Ni kwanini ni vigumu kumngoja BWANA?

Ni kwanini ni vigumu kumngoja BWANA?

Psalm 103

JF-Expert Member
Joined
Jul 5, 2026
Posts
1,657
Reaction score
2,700
"""Bali wao wamngojeao BWANA watapata nguvu mpya;,,,, watapanda juu kwa mbawa kama tai;,,, watapipiga mbio wala hawatachoka;,,,, watakwenda kwa miguu,,, wala hawatazimia"""
Isaya 40:31......

"""Umngoje BWANA uwe HODARI,,,, Upige moyo konde,,,,,, naam umngoje BWANA.....
Zaburi 27:14......

Kwanini leo ni vigumu, kumngoja BWANA???

Cc: Samson Ernest, Baba mtakatifu91, Dogoli kinyamkela, Matunzo 02, Mopak, Seran
 
Mbona wa zamani walifanikiwa,,, ukiondoa hiyo mitandao ya kijamii ilikuwa haipo kwa wakati huo...
Enzi hizo ukitaka kusafiri ilikuwa ni lazima utembee kwa miguu au utumie mnyama, ukitaka habari utaipata kwa njia ya barua , maisha yenyewe yalikuwa yanawalazimisha kuwa na patience, tofauti na sasa hivi ambapo kila kitu unakipata ndani ya muda mfupi sana.

Kumbuka Ibrahimu alisubiri mtoto miaka 25, na Musa alisubiri miaka 40 jangwani, shida ni kwamba historia inasomeka kwa dakika 5 kwenye Biblia, lakini kiuhalisia hao watu walisota sana kuliko sisi.
 
“Utafuteni kwanza ufalme Mungu na hayo yote mtazidishiwa”
 
Presha ya jamii na mitandao ya kijamii ni kubwa mno, peer pressure inakulazimisha uonyeshe matokeo haraka, ilhali mchakato wa Mungu unahitaji usiri na utulivu.
Inawezekana kuna kitu unakijua au upo kwenye process za kujua. “Ongeza kuutafuta ufalme wa Mungu” soon utafunguka na kuongezewa kila kitu
 
Enzi hizo ukitaka kusafiri ilikuwa ni lazima utembee kwa miguu au utumie mnyama, ukitaka habari utaipata kwa njia ya barua , maisha yenyewe yalikuwa yanawalazimisha kuwa na patience, tofauti na sasa hivi ambapo kila kitu unakipata ndani ya muda mfupi sana.

Kumbuka Ibrahimu alisubiri mtoto miaka 25, na Musa alisubiri miaka 40 jangwani, shida ni kwamba historia inasomeka kwa dakika 5 kwenye Biblia, lakini kiuhalisia hao watu walisota sana kuliko sisi.
Unaweza kusubiri miaka 40 in really?

Mda mwingne nahish kama kila kitu ni planned toka kuumbwa.
 
Kumgonja Bwana ni changamoto hata akija leo waliomugoja ni wachache sabab huwezi kumgoja mtu ambaye humkumbuki wala kumfikilia mtu akipata nafasi kidog anaigia kwenye mitandao ya jamii kwa hali hiyo unadhan mtu atamgojaje bwana?
 
Hata musa alipochelewa/ kawia kule mlimani tuliendelea na haruni kidogo na sanamu, Na Mungu alielewa akatusamehe🥹
 
Amen mtumishi
Mimi sio mtumishi na sitakuja kuwa. Am a business man. Ila najua kinachosumbua watu wengi ni kushindwa kutafsiri kile kitabu walicholetewa na wazungu, wakabiwa wakikifuata wataenda mbinguni😂 Bila kujua ile blue print ya kufanikiwa kwenye kila jambo ulitakalo chini ya jua, shida hawana uwezo wa kutafsiri kilicho andikwa. Sasa wanatafsiriwa na watu wanaotaka kuwaburuza
 
Back
Top Bottom