Ni nani huyu Cool 9 Jamani?

Grand Master Dulla

JF-Expert Member
Jul 20, 2012
411
146
Miaka ya 80-90 kulikuwa na jamaa mmoja mitaa ya Manzese na Magomeni alikuwa anaitwa Cool 9. Huyu bwana alikuwa ni maarufu sana Dar es salaam na chanzo cha umaarufu wake ni kwamba huyu jamaa alikuwa ni fundi sana wa kupigana.

Alikuwa nafikiri ndio mbabe wa dar es salaam enzi hizo sasa sijui aliishia wapi mana alisifika sana.Kwa yeyote mwenye kumjua na kujua vituko vyake si vibaya tukakumbushana vitu vya zamani, ingawa vingine vilikuwa vinachukiza lakini maudhi yake yameshamezwa na wakati na itakuwa kama kumbukumbu kwa matukio tusiyoyajua.

Tumjadili jamani
 
Mi nishamsikia, na sifa yake kubwa ni kuwa ukienda cinema enzi hizo au mbowe klabu na demu kisu, basi huchezi nae kwa raha, anakuja kumbambia na kumvutia kwake, ole wako ulete kidodomo unapewa NAKOZ za kufa mutu. Basi akawa anawaonea wahindi huyooooo. Kama we demu kisu unajua sana kuyarudi matwist na jazz band mkisikia yupo ukumbini shurti kucheza kama wagonjwa wa kifaduro lasivo ndo ushapata kampani hivooo! Hii ishu alinipa mama Lara 1 enzi hizo akiwa Mzumbe ila ndo kamaliza Aghakani (Mzizima) anamchuna baba lara 1 akiwa kapata kazi, baada ya kurudi Unyamwezini, ila ushamba wa Marangu haujamuisha. Kila weekend Mama Lara 1 ANAMUONESHA JIJI NA MATAA YAKE!!!! Chezeya! Bata lilikuwa Zamani saivi tunazuga tu!!!! Umenikumbusha mbali sanaaaaaa! AGE IS A THIEF!!!!!
 
Mi nishamsikia, na sifa yake kubwa ni kuwa ukienda cinema enzi hizo au mbowe klabu na demu kisu, basi huchezi nae kwa raha, anakuja kumbambia na kumvutia kwake, ole wako ulete kidodomo unapewa NAKOZ za kufa mutu. Basi akawa anawaonea wahindi huyooooo. Kama we demu kisu unajua sana kuyarudi matwist na jazz band mkisikia yupo ukumbini shurti kucheza kama wagonjwa wa kifaduro lasivo ndo ushapata kampani hivooo! Hii ishu alinipa mama Lara 1 enzi hizo akiwa Mzumbe ila ndo kamaliza Aghakani (Mzizima) anamchuna baba lara 1 akiwa kapata kazi, baada ya kurudi Unyamwezini, ila ushamba wa Marangu haujamuisha. Kila weekend Mama Lara 1 ANAMUONESHA JIJI NA MATAA YAKE!!!! Chezeya! Bata lilikuwa Zamani saivi tunazuga tu!!!! Umenikumbusha mbali sanaaaaaa! AGE IS A THIEF!!!!!

i see lara tupe stori zake bwana mana unaonekana unamjua vizuri sana.
 
Mie sijawahi kumsikia huyo jamaa..! Labda nilikuwa bado mdogo..!
 
i see lara tupe stori zake bwana mana unaonekana unamjua vizuri sana.

Hahahaaaaa! Mpaka niwe na Mamushka Lara 1 mutoto ya migo migo ndo anaemjua uzuri, mie ananihadithiaga kidogo kidogo katika shindano letu lisilo rasmi la MAMA VS MWANA NANI ANATEKETEZA BATA ZAIDI KATIKA UJANA!!!! Hahahaaaaa! Nampaga ushindi wa mezani tu, manake KULA BATA ENZI HIZO WAKATI WENZIE BUSY WAKIJENGA NCHI SI MCHEZOOO!!!! Sasa kuonesha yeye zaidi ndo ananipaga stori za wakali wa enzi hizooooooo!

Nyingine nilisikiaga kuwa akienda kwenye vilabu au sehemu ya pombe anaanzisha vagi lolote afu anamwga ile mitingasi na kukomaa wamdai yeye ili aonekane anazooooo.
 
alisha kufa.pale iringa alikua na crew yake yakina chansela na wengne kibao jamaa alikua anapga ngumi mbaya dizan kwao wote walikua wababe maana ata dada'ke alikua anapga mbaya.kuna wakati walifanya msako iringa wanakamata vibaka ukikutwa na panki au mlege unapgwa mbaya kisa mwenzao alipgwa na cku km 3 baada ya msako wenzao km2 walikufa kwa shaba 2kio la ujambaz mlandege godauni akiwemo kaka'ke alikua anaitwa ayat.umaarufu wake mkubwa ulitokana na kupgwa shaba mkononi ktk ugomv na mzungu.pia mkigana ukampga jua kila mkutanapo lazma alianzishe tena.
 
Hahahaaaaa! Mpaka niwe na Mamushka Lara 1 mutoto ya migo migo ndo anaemjua uzuri, mie ananihadithiaga kidogo kidogo katika shindano letu lisilo rasmi la MAMA VS MWANA NANI ANATEKETEZA BATA ZAIDI KATIKA UJANA!!!! Hahahaaaaa! Nampaga ushindi wa mezani tu, manake KULA BATA ENZI HIZO WAKATI WENZIE BUSY WAKIJENGA NCHI SI MCHEZOOO!!!! Sasa kuonesha yeye zaidi ndo ananipaga stori za wakali wa enzi hizooooooo!

Nyingine nilisikiaga kuwa akienda kwenye vilabu au sehemu ya pombe anaanzisha vagi lolote afu anamwga ile mitingasi na kukomaa wamdai yeye ili aonekane anazooooo.

Duh!!
Hatari Sana!
 
Iringa jamaa alikuwa anaogopeka kishenzi, ndo ilikuwa inadaiwa jamaa anachapa iringa nzima. Vijana wa leo kwa taarifa yenu enzi za mwalimu kulikuwa na mbabe wa darasa, shule, mtaa mkoa. Hao jamaa walikuwa balaa tupu usiombe ukanyage reli zao. Wanakudunda mbaya, siku hizi maisha yamekuwa peace sana, hakuna tena yale mambo ya ubabe
 
kulikuwa na ka mtindo flani songea miaka ya themanini. Nilikuwa std three tulipohamia songea nikakuta watoto wagomvi shuleni vibaya mno, ugomvi nje nje mkizipiga ukimdunda utasikia naenda kuagizia, hapo anamaanisha anakwenda kumtafuta mtu au kikundi waje wakudunde. Utashangaa mmetoka maeneo ya shule unakutana na wababe wanakusubiri kitakacho endelea hapo ni kichapo hahaaa
 
alisha kufa.pale iringa alikua na crew yake yakina chansela na wengne kibao jamaa alikua anapga ngumi mbaya dizan kwao wote walikua wababe maana ata dada'ke alikua anapga mbaya.kuna wakati walifanya msako iringa wanakamata vibaka ukikutwa na panki au mlege unapgwa mbaya kisa mwenzao alipgwa na cku km 3 baada ya msako wenzao km2 walikufa kwa shaba 2kio la ujambaz mlandege godauni akiwemo kaka'ke alikua anaitwa ayat.umaarufu wake mkubwa ulitokana na kupgwa shaba mkononi ktk ugomv na mzungu.pia mkigana ukampga jua kila mkutanapo lazma alianzishe tena.

Jamaa alikuwa ni noma alikuwa na kina chancellor wa iringa alikulia iringa na dar ila kwao ni dar ubungo na manzese na baba yake mzee yahya anakaa ubungo iringa ni kwa mama yake,alikuwa anapiga ngumi balaa dar nzima wanamjua huyo miaka hiyo sifa yake kubwa waliyokuwa wanamwogopea ni jambazi na alikuwa anakamatwa sana sababu ya tuhuma hizo za ujambazi wa silaha,ni kweli alipigwa bunduki iringa nafikiri siyo na mzungu bali na dereva wa magari ya mafuta masemi yanayokwenda zambia enzi hizo mafuta hadimu madereva wanatembea na bunduki ujambazi nje nje,alikuwa anawazuia saa 2 usiku wasiondoke mpaka washerehekee nao,ndipo dereva akadhani anabugudhiwa akampa ya mkono,
kaka skendo unamjua vizuri sana wewe ebu tupe stori zake na vituko vyake zaidi usiache kutupa uondo wake bwana.
 
mjomba skendo tupe historia ya huyo dada yake alikuwa anaitwa nani? na huyo kaka yake alikuwa anaitwa nani pia mana unaonekana unamjua vema sana tupe tupe kaka.
 
aisee lara muulize mama lara 1 stori zake basi halaf tujuze basi tunataka kujua vituko vyake usisahau.
 
Back
Top Bottom