Hivi huu muda ni upi wa kujua ndo Bwana atanipa huyu mke?Ufafanuzi plz!Shagiguku ndo mawazo gani hayo jamani. Mmmh mke mwema kwako anatoka kwa bwana Mungu, hebu tulia na Mungu, wakati ukifika utamuona tu.
Da Pretty umenikumbusha hapa kituoni ninapopandia daladala kuna dada nakutana nae kila asubuhi nampenda kweli wallahi ila muda mchache wa kumweleza:dance:, kesho nitaanza kampeni rasmiKwenye kituo unachopandia daladala kwenda ofcn au ndani ya daladala,
wa mgahawani muda wa lunch wazushi kibao!
Kama hupandi daladala we jaribu kutupia macho ukiwa wapita,hasa asubuhi.
Dah! Kazi kweli kweli, sasa hivi labda uende chuo cha kutongoza maana inaonyesha we ni bonge la mshamba kwenye hizi fani(jokes bwana) usijali mjomba haya mambo huwa yanakuja automatically, cha muhimu we jichanganye na watu wote katika sehemu zao walipo mf chuch, kazini na uonyeshe upendo kwa hawa viumbe(unawatafuta) na uonyeshe unawajali.
Inaelekea upo serious sana hata njiani ukikutana na warembo huonyeshi uso wa bashasha (sio bashasha la kulazimisha), mkuu hakuna formula wapo wengi tu kuanzia unapotoka tu mlangoni kwako, unaokutana nao njiani, kwenye vituo vya daladala mpaka maeneo yako ya mishemishe kikubwa na wewe uchamke kiasi kwamba hata uwepo wako watu wawe wanautambua na ukiwa haupo watu wanakuulizia (ukianzia hapo mambo mengine yanafuata, yaani huna hata madada wa hiari? au kwenye group discussion nako ulikuwa hushiriki? na kama unashiriki kulikuwa hakuna hata somo moja ambalo mchango wako ulikuwa unaonekana kiasi kwamba ukajenga interest ya kuongeza marafiki wengi mwisho wa siku kwenye ku-network ukaanza kukutana na sampuli tofauti tofauti humo humo unaweza kubahatisha kwa kuanza na urafiki then UCHUMBA)
Kwani Mimi sio mtakatifu???
Wana JF nisaidieni kwa hili....
Hivi karibuni nimeanza kazi baada ya kuhitimu chuo. Kipindi nikiwa nasoma nilikuwa sijihusishi na mambo ya mapenzi na wala nilikuwa sina mchumba kwa wakati huo. Hivi sasa ndo naanza maisha ila sijafahamu mazingira ambayo nikipitapita ntapata mchumba. Najua humu ndani kuna wanandoa, wenye wapenzi pamoja na wengine wenye uzoefu nadhani baadhi watakuwa walipitia huku. Jamani wana JF naombeni msaada wenu wa mawazo.