Ni kweli USA supremacy ina collapse?

Twende taratibu

Unasema China hategemei soko la US na ulaya kuuza bidhaa zake, si ndio?

Unaweza ukaleta hapa Balanc of Trade baina ya US na China? Pia tutazame BoT ya China na Ulaya?

Naomba tuongee kwa facts ili sasa tujue ni nani muongo.
Kaka ningependa usome kwa utuo uelewe nini nakusudia,au wacha nikuweke sawa.
Kiufupi nachomaanisha USA sio soko pekee la China ingekua ni soko pekee kipindi Trump anawaongezea ushuru China ingechutama ila nayo ilidinda na USA ndio ikawafiki.
 
Mkuu haitaji rocket science kujua hili,ajaribu tu kufikiria kwenye ukoo yule mwenye utajili wakutisha na yule wakawaida ni nani mwenye ushawishi?.Sasa sijui mtu anakuaje na uchumi mkubwa afu asiwe na ushawishi!
Japan na Russia nani mwenye ushawishi kushinda mwenzake ? Korea kusini na Russia nani mwenye ushawishi kushinda mwenzake ? India na Russia nani mwenye ushawishi kushinda mwenzake ? Italy na Russia nani mwenye ushawishi kushinda mwenzake ? Canada na Russia nani mwenye ushawishi kushinda mwenzake ?
 
Hujapewa alichoandika ,kichwa kizito kama fenesi .
Amemaanisha freedom of worship iliyopo USA haipatikani sehemu yoyote dunia hii ,na hii inasaidia kuaccomodate watu toka backgrounds tofauti wahindu ,waislamu ,wakristo ,wabudha ,wapagani/atheists pia wanatambulika hata waabudu matambiko na washirikina pia wanauhuru huo pale USA .
 
Umelogwa wewe
 
Kisiasa China ni mwiko kuingilia sera za ndani za taifa lengine, serikali ya China kwa sera za nje ya China haziiruhusu China kuingilia mambo ya ndani ya mataifa mengine ndio maana China haina agenda kama za U.S.A za kulazimisha mataifa mbalimbali yaendane Kama U.S.A na mataifa ya magharibi China anafanya biashara na nchi yoyote pasipo kuingilia namna hiyo nchi inavyo jiendesha na hapa China amejipatia ushawishi mkubwa kwa sera zake za mambo ya nje hasa hasa Afrika , Asia na mataifa mbalimbali ya Amerika kusini.
 
Yaan haya mawazo mfu sijui hua mnayatoa wapi.. je Kuna dalili ya kuonesha USA anaenda kwanguka?
 
Unge elezea hoja yako katika lugha inayo faa ingekuwa na ujazo zaidi kuliko hiki ulicho fanya.
 
Sawa nimekuelewa kaka
 
kisiasa kwa nilivyofuatilia mm kaka China huwa inaheshimu sovereignity ya mataifa mengine.
Huwa haina kawaida ya kuishinikiza taifa ifanye inachotaka ndio ifanye nayo makubaliano eidha kibiashara au kimsaada wa kifedha kama afanyavyo USA mara watu wakubali ushoga,mara kufanya regime change akae kiongozi wanaomtaka wao n.k. Hii imefanya mataifa mengi yapende kujihusisha kidiplomasia na China kuliko USA.
China anachoangalia ni business tu kaka,ninyi kuweni madikteta ama uaneni yeye haimuhusu maana kila nchi ina sovereignity yake.
Pia China amejitahidi kujiunganisha na mataifa karibuni yote ya kimasikini ambayo yalitupwa mikono na USA na Western powers kijeshi na kibiashara kama vile Cuba,Fiji,mataifa ya ukanda wa Asian pacific na mataifa baadhi ya South America bila kusahau mataifa ya Carrebean.
North Korea unayoiona ina nguvu ya kufyatua makombora ni kwa usaidia wa China na hiyohiyo China ndio iliyoisaidia North Korea 1959 kumtwanga South korea na washirika wake kuanzia Jangsari wakati wa vita za mgawanyo za Kikorea.
kwa uelewa wangu kisiasa hapo ndipo napofaham jinsi China ilivyopiga hatua.
Dunia haipo Europe na America pekeake,Africa,South America,Asia,Carrebeans kote huko China ana ushawishi mkubwa sana palipo pagumu ni Western Europe ,Australia na America kaka ambako ushawishi bado.
 
Yaan haya mawazo mfu sijui hua mnayatoa wapi.. je Kuna dalili ya kuonesha USA anaenda kwanguka?
Yapo kaka,labda kudura ya Mungu imchague USA aendelee kubaki.
Kipindi cha nyuma kuna taifa lililokua linathubutu kumjibu USA kijeshi?Hapana ila sasa hivi mabwana wadogo wanamvuta sharubu USA mathalan North korea,Iran.
Kuna taifa lililokua linathubutu kuhoji vikwazo vya kiuchumi vitakavyotolewa na USA?Hapana ila sasa hivi yapo hayo mataifa pande zote duniani mpaka za kimasikini huku wakimuona China atawabeba,HAIMAANISHI KWAMBA USA BADO HAINA NGUVU NA USHAWISHI!HAPANA ILA USA SIKU HIZI INAKUA CHALLENGED KILA KONA KAKA.
Na ukiona wewe mzee unaanza kuwa challenged na walio chini yako jua washabaini wapi panatobo wapenyeze dole.
 
Kumshinda U.S.A sio kitu chepesi Kama baadhi ya watu wanavyo dhani inahitajika akili nyingi zaidi kuliko nguvu nyingi hata China wenyewe hili mara kadhaa kupitia wachambuzi nguli wa kisiasa wa CGTN China wamekuwa wakisema mara kadhaa ninapo kuwa nawa fuatialia target ya China kuifikia uchumi U.S.A ni mwaka 2050 hapo sio kuipita bali ni kuifikia tu na Kuna mawili China inaweza kuifikia au kutoifikia kutokana na sababu mbalimbali hasa hasa ishi ya Taiwan ikiripuka na hii ndio risasi moja kuu U.S.A aliyo nayo kumdhibiti China kama wangelijua haya yanayo tokea sasa hivi U.S.A , U.K na Portugal ishi za Macau na Hongkong wasingekubali zirudi China kiurahisi vile ishu ya Taiwan nayo walijikanyanga hasa hasa U.S.A miaka ya 1971, 1978+ 1979 hapa kwa kweli kwenye hizi ishu Deng Xiaoping na Chairman Mao waliwazidi maarifa na ujanja viongozi wa U.k, Portugal na U.S.A . Wataalamu mbalimbali wa siasa za kimataifa wanasema kwa sasa hakuna ushindani hatari unaotokea Kama wa U.S.A na China hawa wana ushindani wa hatari katika maswala mbalimbali ya kiuchumi, Kisayansi/kiteknolojia na kibiashara makampuni mbalimbali ya U.S.A yanajimegua taratibu kutoka China na makampuni makubwa ya kiserikali kutoka China Yana jitoa kutoka katika soko la hisa la marekani , China kapigwa ban na U.S.A kwenye Chips serikali ya China wamewekeza kiwanda chao kupitia mwanachama wao wa CPC Kama kawaida yao kudevelop Chips making na Sasa hivi kiwanda cha China SMIC kinakuja kwa kasi balaa katika ulimwengu wa Chips mpaka kimekuwa tishio kwa TSMC na marekani , Belt& Road Initiative[ 1 tln dollar wamewekeza ] nao marekani na G- 7 nao wanakuja na ya kwao [ 600bln dollar wamewekeza ] , kwenye space race napo China na Marekani wanatifuana balaa hii Vita ya kibiashara kati ya marekani na China inafurahisha na kuelimisha ukiifuatilia lakini kwa hali inavyo kwenda lazima kuna mmoja kati yao atapotezwa balaa.
 
Hapa nmekupata mkuu kwamba uchumi hau determine ushawishi wa nchi husika
 
Hapa nmekupata mkuu kwamba uchumi hau determine ushawishi wa nchi husika
Nilicho kuwa na maanisha ushawishi haujengwi na uchumi tu kuna sababu zengine pia zinajenga ushawishi mfano ni sisi hapa Tanzania hatuna uchumi mkubwa kama Kenya Ila historia yetu iliyo jengwa na mwalimu wakati wa ukombozi wa Afrika hasa hasa Kusini mwa jangwa la sahara hakuna nchi kwa hapa EAC inayotufikia sisi Kiushawishi na kuaminika .
 
Yaan haya mawazo mfu sijui hua mnayatoa wapi.. je Kuna dalili ya kuonesha USA anaenda kwanguka?
Kama hujaiona hutaiona tena. Hata Rome... Egypt... Greece Ottoman Hakuna aliyeona but they all fall. Now us Ina sign zote za fallen empire. Sema mahaba na ushabiki unawapa watu upofu.
 
Tatizo wengi wanadhani ikija ishu ya kuiangusha USA wanaiwaza China na Russia yaani wanawaza vita tu. Wanasahau watu muhimu sana "Watu walioiopandisha USA hapo ilipo" then same people walioingiza Ujamaa China kupitia Mao... Karl max the blood descendant WA Ile familia.... They have used USA enough and now it's time for other to take the lead. We ushajiuliza miaka kibao nyuma China alikuwa Hana hata misuli ya kutunisha wao now hata Ana uwezo WA kuleta mikwara hiyo... Anaipata wapi kiburi hiko???? All of then are puppets... And it will be like the owner of two dogs decided to make then fight and him and his friends wakae pembeni wakifurahi na wakipata mvinyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…