Ni kweli Nelson Mandela alifia gerezani 1985?

Babu Kijiwe

JF-Expert Member
Mar 31, 2010
4,762
4,576
Habari zenu wadau, katika pitapita zangu nimekutana na mwandishi mmoja anayedai kuwa mtu anayefahamika kwa jina la Nelson Mandela, si huyu tunaye mfahamu sisi, Nelson original alifia jela mwaka 1985. Kwa mujibu wa maelezo yake nikwamba huyu tunaye mfahamu alitafutwa mtu anayeendana naye kidogo na alilazimishwa kutoa talaka kwa Winnie Mandela maana wangekaa pamoja kwa muda mwanamama huyu angejua kuwa hakuwa Mandela Original.

Inasemekana mwanamuziki Johnny Clegg alishawahi pia kuimba kitu hiki katika wimbo wake wa "Asimbonanga" yaani hatujamwona yeye. Kwenye wimbo huo kuna maneno Asimbonang' uMandela thina akimaanisha hatujamwona Mandela Laph'ekhona - mahali alipo Laph'ehleli - mahali alipo zikwa. Wimbo huu ulitoka mwaka 1987.

Nani aliyetolewa gerezani 1990?

Inasemekana ni mtu ajulikanaye kwa jina la Gibson Makanda ambaye alipelekwa katika gereza la Pollsmor mwezi May mwaka 1985 na akiwa huko alifanyiwa plastic surgery iliyofanywa na timu ya madaktari wachache toka London Uingereza, mara baada ya zoezi hilo kufanikiwa alipatiwa mazoezi ya kuongea na kutembea kama Nelson Mandela mpaka alipo fuzu ndipo mpango wa kumtoa ukatekelezwa ndomaana hata baada yakutoka alilegeza sana masharti kwa watu weupe.

Nilipitia pia vyanzo mbalimbali mtandaoni nikakutana na zaidi ya waandishi 50 tofauti wakizungumzia juu ya Gibson Makanda kuigiza kama Nelson Mandela.

Je, nikweli Nelson Mandela alifariki mwaka 1985?

Nel.jpg
 
=============================
Ooh mwanangu dunia ina mambo,
sikia maneno,
nakwambiaka,
mupe roho yako Mola wako,
heshima kwa wazazi eee mwanangu.

Dunia hii mama lukumba lukumba,
dunia hii ina mambo mwendo wa ngamia,
dunia hii mama lukumba lukumba,
dunia hii ina mambo mwendo wa ngamia.

Chunga mwenjiyo atakudanganya,
kwa yote ile atapenda yeye,
kipenda roho kila mutu na yake,
yake ni yake na yako ni yako.

Dunia hii mama lukumba lukumba,
dunia hii ina mambo mwendo wa ngamia,
dunia hii mama lukumba lukumba,
dunia hii ina mambo mwendo wa ngamia.

Mwendo wa kobe maele maele,
mwendo wa chui kuwinda winda,
mwendo wa nyoka lukumba lukumba,
mwendo wa ngarama ah njia ya faradhi.

Dunia hii mama lukumba lukumba,
dunia hii ina mambo mwendo wa ngamia,
dunia hii mama lukumba lukumba,
dunia hii ina mambo mwendo wa ngamia.

Tabu na raha inakungojea,
inategemea akili yako,
tafutaaaa eh utapata eh,
kumbuka maneno nakwambiaka.

Dunia hii mama lukumba lukumba,
dunia hii ina mambo mwendo wa ngamia,
dunia hii mama lukumba lukumba,
dunia hii ina mambo mwendo wa ngamia.

By Lady Issa
 
We might need an Enquiry Commission into this, in order to establish arguments...if possible his body be exhumed and DNA testing be carried!...as it was with Palestinians' Yasser Arafat whose body was exhumed in 2013 for biochemistry testing to establish if the leaders' death was caused by polonium & lead poisoning or it's rather a natural death...ukweli ulipatikana with 3 teams conducting an investigation...sasa nini kishindikane kwa Madiba kama hizi fununu zina ukweli!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hili jambo ni fikirishi sana kwasababu misimamo na hoja aliyokuwa nayo Mandela wa kabla ya kufungwa na baada ya kutoka gerezani ni tofauti kabisa.

Pia swala la kumtaliki Winnie kwa hoja dhaifu aliyoitoa Mandela nayo ina ukakasi. Si Mandela yule aliyehamasisha umoja wa kitaifa na maridhiano kati ya makabira ya wanakusini katika kupambana na mkaburu kutoa taraka kwa Winnie bila ya kusikiliza ushauri kutoka kwa wazee na marafiki zake wa karibu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom