Inaonekana wewe hujafatilia ajenda za kikao kile ndio maana unasema haya!
Kuna mambo mbalimbali yenye maslahi kwa taifa yaliyo jadiliwa, nikupe tu mfano;
Kuna teknolojia imetambulishwa nchi, inaitwa Tele Piercing, kama sijakosea, ila namna inavyofanya kazi ni kama ifuatavyo;
Teknolojia hii ni mahususi katika kukabiliana na tatizo la upungufu wa walimu nchini, kwani kifaa hicho kitafungwa kwenye mashule yapatayo 150 kote nchini, hasa zile zenye upungufu mkubwa wa walimu. Lengo hapa ni kuwezesha mwalimu mmoja, labda aliepo Dar, kuweza kufundisha watoto wote kwa wakati mmoja kwenye mashule yote 150 ambayo yamefungwa kifaa hicho.
Hivyo, kufanyika kwa mkutano huu kumeleta tija kubwa kwa taifa, na sio vyema kupotosha mkuu.
Wewe ni mwalimu au unasema kufurahisha wana JF? Hiyo technology ya Tele Piercing haiwezi kutumika kwa shule zetu hata ukienda shule za hapo Dar ni vigumu kwa sababu zifuatazo:
1. Kiingereza kwa watoto wetu wote hadi waliopo vyuo vikuu ni tatizo kubwa na hivyo kama unajua vema walimu wengi wanafundisha kwa kiswahili na kuandika notice kwa kiingereza.
2. Mradi wa 'big results' haujaanza maana unafahamu teknolojia hiyo inahitaji umeme. Kwa sasa nchi yetu ina 19% ndo wanaopata umeme na umeme wenyewe hata ukiwa na saloon ya kunyolea nywele usipokuwa na standby generator utaliwa tu maana huwa hakuna ratiba maalum ya kukatika umeme. TANESCO wao wanayo ratiba lakini haifuatwi na kila mara utasikia kuna technical fault ilitokea mtuwie radhi.
3. Mtindo wa kufundisha kwa sasa ni students centred learning na teknolojia hiyo ni zaidi lecture method ambayo itafanya mambo yaende nyuma badala ya kwenda mbele.
4. Teknolojia hiyo inapendekeza wanafunzi wasome kwanza vitabu mbali mbali kabla ya kuingia kwenye darasa...unajua ukitaka kumficha kitu mtanzania unakiweka kwenye maandishi licha ya kwamba vitabu vyenyewe havipo.
5. Nahisi utasema wanatumia pia solar energy kuendesha mitambo hiyo, nenda katika zahanati zetu vijijini uone solar panel moja tu ilivyoshindwa kuhudumia walau spot light ya kijijumba cha zahanati maana utunzaji ulikuwa karibu na zero na sehemu nyingine wajanja walihamishia kwao, sembuse kwenye shule zetu zenye walinzi wa sungusungu?
6. Watanzania tunapenda vitu dhahania na huu nao ni mradi dhahania, watoto wetu hawajui hata kutumia simu na nilimsikia JK akiongelea iPod n.k kana kwamba mtu aliyeko NYANSULUBI na kule kwetu Mabondekwinama atakuwa tu na uwezo huo
7. Mitandao yetu hadi benki na TRA utaambiwa leo mtandao uko chini (hadi kwenye ATM) na TTCL na mkonga wa taifa waliosema ni suluhisho la kudumu na hub iko University of Dar es Salaam na wame-subscribe Mbps nyingi nadhani zaidi ya 12 lakini kaangalie mtandao ulivyo hadi wamelazimika kuomba kuunganishwa na TERNET badala ya mkonga wa taifa ili mambo yaende vema.
Hivyo tusijifanye kama vile tupo na miradi ya kuwaletea tu ulaji watu wa kuuza hizo mashine za namna hiyo wakati hazitazaa matunda. Elimu yetu haijaharibika maana mtindo wa elimu iliyotolewa Tz kuanzia miaka ya 77 hadi leo ni ule ule isipokuwa kitu kimoja tu nacho ni 'alternative to practical' vingine vyote vimebaki ukiacha mabadiliko ya Mungai yaliyodumu kwa muda mfupi. Naye kama hukujua alipewa na kichaa mmoja wa Liege Ubelgiji aliyekuwa na ubia wa kuendesha shule zake kule Iringa kumbe kaingizwa mkenge!Miaka yote hiyo mfumo umefanya kazi vizuri hadi kwenye miaka ya kuanzia late 90's ni vema kujiuliza kwa nini kuliko kutafuta mfumo mbadala maana mfumo ulifanya kazi vema na watu walifaulu na vijana walisifika kote walikoenda kusoma. Hatukuwa na watanzania wasiojua kiingereza wala wa kubabaisha na kuanza kuwa VIHIYO. Unajua wa kwanza kuwa KIHIYO ni mbunge kwa hiyo waliopelekea mambo haya kufika hapa tulipo tuanze na WANASIASA tutapata suluhisho.
Najua unaipenda nchi yako Tz kama ninavyoipenda lakini umeghubikwa na kutetea chama zaidi kuliko nchi...nadhani Tz ni wazo pana zaidi kuliko CUF, CDM, CCM etc