Ni maandamano au ni mapinduzi?

Ni maandamano au ni mapinduzi?

Wabongo bwana, kweli CCM imewafifisha akili! Sasa kwa nini serikali itumie nguvu zote hizi wakati tumeaminishwa kuwa serikali ya awamu hii inapendwa sana kuliko awamu zilizotangulia. Na je hao 'wachache' wasioipenda wakiachwa waandamane na kuongozwa na poilisi ili waeleze wanachotaka kueleza kuna ubaya au hasara gani? Mimi ningekuwa ninamshauri mtukufu asiyejaribiwa, ningesema atoe amri kwa poiliccm kuhakikisha wanatoa ulinzi wa kutosha kwa waandamanaji po pote pale maandamano yanapopangwa kufanyika ili tusikie wanataka serikali ifanye nini. Sijui kwa nini CCm inaogopa mikutano ya hadhara na maandamano?
Sidhani kama kutakuwa na maandamano. Lakini ni vema kuonyesha uwezo wa walinzi wetu.

Ni sawa na kuishi kwenye eneo lisilo na uhalifu. Sio busara kuacha mlango wazi.

Weka kufuli kubwa mlangoni hivyo kwamba hata kama kungekuwa na mtu anaeshawishika ataipita tu nyumba yako kwa kuliona lile kufuli.
 
Hahahahahahaaaaaaa. Hapo mmeeleweka. Siku hiyo wanaume wa Kazi watakuwa na zana zote halali. subirini mkufilie mbali wakati huyo anayewahamasisha ananyonya koni huko majuu
Hao unaowategemea kuondoa hayo maandamano pia wamechoka na udictator uchwara
 
Sijamtisha mtu bali nimeeleza uhalisia. Fanyeni hayo mapinduzi dhen muone cha mtema kuni
Acha ujinga ww hata maisha unayoyaona ww sasahiv yasingeandaliwa na wakina mkwawa uaingeyakuta hiv leo hii tunawakumbuka kwa ushujaa wao na tunaofaidi ni cc kwahiyo watakufa watakaobaki watafaidi maisha kwani kuna nini acha uzembe ww
 
inaweza kuwa uelewa wako mdogo tu! maandamano si tu ya kupinga kitu fulani. yapo pia maandamano kumpinga kiongozi fulani aliye madarakani na yakawa na lengo la kumwambia aliye madarakani tunataka uondoke madarakani. sasa mtawala atapima wanaotaka aondoke je wana hoja? na je ni wengi kuliko wanaotaka abak madarakani?? nani aliye kwambia maandamano ni kuomba kupunguzwa kwa bei ya sukari?

kiufupi maandamano ya kumpinga rais aliye madarakani yanaruhusiwa tena kwa tangazo kabisa tunaandamana ili aondoke rais madarakani.
 
Unachotakiwa kujiuliza wewe unakwenda kushiriki mapinduzi au unakwenda kushiriki maandamano? kama ni mapinduzi lazima silaha za moto zitakukabili
Kwa misri waandamanaji walikua na silaha mbona mubarak alitoka na huku itakua hivyo hivyo
 
Ndiyo maana serikali imerudisha JKT ili watanzania wapate elimu zaidi kuhusu nchi na utawala na uhalali wake. JKT tulifundishwa somo la silaha kwamba; Bunduki imetengenezwa kwa dhumuni la kumuua binadamu.mwisho wa kunukuu.Maelezo ya Lizbon yako sawa kabisa.Ukija kimapinduzi maana yake utadhibitiwa kwa silaha za moto ambazo madhumuni yake hutumika kumuua binadamu. Mange na kundi lake hawakupitia JKT hawajui ni wakati gani askari hubadilika na kuwa mnyama, wasubiri hiyo tarehe waliyoitaja watashuhudia askari wanavyobadilika ktk kuhakikisha wanawalinda wananchi watii sheria
Watawalinda au watawaua wananchi? Kwani sasa hivi hawauawi raia? Hata sasa tunaumia sana Watanzania wenzetu kuuawa na wengine kutekwa na kuteswa.
 
Wadau, amani iwe kwenu.

Nimefuatilia baadhi ya mitandao ya kijamii hususan Instagram na Telegram kuhusu haya makundi ya watu wanaotamani kuuangusha utawala wa Rais Magufuli. Kwa kiswahili wanasema kuwa hayo ni maandamano ya Amani. Ila kwa Kiingereza wanatamka Tanzania Revolution.

Kwa uelewa wangu, Maandamano tafsiri yake kwa Kiingereza ni Demonstration au Protests. Na Revolution maana yake kwa kiswahili ni Mapinduzi. Kwa uelewa wangu finyu, busara huweza kutumika katika kudeal na maandamano ikiwa ni pamoja na matumizi kiduchu ya nguvu. Ila Mapinduzi hapo lazima ujidhatiti kukabiliana nayo. Hapo silaha za moto na nzito hutumika na ni haki ya vyombo vya dola kutumia nguvu zote ili kulinda himaya dhidi ya maadui wa ndani na nje.

Kingine, Maandamano hudhibitiwa na Jeshi la Polisi. Ila Mapinduzi hapo wanaume wa kazi, JWTZ huingia mzigoni. Hapo silaha zinazotumika ni za moto tu. Hawajafundishwa kutumia TEAR GAS hao.

Kwa hiyo, ni vema wale wanaotamani kuona utawala wa Rais Magufuli unaangushwa wakatafakari upya ni nini hasa wanataka kufanya siku hiyo na nini madhara yake. Ni vema wakaweka wazi je wanataka kuandamana ama wanataka kufanya mapinduzi? Maandamano YES ila MAPINDUZI ni BIG NO. Watu wasije kufumuliwa vichwa wakifanya mapinduzi then wakaanza kulalamika kuwa jeshi la polisi na JWTZ wametumia nguvu ya ziada.
Kazi za jwtz ni kulinda watu,mali na nchi.

Endapo watu wanaandamana halafu ukawapiga risasi na huku wewe ni jwtz au police inabidi uache kazi,au ujieleze,kwanini unapiga watu risasi wakati kazi yako ni kulinda watu?

Majeshi yetu inabidi wapewe semina elekezi kuhusu wajibu wao
 
Kwa maana hiyo wale waliopiga risasi za moto kuke kinondoni walikua Jw kwenye mavazi ya polisi?

Na kwanini uite mapunduzi na sio maandamano??
 
Hapo si CCM tena. Hapo ni wazee wa kazi. JWTZ. Tena ni kitambo hawajatest mitambo yao
Tupo tayari kufa hata kuwa vilema, Historia ya nchi yetu itatukumbuka kwa mema na ninyi mtakumbukwa kwa unaa wenu.
 
Back
Top Bottom