MAKOLE
JF-Expert Member
- Feb 5, 2012
- 618
- 280
Inaonekana wewe hujafatilia ajenda za kikao kile ndio maana unasema haya!
Kuna mambo mbalimbali yenye maslahi kwa taifa yaliyo jadiliwa, nikupe tu mfano;
Kuna teknolojia imetambulishwa nchi, inaitwa Tele Piercing, kama sijakosea, ila namna inavyofanya kazi ni kama ifuatavyo;
Teknolojia hii ni mahususi katika kukabiliana na tatizo la upungufu wa walimu nchini, kwani kifaa hicho kitafungwa kwenye mashule yapatayo 150 kote nchini, hasa zile zenye upungufu mkubwa wa walimu. Lengo hapa ni kuwezesha mwalimu mmoja, labda aliepo Dar, kuweza kufundisha watoto wote kwa wakati mmoja kwenye mashule yote 150 ambayo yamefungwa kifaa hicho.
Hivyo, kufanyika kwa mkutano huu kumeleta tija kubwa kwa taifa, na sio vyema kupotosha mkuu.
Hapo kwenye red nimeipenda hii. Mungu anisaidie niweze kuishi kuyaona hayo nmaajabu hapa Tanzania. Wasiwasi wangu ni je? wanafunzi wangapi huko mavijijini watasaidiwa na mradi huu? au utaishia mijini tu? maana huo umeme wenyewe haujafika vijijini..........