Hivi kwa nini tunajitoa ufahamu kwa kuwashutumu wanaompinga Prof, ilhali taasisi za serikali yake, CAG na PCCB wameona amefanya mambo kwa mapungufu makubwa? Je, tunajaribu kuzidharau taasisi hizi na kuona kwamba wabunge ndiyo wa kulaumiwa?
Kuisakama kamati ya PAC juu ya ripoti yao ambayo ilijadiliwa na bunge zima na kuwekewa maazimio ya maridhiano ni kujifanya hatuelewi kabisa kilichotokea, matokeo yake tunajenga visasi kwa mtu mmoja mmoja aliyekuwepo kwenye kamati ile...mtazamo wa aina hii juu ya mambo ya kitaifa unatia shaka sana uwezo wetu wa kuchambua mambo.
Zaidi ya hayo, uwaziri ni political post, kwa sababu hakuiomba kazi hiyo, basi asiondoke kwa kuvunjiwa heshima...tukumbuke kwamba Bunge limependekeza kwa Rais amuwajibishe, na hatua za kisheria ndiyo zitakazoonesha sasa ana makosa gani...akiwa hana hatia si ataendelea kupeta sehemu nyingine? Hivi Kuwa mchapakazi lazima uwe waziri?
Wenzetu tuhuma tu zinatosha kumfanya mtu aachie ngazi, sasa sisi ni vile hatuna mishipa ya aibu au nini hasa? Haya mambo yako wazi, watu tunaamua tu kuendesha mijadala humu kama vile PCCB, CAG, PAC na Bunge vyote vilikosea...kama hatuamini taasisi hizi tumwamini nani?