Ni kwamba Dr Slaa katoswa au?

Ni kwamba Dr Slaa katoswa au?

WanaJF!

Hivi karibuni Tanzania ilikuwa mwenyeji wa mkutano mkubwa ulioenda kwa jina '2013 GLOBAL SMART PARTNERSHIP' ambao uliongozwa na rais Jakaya Kikwete uliofanyika hapa Dar es salaam. Mkutano huu ulihusisha wadau mbalimbali wakiwemo marais, mawaziri, wafanyabiashara wakubwa, wanasiasa na watu mashuhuri.

Ni mkutano ulioipa Tanzania heshima ya kipekee sana katika historia ya nchi yetu, hasa ukizingatia ujumbe wa mkutano huo na ajenda mbalimbali zilizo jadiliwa zenye kulenga kuiwezesha nchi yetu kufanya mapinduzi ya teknolojia ya habari na mawasiliano.

Jambo lililo nishangaza kwenye mkutano huo ni kukosekana kwa uwakilishi wa vyama vya siasa hasa vya upinzania, ukizingati mambo mengi yaliyo jadiliwa yana athiri taifa letu hasa kwenye nyanja ya teknolojia. Kwa vyama vingine sitaweza kuvijadili kwa kuwa ina semekana ni CCM-B, lakini ilikuwaje CHADEMA hakikushiriki?

Kama itakumbukwa, April 8, 2013, Dr Slaa alishiriki kwenye mkutano wa CEO Round Table, na nilimpa pongezi sana kwa kushiriki kwake kwenye mkutano huo, kwani ajenda ilikuwa inazungumzia 'PUBLIC PRIVATE PARTNERSHIP', ambayo ni ajenda nzuri na yenye tija kwa taifa. Lakini iweje hii ya GLOBAL SMART PARTNERSHIP asishiriki? ni kwamba serikali imemtosa au yeye hakupenda kujihusisha na mambo ya serikali?
HAMY-D Mapenzi yako kwa chama makini chadema sasa yako wazi, Karibu Chama Makini Chadema.
 
Ila ki-ukweli hapa HAMY-D ana hoja ya msingi. Inakuwaje vyama ambavyo vinapingania kuingia IKULU havishikriki katika shighuli nyeti kama hizi??? Inawezekana

(1) Ni uchoyo wa kijinga wa CCM au
(2) Ni upuuzi wa kijinga wa vyama vya upinzani kukataa kushiriki

Jibu ni lipi???

Hao mialiko wasiyosusa ni chai na juice ikulu hata hivyo miongoni mwao ni nani mwenye uwezo wa kujadili maendeleo na viongozi wa kimataifa?
 
documents za kikao zipo kwenye dust bin pale airport VIP, zote ziliachwa wakati washiriki wakipaa mkutano huu ulikuwa ni INTERNATIONAL BUFFET IN TANZANIA kama ilivyo mikutano yote inayoandaliwa bongo, sema tu wakubwa wanakula zaidi ya buffet kwa kuongeza pesa za matumizi na kuunda kampuni za kuhudumia mkutano.

Phd kazakhstan , June 30th, 2013

Kwa hiyo tija kwa Taifa ni ipi hapo kama siyo kuzidi kuongeza tatizo la wasio na hajira?na hicho kifaa kitakuwa na uwezo wa kkusahhisshia wanafunnzi?au mwalimu atasafiri kusahisha kazi za wanafunzi wake?
 
Unashangaza, hivi unaamini kuna kitu pale au ni sanaa? Dr wa ukweli hazundumzii mambo ya kufikirika sana. Wewe kila kitu ni Dr Slaa tuu,kwa taarifa yako mambo ya kisanii huwa hajihusishi. Haya huyo Mkulu wako ambaye hajui kwa nini nchi yake ni masikini ameongea nini? Mijadala yenye tija subiri after 2016 utaiona.

Mkuu, tuwe wazalendo, hatuwezi kuipuuza Tanzania mpaka hapo hiyo furaha yenu ya Dr Slaa kutawala ifike. Kwani Tanzania ni bora zaidi kuliko awa wanasiasa wetu. Ilipaswa washiriki ili wakatoe michango yao!
 
nngu007,

Sitaki kuamini kama Rwanda awakupata mwaliko ama Malawi, sina uhakika kama ni wanachama, ila Kenya dharura yake ilitangazwa. Sidhani kama serikali imefanya ulafi wa aina yoyote kwenye huu mkutano, ukizingatia watu mashuhuri wa hapa hapa nyumbani walikuwa wengi. Jambo la kushtua ni kwamba ilikuwaje watu wa muhimu na wenye ushawishi kwenye jamii kama Dr Slaa wasihudhurie?

Huwezi kuhudhuria tu bila kualikwa haukuwa mkutano wa wazi kwa kila mtu... Vitu vya hii serikali vyote vinafanyika kwa misingi ya manufaa ya kisiasa, hakuna utaifa.
 
Inaonekana wewe hujafatilia ajenda za kikao kile ndio maana unasema haya!

Kuna mambo mbalimbali yenye maslahi kwa taifa yaliyo jadiliwa, nikupe tu mfano;

Kuna teknolojia imetambulishwa nchi, inaitwa Tele Piercing, kama sijakosea, ila namna inavyofanya kazi ni kama ifuatavyo;

Teknolojia hii ni mahususi katika kukabiliana na tatizo la upungufu wa walimu nchini, kwani kifaa hicho kitafungwa kwenye mashule yapatayo 150 kote nchini, hasa zile zenye upungufu mkubwa wa walimu. Lengo hapa ni kuwezesha mwalimu mmoja, labda aliepo Dar, kuweza kufundisha watoto wote kwa wakati mmoja kwenye mashule yote 150 ambayo yamefungwa kifaa hicho.

Hivyo, kufanyika kwa mkutano huu kumeleta tija kubwa kwa taifa, na sio vyema kupotosha mkuu.
In teaching methodology, training is more effective when is given directly to students. In current situation with addition to teaching methodology requirments we have poor infrastructure to support the technology. With these facts in mind I find this technology absolete to primary and secondary level students in Tanzania where the deficit of teachers is apparent.
 
WanaJF!

Hivi karibuni Tanzania ilikuwa mwenyeji wa mkutano mkubwa ulioenda kwa jina '2013 GLOBAL SMART PARTNERSHIP' ambao uliongozwa na rais Jakaya Kikwete uliofanyika hapa Dar es salaam. Mkutano huu ulihusisha wadau mbalimbali wakiwemo marais, mawaziri, wafanyabiashara wakubwa, wanasiasa na watu mashuhuri.

Ni mkutano ulioipa Tanzania heshima ya kipekee sana katika historia ya nchi yetu, hasa ukizingatia ujumbe wa mkutano huo na ajenda mbalimbali zilizo jadiliwa zenye kulenga kuiwezesha nchi yetu kufanya mapinduzi ya teknolojia ya habari na mawasiliano.

Jambo lililo nishangaza kwenye mkutano huo ni kukosekana kwa uwakilishi wa vyama vya siasa hasa vya upinzania, ukizingati mambo mengi yaliyo jadiliwa yana athiri taifa letu hasa kwenye nyanja ya teknolojia. Kwa vyama vingine sitaweza kuvijadili kwa kuwa ina semekana ni CCM-B, lakini ilikuwaje CHADEMA hakikushiriki?

Kama itakumbukwa, April 8, 2013, Dr Slaa alishiriki kwenye mkutano wa CEO Round Table, na nilimpa pongezi sana kwa kushiriki kwake kwenye mkutano huo, kwani ajenda ilikuwa inazungumzia 'PUBLIC PRIVATE PARTNERSHIP', ambayo ni ajenda nzuri na yenye tija kwa taifa. Lakini iweje hii ya GLOBAL SMART PARTNERSHIP asishiriki? ni kwamba serikali imemtosa au yeye hakupenda kujihusisha na mambo ya serikali?


Nape bwana!!!, unaniachaga hoi kweli, tangu uanze kutumia ID hii umeongeza post kweli, halafu zote unaangukia pua. Hahahaha
 
nngu007,

Sitaki kuamini kama Rwanda awakupata mwaliko ama Malawi, sina uhakika kama ni wanachama, ila Kenya dharura yake ilitangazwa. Sidhani kama serikali imefanya ulafi wa aina yoyote kwenye huu mkutano, ukizingatia watu mashuhuri wa hapa hapa nyumbani walikuwa wengi. Jambo la kushtua ni kwamba ilikuwaje watu wa muhimu na wenye ushawishi kwenye jamii kama Dr Slaa wasihudhurie?

HAMY-D bwana!
Majibu unayo mwenyewe kumbe!
Kwa kukubali kwamba DR. SLAA ni kati ya watu WA UMUHIMU NA WENYE USHAWISHI kwenye JAMII unamaanisha hawana haja ya kujitaabisha kujulikana!
Na najua unaelewa maana ya neno JAMII
Tuwaache wahudhurie wale wasiojulikana kwenye JAMII...
Kama FASILI yako ya neno jamii inamaanisha TANZANIA peke yake ni vizuri ujue kwamba MAKONGAMANO hayapigi KURA.

JAMII ndo hupiga kura na huko tayari yuko/wako maarufu tayari...
Viongozi wa MAKONGAMANO na wapenda picha wapo.
SLAA si kati yao.
 
WanaJF!

Hivi karibuni Tanzania ilikuwa mwenyeji wa mkutano mkubwa ulioenda kwa jina '2013 GLOBAL SMART PARTNERSHIP' ambao uliongozwa na rais Jakaya Kikwete uliofanyika hapa Dar es salaam. Mkutano huu ulihusisha wadau mbalimbali wakiwemo marais, mawaziri, wafanyabiashara wakubwa, wanasiasa na watu mashuhuri.

Ni mkutano ulioipa Tanzania heshima ya kipekee sana katika historia ya nchi yetu, hasa ukizingatia ujumbe wa mkutano huo na ajenda mbalimbali zilizo jadiliwa zenye kulenga kuiwezesha nchi yetu kufanya mapinduzi ya teknolojia ya habari na mawasiliano.

Jambo lililo nishangaza kwenye mkutano huo ni kukosekana kwa uwakilishi wa vyama vya siasa hasa vya upinzania, ukizingati mambo mengi yaliyo jadiliwa yana athiri taifa letu hasa kwenye nyanja ya teknolojia. Kwa vyama vingine sitaweza kuvijadili kwa kuwa ina semekana ni CCM-B, lakini ilikuwaje CHADEMA hakikushiriki?

Kama itakumbukwa, April 8, 2013, Dr Slaa alishiriki kwenye mkutano wa CEO Round Table, na nilimpa pongezi sana kwa kushiriki kwake kwenye mkutano huo, kwani ajenda ilikuwa inazungumzia 'PUBLIC PRIVATE PARTNERSHIP', ambayo ni ajenda nzuri na yenye tija kwa taifa. Lakini iweje hii ya GLOBAL SMART PARTNERSHIP asishiriki? ni kwamba serikali imemtosa au yeye hakupenda kujihusisha na mambo ya serikali?

mwigulu alikuwepo?
 
Inaonekana wewe hujafatilia ajenda za kikao kile ndio maana unasema haya!

Kuna mambo mbalimbali yenye maslahi kwa taifa yaliyo jadiliwa, nikupe tu mfano;

Kuna teknolojia imetambulishwa nchi, inaitwa Tele Piercing, kama sijakosea, ila namna inavyofanya kazi ni kama ifuatavyo;

Teknolojia hii ni mahususi katika kukabiliana na tatizo la upungufu wa walimu nchini, kwani kifaa hicho kitafungwa kwenye mashule yapatayo 150 kote nchini, hasa zile zenye upungufu mkubwa wa walimu. Lengo hapa ni kuwezesha mwalimu mmoja, labda aliepo Dar, kuweza kufundisha watoto wote kwa wakati mmoja kwenye mashule yote 150 ambayo yamefungwa kifaa hicho.

Hivyo, kufanyika kwa mkutano huu kumeleta tija kubwa kwa taifa, na sio vyema kupotosha mkuu.

Apo ni maendeleo au msiba wa taaluma?..mwalimu dar afu mwanafunzi tunduma?ee Mwenyez epushia mbali..
 
baba Mwanaasha: Ok forget about your teacher!
One plus one is? ......
Wanafunzi: two
baba Mwanaasha: Not three!! hahahaaaa

Huyo ndo baba Mwanaasha
 
Apo ni maendeleo au msiba wa taaluma?..mwalimu dar afu mwanafunzi tunduma?ee Mwenyez epushia mbali..

Mkuu, hicho kifaa kitakuwa kwenye screen kubwa sana yenye uwezo wa kuonyesha hata chunusi/kipele yako mkuu.

Pia itakuwa na kitufe endapo mwanafunzi ana swali la kuuliza.

Lakini kama hiyo haitoshi, mwanafunzi anapo uliza swali, ataonekana kwenye shule zote 150 zitakazo fungwa kifaa hicho.

Mkuu, wewe unaelewa changamoto iliyopo juu wa walimu wetu, ni vyema huu mfumo utumike huku serikali ikiendelea na jitihada zingine za kuweka mazingira bora kwa walimu.
 
Inaonekana wewe hujafatilia ajenda za kikao kile ndio maana unasema haya!

Kuna mambo mbalimbali yenye maslahi kwa taifa yaliyo jadiliwa, nikupe tu mfano;

Kuna teknolojia imetambulishwa nchi, inaitwa Tele Piercing, kama sijakosea, ila namna inavyofanya kazi ni kama ifuatavyo;

Teknolojia hii ni mahususi katika kukabiliana na tatizo la upungufu wa walimu nchini, kwani kifaa hicho kitafungwa kwenye mashule yapatayo 150 kote nchini, hasa zile zenye upungufu mkubwa wa walimu. Lengo hapa ni kuwezesha mwalimu mmoja, labda aliepo Dar, kuweza kufundisha watoto wote kwa wakati mmoja kwenye mashule yote 150 ambayo yamefungwa kifaa hicho.

Hivyo, kufanyika kwa mkutano huu kumeleta tija kubwa kwa taifa, na sio vyema kupotosha mkuu.

Kwahiyo hichi kifaa kinaweza fanya kazi hata kule kwetu Nanyamba, Kanyangereko, Chizumbura, na uvinza ambapo umeme haupo? Nijuavyo shule zisizo na walimu hasaaaa ni kati ya hizo toka nyumbani kwetu; ama ndo yaleyale mwenye nacho huongezewa kitafungwa hapa hapa Dar?
 
Ila ki-ukweli hapa HAMY-D ana hoja ya msingi. Inakuwaje vyama ambavyo vinapingania kuingia IKULU havishikriki katika shighuli nyeti kama hizi??? Inawezekana

(1) Ni uchoyo wa kijinga wa CCM au
(2) Ni upuuzi wa kijinga wa vyama vya upinzani kukataa kushiriki

Jibu ni lipi???
Mkuu Manyi;Hamy-D hakuzungumzia Chadema kutoswa kazungumzia Dr Slaa katoswa.wewe unataja vyama vya Upinzani.Hamy-D post zake ameambiwa asipomzungumia mabaya Dr Slaa hapati buku7 za lumumba.
 
Mkuu Manyi;Hamy-D hakuzungumzia Chadema kutoswa kazungumzia Dr Slaa katoswa.wewe unataja vyama vya Upinzani.Hamy-D post zake ameambiwa asipomzungumia mabaya Dr Slaa hapati buku7 za lumumba.

Mkuu, kama ufahamu namna ya uongozi kwenye vyama vya siasa ni bora uulize. Sababu ya mimi kumtaja Dr Slaa ni kwa kuwa yeye ndiye mtendaji mkuu wa CHADEMA na si vinginevyo.
 
Back
Top Bottom