Ni nani Dr. William Mgimwa?

huyu jamaa hamna kitu, tunaletewa msomi wa IFM diploma alafu tunaambiwa doctor...uchaguzi huu umezingatia nini lakini? sijui, labda tuone delivery yake itakavyokuwa.
Wapendwa ma great thinker naomba mnielimishe maswali yafuatayo: 1. Je chuo Kikuu cha IFM au MZUMBE hakiwezi kutoa viongozi wa juu ktk nchi hii mpaka awe ametoka UDSM. 2. Hao mliowasifia na ma CV makubwa na wametoka UDSM mkawageuka! 3. Je utendaji na uadilifu unatokana na chuo kikuu mtu alichosoma?. 4. Kama ni hivyo hao walioonekana kukosa uadilifu au uwajibikaji ni product ya chuo gani?. Mwisho wale mnaokumbuka hadithi ya Daudi kutoka uchungaji kondoo, kumuua goliath hadi ufalme. Nani ajuae huyo Bwana aweza kuwa performer mzuri. Si wakati wa kumkatisha tamaa na kumhukumu ila ni kusimama pamoja, kumsaidia inapobidi kama tuna mapenzi mema ya kweli na nchi yetu. KWA MSAADA WA MUNGU TUTATENDA MAKUU.
 
Ebu tuone baada ya mwaka kama comment kali dhidi yake zitaendelea kuwa Valid!
 

wakuu ili ni jembe kishule na kiutendaji tumpe muda mtaona wenyewe,wakuu samahani lakini naomba mniwekee 'cv' ya mh mbowe na 'cv' ya mh lema!!
 

Mkuu umesema yote na kutetea kila kitu lakini hujasema alipata PhD ya kitu gani ? Kaisomea wapi ? Na kwa nini kwenye CV haiko ila ameitwa tu Dr? Ni katika kujua tunaongozwa na mtu wa aina gani hebu nisaidie kuelewa tafadhali
 
naona na cv yake kasoma seminari kwa hiyo anaweza kuwa na hofu ya Mungu pia..Tumuombee tu apate ushirikiano asije akaachwa kama pinda!
 
sina ufahamu sana lakini kwa uelewa wangu tumsubiri tuone lakini kigezo cha elimu naomba tusikitumie sana maana nimeona Dr. Prof. wengi sana kwenye baraza hili ila ukiangalia ndio hao hao wanaoipeleka nchi shimoni. kikubwa naona uadilifu, na akili ya kuzaliwa ni muhimu zaidi
 
Kwanza kabisaa kama ulivyo andika hapo kenye maandishi mekundu...naomba kukwambia IFM sio chuo kikuu...ni taasisi ya elimu ya juu, chuo kikuu kina sifa zake ambazo IFM haina...alafu hapa watu wanacho hoji ni udaktari wake unatokana na nini maana kwenye cv hujaoneshwa..pili uchapakazi wa mtu haufati chuo..tunajua kabisaa UDSM na TUMAINI ndio vyuo vinavyo toa wanasheria wazuri...na watu wa fedha(wahasibu, taxexperts, Finance mangers) wazuri wanatoka IAA, MZUMBE, NA IFM...nachotaka kusema hapa utendaji wa mtu hauangalii chuo alichosoma ila yeye mwenyewe!
 
Kazaliwa,Kalelewa na Kakulia benki, balance sheet anaielewa.Iwapo Key Performance Indicators zake zipo kiwango cha juu basi atatufikisha Kaanani.

Hivi mkuu unadhani MoF ni tawi la benki kwamba Waziri anaenda kuandaa financial statements na vitu vinavyofanana na hivyo?




Are you serious?

Yaani JF haina opportunity ya kudiscuss watu waliopewa madaraka makubwa kama huyo baba atakayekuwa anaongoza treasury yetu?

Kwa maelezo yao, basi umekuwa kioo halisi cha watanzania, wanaopanda bangi wakategemea kuvuna mahindi!!



Ndugu Hemed Maronda,

Kama kweli haya umeyasema ukiwa sober na unayaamini kwa moyo wako wote, basi una matatizo makubwa na unahitaji kuonana na psychological counsellor. Siwezi kuamini kwamba uko mentally sound na hujaona matatizo ya JK na kwamba bado unaamini anaweza kufanya miujiza yoyote kututoa hapa tulipozama kwenye matope!

Very pathetic in deed!!
 
Muacheni Dr Mgimwa afanye kazi, mpeni nafasi.Hii negativity haitatufikisha popote.
 
Naomba ufute kauli yako, TUMAINI kinatoa wanasheria vilaza..vilevile majority ya watu wanaoenda kusoma IFM, IAA na MZUMBE wanakuwa hawakupata credit nzuri Form VI za kuwawezesha kuingia UD kusoma BCOM, BA Economics nk. Tunao makazini, wengi wao ni mzigo tu hata huku maofisini.
 

SWEET GIRL tumemwelewa kupitia kwako; muhimu sheria za kodi zisibague watu yaani mtumishi wa umma unamtoza kodi kidogo yule wa sekta binafsi unamtoza kodi kubwa. Tuko nchi moja sheria zitende kazi sawa kwa wote; ni salamu zangu kupitia kwako SWEET GIRL hakikisha zinamfikia
 
Last edited by a moderator:

Hatuhitaji mtu mwenye roho nzuri kwani hawezi kuwa na roho hiyo kwa kila mtanzania, Uchapakazi mzuri tunao uhitaji ni kwa nafasi aliyopewa sasa. Siwezi kuamini kwamba wakati wa uteuzi wa Mustapha Mkulo Rais hakuwa ameyatambua maadili na uchapakazi wake. Uwajibikaji kuanzia ngazi za juu ndicho kitakuwa kipimo chake kwa watanzania. Tumekuwa tukiwaona wawajibikaji wakati wakiwa mitaani lakini wakishapewa nyadhifa wanageuka na kuwa watumwa wa uwajibikaji kwa chama au viongozi wa juu .
Kuidhinisha memos zisizofuata misingi ya sheria ya kazi yake na kuburuzwa kwa maslahi ya wachache hakuta lisaidia Taifa. Kwa kuwa elimu yake ni ndogo tutegemee uzoefu wake katika kazi.
 
. Heshima yako greater thinker kwa ufafanuzi wako mzuri na wenye tija. Siku iwe njema kwako.
 
. Mkuu reformer hivi elimu ya CAG imekaa vipi? Amepitia chuo gani baada ya kumaliza kidato cha VI? Je hana uhusiano wowote na Mzumbe? Umeuonaje utendaji kazi wake? Je hakuna vilaza maofisini wanaotoka UDSM? Ni kweli waliopo ni wa Mzumbe na IFM tu?
 
. Mkuu reformer hivi elimu ya CAG imekaa vipi? Amepitia chuo gani baada ya kumaliza kidato cha VI? Je hana uhusiano wowote na Mzumbe? Umeuonaje utendaji kazi wake? Je hakuna vilaza maofisini wanaotoka UDSM? Ni kweli waliopo ni wa Mzumbe na IFM tu?
 

Tuambia na Phd toka chuo gani?fake toka Mzumbe?
 

Haya uliyoyaandika umetumia data zipi ...Kwa taarifa yako watu wengi waliamini Ud ndio kilikuwa chuo bora kwa upande wa sheria...lakini hata kukiweka kati ya vyuo vinavyotoa wanasheria bora tanzania nimekipendelea...fuatilia matokeo ya chuo cha sheria (shool of law) uone jinsi gani ni wanafunzi wa chuo kipi wanafaulu...turudi kwa IFM IAA na MZUMBE...mimi mwenyewe nimekuwa kwenye majopo ya interview, nime supervise wanafunzi wengi tu wa field na nimefanya kazi katika uwanda waUhasibu na usimamizi wa fedha..hakuna product mbovu kama zinazotolewa na UD na UDOM pamoja na wengi wao kuwa na GPA za maana...na hakuna wanafunzi wazuri kama wa IAA na Mzumbe pamoja na IFM, ingawa IFM nao sio wazuri kiivyo..naomba ujue UD sasa hivi kinasimamiwa na jina tu fanya utafiti na sio ushabiki...nway nilikuwa nakueleza tu lakini jua kuwa mjadala ulikuwa wa waziri mpya wa fedha sio vyuo vikuuu!
 
NB: siku zote jua kufanya vizuri form six sio kufanya vizuri chuoni, na kwa taarifa yako wanfunzi wengi wazuri huwa hawafanyi vizuri formsix kwa sababu system iliyopo haiwafevi!
 
. Mkuu reformer hivi elimu ya CAG imekaa vipi? Amepitia chuo gani baada ya kumaliza kidato cha VI? Je hana uhusiano wowote na Mzumbe? Umeuonaje utendaji kazi wake? Je hakuna vilaza maofisini wanaotoka UDSM? Ni kweli waliopo ni wa Mzumbe na IFM tu?
Read between lines usikurupuke tu..I said majority of them I did not say all of them
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…