Ni mahafali ya binti yangu

Ni mahafali ya binti yangu

Kutengana siyo historia nzuri, kama katika ukoo wako mama yako au bibi walitengani, jua fika mbeleni yatatokea kwa binti yako! Dawa ni kuomba huo mkosi kizungu tunasema’Curse’ ivunjwe kwa sala maalum bila malipo wala mchango(free of charge)ukihitaji ushauri sema.
Mmeshaanza mambo yenu na nyie sasa..khaaa
 
Salamu sana,

Poleni na majukumu ya kujenga taifa.

Kwanza kabisa napenda kumshukuru sana Mungu Kwa ajili ya binti yangu ambaye amehitimu chuo. Alisoma shahada yake Chuo Cha Usafirishaji Ubungo.

Lengo kubwa la Uzi huu ni kutoa neno la shukrani Kwa wale wote walionitia moyo hasa wakati ule alipokosa mkopo. Namshukuru sana Katibu Mkuu wizara ya elimu ambaye niliingia ofisini kwake nikajieleza na akanishauri, hata hivyo mwaka wa pili alifanikiwa kupata mkopo.


Wapendwa, kwa mapenzi mema kabisa nawakaribisha kwenye mahafali hayo 13/1/2018. Njoo hata tupate soda tu. Endapo utajaliwa kuja niambie ili nikupe simu namba.

Mtakaopenda kutununulia soda pia karibuni.

Ni mbali sana Mungu ametutoa. Nina ushuhuda wa kipekee kwani huyu binti akiwa nursery school ndipo tulipotengana na baba yake ila Mungu hakututupa. Kila hatua amekuwa nasi.

Karibuni.

Mkinitukana nitalia.
Hongera mama mkwe. Posa inaruhusiwa?
 
Umtafute mwenyewe sasa,
PM nikija ni kufuata hela ya soda tu,
Mmmmh mama kama nakuona hiviii, huyu kasema mahari umeitikia chapchap lkn Mimi nimeyekwambia Niko mweuPE, sina pesa wala ajira ila nahtaj mwanao HUJANIJIBU ATA !, LOL kwel mkono mtupu haulambwi na PESA NDO karibu @ KITU.Haya mama.Usjar
 
Mmmmh mama kama nakuona hiviii, huyu kasema mahari umeitikia chapchap lkn Mimi nimeyekwambia Niko mweuPE, sina pesa wala ajira ila nahtaj mwanao HUJANIJIBU ATA !, LOL kwel mkono mtupu haulambwi na PESA NDO karibu @ KITU.Haya mama.Usjar
Jiamini tu mwanangu, mbona uko vizuri tu;
hata mbuyu ulianza kama mchicha.
 
Hamna mtu aliyegusia suala la ajira wengi ni pongezi na marriage tuu. Kweli vyuma....
 
Kweli ajira kwake muhimu sana,
baada ya mahafali nitarudi na uzi wa kuomba mwenye
kuweza kumsaidia ili apate ajira,
amesoma Logistic and transport management.
Najuwa JF ni kisima binti yangu atapata kazi tu.

Hamna mtu aliyegusia suala la ajira wengi ni pongezi na marriage tuu. Kweli vyuma....
 
Hongera mamndenyi kwa ujasiri wa kupambana
Ila haina haja ya kujuta yaliyotokea huko awali maisha yanasonga mbele daima
Mpe hongera mjomba kwa kupata elimu
 
Back
Top Bottom