Ni lini Frederick Sumaye amehamia CHADEMA?

Hot Lady

JF-Expert Member
Aug 7, 2014
1,035
638
Ijumaa kareem ndugu zangu.

Wakati Sumaye anatangaza kujivua uanachama wa CCM, alisema kuwa anaenda UKAWA lakini hakubainisha anaenda chama gani. Taarifa za ndani zilisema kuwa Sumaye anahamia NCCR na kwamba ndiye anayeandaliwa kugombea Urais ikiwa Lowasa ataishia njiani.

Hata hivyo, akiwa Mkoani Simiyu, Sumaye ameonekana amevaa jezi za CHADEMA hali inayoashiria kuwa na yeye amejiunga kwenye chama hicho. Nadhani Sumaye ameangalia upepo hasa kutokana na viongozi waandamizi wa NCCR Mageuzi kumjia juu Mwenyekiti wao na kutishia kujiondoa UKAWA. Wakati Sumaye akionekana amevaa jezi za CHADEMA, Lowasa ameendelea kugombea kuvaa gwanda za chama hicho ambapo amekuwa akibadilisha mashati huku kila analovaa kutoshabihiana kabisa na sare za chama chake.

Kwa mtazamo wangu, ikiwa Sumaye ameelekea CHADEMA, ni dhahiri kwamba viongozi wote wa UKAWA kwa sasa ni CHADEMA na kwamba hata huyu Mbatia kinachomuweka NCCR ni jimbo la Vunjo tu na baada ya Uchaguzi atatimkia huko kwa vile hana uwezo wa kushinda jimbo hilo

image.jpg image.jpg
 
kwa nini kila anayehama kutoka kaskazini anaenda chadema tu?
 
CHADEMA ni chama cha Wachagga na Wakaskazini. Toka mwanzo nilisema kuwa Sumaye hawezi kwenda NCCR. alikuwa anasubiri vuguvugu lipite tu ili asionekane kuwa kanunuliwa na Lowasa

Mkuu ebu tupe dondoo kinachojili mpaka sasa
 
Jamani acheni jazba hivi ni chama gani kikubwa Tanzania baada ya ccm ? tuwe wakweli kwa hilo sasa kujiunga chadema ni jambo la maana kwa sababu upinzani wa kweli unatoka kwa watu wanaojua maendeleo kama watu toka pande hiyo, mimi kwangu sina ubaguzi kwa hilo mwache mzee sumaye ajinafasi na bado wengi watatoka baada ya matokeo na tunaona mtasemaje?
 
Kumbe shida ni mavazi? Mwalimu JK Nyerere alikuwa chama gani? lete ushahidi wa picha wa nguo za kijani alizovaa wakati wa miaka takribani 24 ya uongozi wake!

The battle is on UKAWA vs CCM, the rest(ACT-Wazalendo, TLP, n.k) is just bakground noise. Na hawa wana Tshirt zao, mbona hukuuliza swali hilo wakati Prof. Lipumba alipovaa jezi hiyo hiyo? Na picha zililetwa hapa hapa jamvini?!!

Mnataka kufarakanisha mambo ila yahitaji akili ya ziada!
 
Wala hiyo Tshirt aliyovaa Sumaye sio ya CHADEMA, ni ya SuperSport!
 
Ijumaa kareem ndugu zangu.

Wakati Sumaye anatangaza kujivua uanachama wa CCM, alisema kuwa anaenda UKAWA lakini hakubainisha anaenda chama gani. Taarifa za ndani zilisema kuwa Sumaye anahamia NCCR na kwamba ndiye anayeandaliwa kugombea Urais ikiwa Lowasa ataishia njiani.

Hata hivyo, akiwa Mkoani Simiyu, Sumaye ameonekana amevaa jezi za CHADEMA hali inayoashiria kuwa na yeye amejiunga kwenye chama hicho. Nadhani Sumaye ameangalia upepo hasa kutokana na viongozi waandamizi wa NCCR Mageuzi kumjia juu Mwenyekiti wao na kutishia kujiondoa UKAWA. Wakati Sumaye akionekana amevaa jezi za CHADEMA, Lowasa ameendelea kugombea kuvaa gwanda za chama hicho ambapo amekuwa akibadilisha mashati huku kila analovaa kutoshabihiana kabisa na sare za chama chake.

Kwa mtazamo wangu, ikiwa Sumaye ameelekea CHADEMA, ni dhahiri kwamba viongozi wote wa UKAWA kwa sasa ni CHADEMA na kwamba hata huyu Mbatia kinachomuweka NCCR ni jimbo la Vunjo tu na baada ya Uchaguzi atatimkia huko kwa vile hana uwezo wa kushinda jimbo hilo

View attachment 288127View attachment 288129

Embu zoom hiyo picha uone nembo iliyopo kwenye shati halafu ujenge hoja vizuri..
 
CHADEMA ni chama cha Wachagga na Wakaskazini. Toka mwanzo nilisema kuwa Sumaye hawezi kwenda NCCR. alikuwa anasubiri vuguvugu lipite tu ili asionekane kuwa kanunuliwa na Lowasa

Acha uchochez ndugu yangu kwani sumaye ni mchagga? Huu ni uchochezi wakike hujui kitu kaimbe taarabu
 
kwa nini kila anayehama kutoka kaskazini anaenda chadema tu?
Jiulizeni na mkishapata majibu mjijibu wenyewe sisi tunasonga mbele na Lowassa. Hakuna kulala mpaka kielewekeeeeeee!!
 
Back
Top Bottom