Ni kweli Prof Muhongo anahujumiwa?

Ni kweli Prof Muhongo anahujumiwa?

Stanley.

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2011
Posts
659
Reaction score
302
Toka Bunge limalize kazi yake juu ya Escrow kumekuwa na mijadala mizito hasa humu Jf huku wengi wakimtetea Waziri wa Nishati na Madini Prof Muhongo kwamba anasakamwa na baadhi ya watu wenye maslahi binafsi. Sasa kwa wale mliofanikiwa kusoma vizuri taarifa ya CAG na kupitia ile ya PAC na mjadala wa bungeni. Tuwekeeni makosa ya mh Prof Mhongo na wale mnaoamini hana makosa toeni utetezi. Kama hujaelewa vema suala la Escrow usichangie usichojua. Karibuni wajuzi.
 
Hahujumiwi, bali amefanikisha lengo lake.

kama wanasiasa wanavyosema hajawahi kuuza hata mapera lakini sasa huenda tunaweza kumuita bilionea.

Akawatambie wamafunzi sasa akiwa ameshika chaki mbele ya ubao; maana hiyo ndio kazi pekee wanaweza kuifanya kiufanisi maprofesa wa Afrika
 
Makosa ya Prof ni kulidanganya Bunge kwa kusema fedha za ESCROW si za Umma, na kauli hii iliirudia mara kadhaa, ninaamini kwa kuwa sakata hili ni la muda na limejitokeza Bungeni mara kadhaa hivyo Viongozi wote waliohusika walikuwa wakikutana na kujadili suala hili na maelezo ya Prof kung'ang'ania kauli yake ni dhahiri ilikuwa kutii kiapo chake cha kutokutoa siri. na ndio sababu niionayo mimi AG alisema atasimama na wote waliofuata ushauri wake. Binafsi hilo ndilo nilionalo kosa lake kutii kiapo kwenye hamna. Ama kwa upande wa pili naona anasakamwa na wivu, chuki naye kwa jinsi alivyoweza kuwanyima wafanyabiashara mwanya wa kujitwalia rasilimali zetu kwa manufaa yao binafsi, pia ile kujiamini kupita kiasi kupelekea kuwapa makuvu live baadhi yao na baadhi ya wanasiasa wanaotumiwa na wafanyabiashara hao. Lakini kwa utendaji kazi ndani ya wizara tangu wizara hii ianzishwe ame-transform mambo mengi ya wizara kulko mawaziri waliomtangulia.
 
Toka Bunge limalize kazi yake juu ya Escrow kumekuwa na mijadala mizito hasa humu Jf huku wengi wakimtetea Waziri wa Nishati na Madini Prof Muhongo kwamba anasakamwa na baadhi ya watu wenye maslahi binafsi. Sasa kwa wale mliofanikiwa kusoma vizuri taarifa ya CAG na kupitia ile ya PAC na mjadala wa bungeni. Tuwekeeni makosa ya mh Prof Mhongo na wale mnaoamini hana makosa toeni utetezi. Kama hujaelewa vema suala la Escrow usichangie usichojua. Karibuni wajuzi.
hajahujumiwa kajihujumu kwa kudhani utaalamu wa miamba ndiyo kila kitu hapa duniani
 
Muhongo amaziba mianya ya wizi ya wafanyabishara wasiokuwa na uzalendo ndiyo maana kutwa wanamtafuta angalia mengi na mkono wanavyomwandama kisa tu mengi amekosa kitaru cha gesi na mkono kuondolewa kuwa advocate wa Tanesco baada ya kubaini kuwa anafanyabishara badala ya kuitetea Tanesco.
 
Toka Bunge limalize kazi yake juu ya Escrow kumekuwa na mijadala mizito hasa humu Jf huku wengi wakimtetea Waziri wa Nishati na Madini Prof Muhongo kwamba anasakamwa na baadhi ya watu wenye maslahi binafsi. Sasa kwa wale mliofanikiwa kusoma vizuri taarifa ya CAG na kupitia ile ya PAC na mjadala wa bungeni. Tuwekeeni makosa ya mh Prof Mhongo na wale mnaoamini hana makosa toeni utetezi. Kama hujaelewa vema suala la Escrow usichangie usichojua. Karibuni wajuzi.

ukisoma hapa itakuongezea marifa zaidi.
[h=2]Ukiondoa sababu ya kutoelewana na Reginald Mengi, sijaona sababu ya Prof. Muhongo kung'oka[/h]
Wana jamvi, ni matumaini yangu kuwa bado mnaendelea kutafakari mapendekezo hovyo ya Kamati ya PAC yaliyozaa maazimio hovyo ya Bunge juu ya sakata la Akaunti ya ESCROW. Mjadala mkubwa hapa JF kwa sasa ni juu ya sababu ya msingi ya kuondolewa kwa baadhi ya mawaziri kwa kuhusika kwao na sakata la ESCROW achilia mbali utata uliogubika mwenendo mzima wa uchunguzi wake. Ni bahati mbaya sana Ripoti ya CAG haikuainisha makosa ya msingi ya kuondolewa kwa Waziri wa Nishati na Madini, Sospeter Muhongo au hata Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Eliakim Maswi. Hakika hawa jamaa nawaadimire sana kwenye kazi zao. Wameleta displine kwa shirika la umeme na wamevuruga sana miradi ya kifisadi ambayo ilikuwa inapoteza mapato mengi sana ya TANESCO.

Wadau, kuna msemo usemao kuwa mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Ni aibu kwa kamati ya PAC kupendekeza waziri na Katibu Mkuu wa Nishati na Madini wang'oke kwa sababu zisizoeleweka. Eti wanasema kuwa Waziri anaondolewa kwa kusema kwake uongo bungeni. Haya tuambieni, kauli aliyotoa Muhongo ni ile ile aliyotoa Waziri Mkuu Pinda kuwa fedha zile si mali ya serikali wala TANESCO bali ni mali ya IPTL. Pia Naibu Waziri Stephen Maselle alitoa kauli hiyo hiyo ambayo ilitokana na ruling ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Werema. Sasa hapo kosa la Muhongo na Maswi lipo wapi?

Sababu ya pili iliyoainishwa na akina Zitto eti ndo sababu ya Waziri Msomi tena aliyeliletea manufaa makubwa shirika na wizara kwa ujumla wanasema ni kuwa dalali. Eti kwa vile wamiliki wa IPTL na wa PAP walikutana ofisini kwake. Hakika inashangaza sana. Yaani waziri na Katibu Mkuu hawaruhusiwi kukutana na wawekezaji wawe fake au halali? Nani anatambua kuwa mwekezaji fulani ni fake au halali? Hakika inachelesha sana. Nimefuatilia mijadala juu ya sababu ya kuondolewa kwa Viongozi hawa hakika kila mmoja anajikanyaga.

Jamani ifike wakati tuwe wakweli kusema ukweli. Wengi waliopiga kelele ili Maswi na Muhongo waondoke ni wale wale ama waliwahi kukwaruzana hapo nyuma kama ilivyo kwa Ole Sendeka dhidi ya Muhongo, au Kafulila dhidi ya Maswi. Usitegemee kuwa hawa wabunge watakuwa mabalozi wa mahasimu wao.

Wengine wanaopiga kelele ni wale waliotajwa kula mlungula kutoka kwa Reginald Mengi. Tena hawa walikuwa wanaongea kwa jazba kubwa utafikiri wana uchungu kumbe wanatetea rushwa waliyokula. Binafsi hii ndo naona sababu ya msingi ya Muhongo na Maswi kuondolewa. Rushwa rushwa rushwa. Mbowe ananuka rushwa. Zitto ananuka rushwa. Kafulila ananuka rushwa. Mbatia ananuka rushwa. Mnyika ananuka rushwa. Ole sendeka ananuka rushwa. Serukamba ananuka rushwa nk nk. Ndo maana Spika wa Bunge amekemea sana wabunge kupewa fedha kutoka kwa wafanyabiashara ili wawasulubu Mawaziri. Hii ndiyo sababu ya msingi.
 
Muhongo amaziba mianya ya wizi ya wafanyabishara wasiokuwa na uzalendo ndiyo maana kutwa wanamtafuta angalia mengi na mkono wanavyomwandama kisa tu mengi amekosa kitaru cha gesi na mkono kuondolewa kuwa advocate wa Tanesco baada ya kubaini kuwa anafanyabishara badala ya kuitetea Tanesco.

Tena we ndio mtetezi wake sana. Nijibie hoja moja baada ya nyingine za PAC.
 
mmelipwa sh.ngapi
hatumtakiiiiii
aende huko alikokua mwanzo
profesa wa miamba si wa umeme
 
Hahujumiwi, bali amefanikisha lengo lake.

kama wanasiasa wanavyosema hajawahi kuuza hata mapera lakini sasa huenda tunaweza kumuita bilionea.

Akawatambie wamafunzi sasa akiwa ameshika chaki mbele ya ubao; maana hiyo ndio kazi pekee wanaweza kuifanya kiufanisi maprofesa wa Afrika
Chuki zenu na mengi kwa muhongo zitawafikisha pabaya sana ila mungu atasimama na muhongo daima hana kosa ni hujuma na fitina za wafanyabiashara mafisadi waliobanwa kuinyonya wizara ndiyo chanzo cha muhongo kuchukiwa.
 
ukisoma hapa itakuongezea marifa zaidi.
[h=2]Ukiondoa sababu ya kutoelewana na Reginald Mengi, sijaona sababu ya Prof. Muhongo kung'oka[/h]
Wana jamvi, ni matumaini yangu kuwa bado mnaendelea kutafakari mapendekezo hovyo ya Kamati ya PAC yaliyozaa maazimio hovyo ya Bunge juu ya sakata la Akaunti ya ESCROW. Mjadala mkubwa hapa JF kwa sasa ni juu ya sababu ya msingi ya kuondolewa kwa baadhi ya mawaziri kwa kuhusika kwao na sakata la ESCROW achilia mbali utata uliogubika mwenendo mzima wa uchunguzi wake. Ni bahati mbaya sana Ripoti ya CAG haikuainisha makosa ya msingi ya kuondolewa kwa Waziri wa Nishati na Madini, Sospeter Muhongo au hata Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Eliakim Maswi. Hakika hawa jamaa nawaadimire sana kwenye kazi zao. Wameleta displine kwa shirika la umeme na wamevuruga sana miradi ya kifisadi ambayo ilikuwa inapoteza mapato mengi sana ya TANESCO.

Wadau, kuna msemo usemao kuwa mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Ni aibu kwa kamati ya PAC kupendekeza waziri na Katibu Mkuu wa Nishati na Madini wang'oke kwa sababu zisizoeleweka. Eti wanasema kuwa Waziri anaondolewa kwa kusema kwake uongo bungeni. Haya tuambieni, kauli aliyotoa Muhongo ni ile ile aliyotoa Waziri Mkuu Pinda kuwa fedha zile si mali ya serikali wala TANESCO bali ni mali ya IPTL. Pia Naibu Waziri Stephen Maselle alitoa kauli hiyo hiyo ambayo ilitokana na ruling ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Werema. Sasa hapo kosa la Muhongo na Maswi lipo wapi?

Sababu ya pili iliyoainishwa na akina Zitto eti ndo sababu ya Waziri Msomi tena aliyeliletea manufaa makubwa shirika na wizara kwa ujumla wanasema ni kuwa dalali. Eti kwa vile wamiliki wa IPTL na wa PAP walikutana ofisini kwake. Hakika inashangaza sana. Yaani waziri na Katibu Mkuu hawaruhusiwi kukutana na wawekezaji wawe fake au halali? Nani anatambua kuwa mwekezaji fulani ni fake au halali? Hakika inachelesha sana. Nimefuatilia mijadala juu ya sababu ya kuondolewa kwa Viongozi hawa hakika kila mmoja anajikanyaga.

Jamani ifike wakati tuwe wakweli kusema ukweli. Wengi waliopiga kelele ili Maswi na Muhongo waondoke ni wale wale ama waliwahi kukwaruzana hapo nyuma kama ilivyo kwa Ole Sendeka dhidi ya Muhongo, au Kafulila dhidi ya Maswi. Usitegemee kuwa hawa wabunge watakuwa mabalozi wa mahasimu wao.

Wengine wanaopiga kelele ni wale waliotajwa kula mlungula kutoka kwa Reginald Mengi. Tena hawa walikuwa wanaongea kwa jazba kubwa utafikiri wana uchungu kumbe wanatetea rushwa waliyokula. Binafsi hii ndo naona sababu ya msingi ya Muhongo na Maswi kuondolewa. Rushwa rushwa rushwa. Mbowe ananuka rushwa. Zitto ananuka rushwa. Kafulila ananuka rushwa. Mbatia ananuka rushwa. Mnyika ananuka rushwa. Ole sendeka ananuka rushwa. Serukamba ananuka rushwa nk nk. Ndo maana Spika wa Bunge amekemea sana wabunge kupewa fedha kutoka kwa wafanyabiashara ili wawasulubu Mawaziri. Hii ndiyo sababu ya msingi.

Nimekusoma ngoja tupate na mawazo ya wengine kisha tafakuri inahitajika. Mambo haya ni makubwa yanatikisa nchi.
 
Toka Bunge limalize kazi yake juu ya Escrow kumekuwa na mijadala mizito hasa humu Jf huku wengi wakimtetea Waziri wa Nishati na Madini Prof Muhongo kwamba anasakamwa na baadhi ya watu wenye maslahi binafsi. Sasa kwa wale mliofanikiwa kusoma vizuri taarifa ya CAG na kupitia ile ya PAC na mjadala wa bungeni. Tuwekeeni makosa ya mh Prof Mhongo na wale mnaoamini hana makosa toeni utetezi. Kama hujaelewa vema suala la Escrow usichangie usichojua. Karibuni wajuzi.

Ni wazi wewe ndio hukuelewa wala kufatilia swala la Escrow ndio maana umeuliza swali hill!

Nitakukumbusha kosa moja kwa kukudokeza kuna Sehemu Waziri Muhongo alitakiwa kutia sign kabla ya jambo Fulani kufanyika na hakufanya hivyo na bado alikuwa mbishi wakati she ria ilikuwa ina mtaka kufanya hi yo...pengine alifanya hivyo kwa makusudi!
 
Muhongo amewabana mafisadi wakiokuwa wana makampuni binafsi ya kutoa huduma tanesco kwa njia za kifisadi
 
Tena we ndio mtetezi wake sana. Nijibie hoja moja baada ya nyingine za PAC.
Unataka nikujibie hoja gani,wakati nikisubiri hoja unayotaka nijibu niambie muhongo wapi ambapo ametenda kosa kama unatumia akili yako vizuri bila kufungwa na mafisadi unaweza sema kwa uhuru kabisa kosa lipi kafanya profesa muhongo?
 
Ni wazi wewe ndio hukuelewa wala kufatilia swala la Escrow ndio maana umeuliza swali hill!

Nitakukumbusha kosa moja kwa kukudokeza kuna Sehemu Waziri Muhongo alitakiwa kutia sign kabla ya jambo Fulani kufanyika na hakufanya hivyo na bado alikuwa mbishi wakati she ria ilikuwa ina mtaka kufanya hi yo...pengine alifanya hivyo kwa makusudi!
wewe unajulikana ni team Lowasa. Huna jipya
 
Nimekusoma ngoja tupate na mawazo ya wengine kisha tafakuri inahitajika. Mambo haya ni makubwa yanatikisa nchi.
Hakika Mkuu. Mengi anaiweka nchi yetu kwenye wasiwasi mkubwa
 
Unataka nikujibie hoja gani,wakati nikisubiri hoja unayotaka nijibu niambie muhongo wapi ambapo ametenda kosa kama unatumia akili yako vizuri bila kufungwa na mafisadi unaweza sema kwa uhuru kabisa kosa lipi kafanya profesa muhongo?
Mkuu, hakika kwenye hili suala la escrow kuna watu wanajitoa ufahamu kabisa
 
Back
Top Bottom