Ni kwanini ni vigumu kumngoja BWANA?

Ni kwanini ni vigumu kumngoja BWANA?

Ni kweli kumngoja Bwana imekuwa changamoto kwa wengi wetu, kama walivyotangulia kusema baadhi ya wajumbe, nami niongeze kidogo;

Wengi hatuna msingi wa neno la Mungu, tunataka Mungu afanye tunavyotaka kisha tuendelee na mambo yetu yanayomchukiza Mungu.

Vingine tunavitaka kwa tamaa zetu, Mungu akiangalia nia ya vile tunavitaka hivyo vitu anakaa kimya.

Na wale ambao tupo vizuri na Mungu, dunia inatuvuta kwa mengi mazuri, tunaona kama tunachelewa, na hatuishi katika viwango vinavyotakiwa.

Lakini ukiwa na subira/uvumilivu lazima uvune matunda mema, Mungu hutuandaa hatua kwa hatua kupokea yale tunayataka.

Ndio maana mtu anayemwamini Mungu akipata mafanikio, anaweza kudumu nayo muda mrefu kama ataendelea kuwa na uhusiano naye mzuri.

Muhimu ni kuamini Mungu wetu anatupa yale tunayoyahitaji kwake sawasawa na mapenzi yake na kwa wakati wake.

Mungu akubariki sana
Asante sana mkuu kwa ufafanuzi mzuri.....
 
Mkuu Kuna kitu Cha ziada unakijua, Kuna mahali nakwama ila kama ukiweza kuandika zaidi kuhusu hii comment utanisaidia.

Asante kwa mawazo yako
 
Asante kushukuru
Mkuu.... utanisaidia kwa hili....
Hivi ni mda gani unaotakiwa kumngoja BWANA!

>Kuna Ibrahim alisubiri mtoto karibu miaka 13
>Isack alisubiri miaka 13 kupata mtoto...
>Daudi alisubiri miaka 13 kuwa mfalme licha ya kutiwa mafuta na samweli.
>Yusuph alisubiri miaka 13...........kuwa waziri.
 
Presha ya jamii na mitandao ya kijamii ni kubwa mno, peer pressure inakulazimisha uonyeshe matokeo haraka, ilhali mchakato wa Mungu unahitaji usiri na utulivu.
Na hii imekuwa mtihani watu hujikuta wakiiba,kufanya biashara haramu,kudanga,kutembea na waume za watu.Uvumilivu unahitaji roho Mtakatifu pasi na hivyo itakuwa ngumu
 
Mkuu.... utanisaidia kwa hili....
Hivi ni mda gani unaotakiwa kumngoja BWANA!
Kwenye hili huwezi kuweka ukomo wa kumsubiri Bwana na ukiona muda huo umepita unachukua hatua nyingine iliyo kinyume na Mungu wako. Wapo watasubiri kwa siku, wiki, mwezi, miezi, mwaka na miaka.
 
Kwenye hili huwezi kuweka ukomo wa kumsubiri Bwana na ukiona muda huo umepita unachukua hatua nyingine iliyo kinyume na Mungu wako. Wapo watasubiri kwa siku, wiki, mwezi, miezi, mwaka na miaka.
Asante.... sana. mkuu¡ yote yanawezekana kwa jina la YESU......
 
"""Bali wao wamngojeao BWANA watapata nguvu mpya;,,,, watapanda juu kwa mbawa kama tai;,,, watapipiga mbio wala hawatachoka;,,,, watakwenda kwa miguu,,, wala hawatazimia"""
Zaburi 40:31......

"""Umngoje BWANA uwe HODARI,,,, Upige moyo konde,,,,,, naam umngoje BWANA.....
Zaburi 27:14......

Kwanini leo ni vigumu, kumngoja BWANA???

Cc: Samson Ernest, Baba mtakatifu91, Dogoli kinyamkela, Matunzo 02, Mopak, Seran
kumwamini sio kazi maana matendo yake yako wazi ila ukengeufu wetu ndio shida
 
Back
Top Bottom