Rama N Ally
New Member
- Jun 8, 2021
- 2
- 3
Wanaotaka katiba mpya na wasioitaka wote ni watanzania. Katiba mpya siyo chokochoko wala chanzo Cha uhasama, isiwe chanzo cha machafuko au kupeana majina mabaya kama ya usaliti, adui wa maendeleo, kutumika na ubeberu, udikteta , n.k. Hoja za pande zote ziheshimiwe na kuwekwa mezani.
Ni muhimu kushindana kwa hoja katika kuidai au kuipinga katiba mpya na Wala si kutishana, kuvunjiana heshima au kusagiana kunguni kwa pande zote mbili. Wanaoipinga waje na hoja madhubuti na wanaoidai waje na hoja madhubuti pia.
Ni muhimu kushindana kwa hoja katika kuidai au kuipinga katiba mpya na Wala si kutishana, kuvunjiana heshima au kusagiana kunguni kwa pande zote mbili. Wanaoipinga waje na hoja madhubuti na wanaoidai waje na hoja madhubuti pia.