Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 37,621
- 46,265
CHADEMA huwa mna utaratibu wa wowote wa kujadiliana na kukubaliana katika kutengeneza nyaraka zenu na miongozo mbalimbali ya kichama kwa mambo ambayo yatakuwa na umuhimu sana "consequential"?
Nakumbuka Slaa aliwahi kusema "list of shame"/orodha ya aibu ambayo ilimtaja Lowassa kama mmojawapo wa mafisadi wakubwa aliiandika mwenyewe, ndio maana hata akaondoka CHADEMA mlipomkaribisha Lowassa kugombea.
Nimewahi kumsikia Kitila Mkumbo pia akisema kwamba yeye ndiye aliyewaandika ilani yenu ya uchaguzi ya mwaka 2015.
Hivi karibuni niliona Mnyika akiwasilisha mapendekezo kuhusu miswaada ya tume ya uchaguzi na sheria za uchaguzi na mojawapo ya kipengele kilichozua sana mjadala ni uwepo wa wabunge wawili kila jimbo wa jinsia tofauti, baadhi members wa jukwaani wanasema Mnyika ndiye aliyeandika mapendekezo hayo.
Kama chama kikuu cha upinzani mnahitaji kujipambanua kama watu mnaofanya mambo kwa weledi na umakini mkubwa sana mkijua matokeo ya baadaye yanaweza kuwaathiri kwa namna nyingi. Lakini pia mmekiwa walegevu kutoa ufafanuzi makini na thabiti kwa mambo ambayo ni controversial.
Nakumbuka Slaa aliwahi kusema "list of shame"/orodha ya aibu ambayo ilimtaja Lowassa kama mmojawapo wa mafisadi wakubwa aliiandika mwenyewe, ndio maana hata akaondoka CHADEMA mlipomkaribisha Lowassa kugombea.
Nimewahi kumsikia Kitila Mkumbo pia akisema kwamba yeye ndiye aliyewaandika ilani yenu ya uchaguzi ya mwaka 2015.
Hivi karibuni niliona Mnyika akiwasilisha mapendekezo kuhusu miswaada ya tume ya uchaguzi na sheria za uchaguzi na mojawapo ya kipengele kilichozua sana mjadala ni uwepo wa wabunge wawili kila jimbo wa jinsia tofauti, baadhi members wa jukwaani wanasema Mnyika ndiye aliyeandika mapendekezo hayo.
Kama chama kikuu cha upinzani mnahitaji kujipambanua kama watu mnaofanya mambo kwa weledi na umakini mkubwa sana mkijua matokeo ya baadaye yanaweza kuwaathiri kwa namna nyingi. Lakini pia mmekiwa walegevu kutoa ufafanuzi makini na thabiti kwa mambo ambayo ni controversial.