Grand Master Dulla
JF-Expert Member
- Jul 20, 2012
- 411
- 146
- Thread starter
- #41
I see huyu chalii alikuwa ni noma, yeye pamoja na ndugu zake kina Shedadi, Ayat na dada yao alikuwa anaitwa Chola. Kwao mtu aliyekuwa ametulia alikuwa mdogo wao alikuwa anaitwa Ally Tungu. Utemi wa kuchukua mademu kinguvu alikuwa haufanyii disco tu bali hata mitaani, akimtaka demu halafu akatae maisha yake yatakuwa magumu sana hivyo wengi walikuwa wanakubali yaishe.
Alipigwa risasi na dereva wa lori baada ya kusimama mbele ya lori hilo na kulizuia lisiondoke mpaka atake yeye, akamkuta mzee wa kihehe amedata zaidi yake akamuwasha. Kaka yake Ayat alifariki kwenye tukio la ujambazi.
Nakumbuka siku moja disco alikuja akakuta watoto kibao ambao walikuwa na kiingilio pungufu wako nje akawaambia leteni hela mlizonazo nitawaongezea muingie wote. Basi watoto wakampa hela zote baada ya hapo jamaa akazama ndani (na alikuwa halipi kiingilio, muulizeni Papaa Felicia Chaula wa FM academia anamfahamu vizuri).
Wale watoto wakawafuata Polisi wa patrol wakamshitaki. Polisi kuja jamaa akatoka akawaambia kwa ukali kuwa wasimsumbue yuko kwenye starehe zake kama wana shida naye wamfuate kesho, Polisi wakaondoka wamenywea. Dah!
Beefinjector tupe tupe baba tupe stori zake inaelekea unamjua vizuri sana,jina lake kamili alikuwa anaitwa nani mana hilo cool 9 ni la kizungu? chansela,selemani mwarabu wote hao unawajua?