingia katika nafasi ya Urais au nafasi kubwakubwa. Deep State haiwezi kuku-consider kwa nafasi za juu ikiwa tuu wamekuona unatabia za kichawa.
Sababu kubwa inayofanya Machawa wasipewe kipaombele ni tabia yao ya bendera fuata upepo, kutokuwa na msimamo, Usaliti. Yaani Machawa wote kiasili wana nature ya Usaliti ni kutokana hawana msimamo na hawajui nini cha kusimamia. Mwisho Chawa wengi hutokana njaa, ufukara na upeo mdogo wa kufikiri.
Watu wenye upeo mkubwa na wenye vipato kamwe hawawezi kuwa Chawa.
Vijana, unapoingia kwenye siasa elewa vitu kama hivyo. Wengi huishia kuwa Chawa, kulamba viatu vya Wakubwa na hawaendi popote. Na hawawezi kwenda popote kwa sababu sisi Watawala tunajua Machawa ni wanafiki.
Leo anakusifia lakini kesho akipata cheo cha juu ndio huyohuyo atakugeuka.
Machawa msijisumbue kuzitafuta nafasi za juu. Futeni ndoto hizo kwa sababu hatutaruhusu Watu fukara na wenye upeo wa chini kuingia kwenye list ya watawala.
Ijumaa Kareem.
Ukishakuwa Chawa katika siasa jihesabie upo kundi la wanyonge. Utawala unaanzia kwenye nafsi ya mtu. Ukifuatilia watawala wakubwa wa ngazi za juu hasa ufalme au Urais wanafanana tabia moja, kutokuwa Chawa.
Ni rahisi sana mtu asiyechawa kuingia katika nafasi ya Urais au nafasi kubwakubwa. Deep State haiwezi kuku-consider kwa nafasi za juu ikiwa tuu wamekuona unatabia za kichawa.
Sababu kubwa inayofanya Machawa wasipewe kipaombele ni tabia yao ya bendera fuata upepo, kutokuwa na msimamo, Usaliti. Yaani Machawa wote kiasili wana nature ya Usaliti ni kutokana hawana msimamo na hawajui nini cha kusimamia. Mwisho Chawa wengi hutokana njaa, ufukara na upeo mdogo wa kufikiri.
Watu wenye upeo mkubwa na wenye vipato kamwe hawawezi kuwa Chawa.
Vijana, unapoingia kwenye siasa elewa vitu kama hivyo. Wengi huishia kuwa Chawa, kulamba viatu vya Wakubwa na hawaendi popote. Na hawawezi kwenda popote kwa sababu sisi Watawala tunajua Machawa ni wanafiki.
Leo anakusifia lakini kesho akipata cheo cha juu ndio huyohuyo atakugeuka.
Machawa msijisumbue kuzitafuta nafasi za juu. Futeni ndoto hizo kwa sababu hatutaruhusu Watu fukara na wenye upeo wa chini kuingia kwenye list ya watawala.
Ijumaa Kareem.