Ni kina nani hawa wanaotishia usalama wa Rais wetu kiasi hiki?

Akina TL, IMMA advocates, Azory Gwanda, Mawazo... walikuwa wanauza madawa gani?
Tatizo mambo serious unaleta utani..hapo kuna issue bado zipo kwenye upelelzi unazileta hapa za nini..? Kumbe jibu lako ni la kihisia zaidi..nilidhani unaleta mifano hai..lakini nikutonye jomba, kati ya hayo uliyoyataja, kuna baadhi ya kesi wanasema yapo hukohuko kwenu yanajulikana...sasa mmeshafanya Serikali ni jamvi la bibi..madudu yote mnarushia huko.....be careful...mnachinjana wenyewe kwa wenyewe halaf mnasingizia serikai..huu ni ujinga wa division nine
 
Angalia kinachotokea Venezuela kisa Maduro anazuia mafuta kama mtangulizi wake Hugo Chavez ambaye inasemekana walimpa sumu ya kufa taratibu alipoenda mikutano ya kimataifa kwao. Hata Kim Jong Un, usipozuia maslahi yao huna haja hata ya ulinzi seriously, malawi wana tumbaku na Chai tu umeona wazungu wanahangaika nao??, Hata ziara za kuelekea Malawi hakuna. Inafaa kuwaangalia wazungu kwa upeo mkubwa, hapo Uganda kabla jamaa hajagundua mafuta kelele kila siku umekaa muda mrefu ustaafu, alivyogundua mafuta kelele Imeisha wanajua bora wanaemmudu kuliko aje mpya kama Magufuli. Unatakiwa kuwa na upeo kuwaelewa wale jamaa
Wazungu wa wapi na Wewe!!!? Unadhani hao waswahili wanaopotea ni yatima!!!?
 
alienda kumuaga TISS aliyempig risasi mh. TUNDU LISSU. TISS YULE ALING'OA JINO MTAANI AKAAGA DUNIA. ASANTE MUNGU KWA KUTENDA MAAJABU YAKO.
kama mitutu inasaidia mbona anaenda kwa walozi na wachawi hko malawi?
 
Angalia kinachotokea Venezuela kisa Maduro anazuia mafuta kama mtangulizi wake Hugo Chavez ambaye inasemekana walimpa sumu ya kufa taratibu alipoenda mikutano ya kimataifa kwao. Hata Kim Jong Un, usipozuia maslahi yao huna haja hata ya ulinzi seriously, malawi wana tumbaku na Chai tu umeona wazungu wanahangaika nao??, Hata ziara za kuelekea Malawi hakuna. Inafaa kuwaangalia wazungu kwa upeo mkubwa, hapo Uganda kabla jamaa hajagundua mafuta kelele kila siku umekaa muda mrefu ustaafu, alivyogundua mafuta kelele Imeisha wanajua bora wanaemmudu kuliko aje mpya kama Magufuli. Unatakiwa kuwa na upeo kuwaelewa wale jamaa

..natofautiana kidogo na mtizamo wako.

..wakati wa utawala wa Nyerere manowari za makaburu wa afrika kusini zilifika mpaka Dsm na kushambulia.

..pia viongozi wa vyama vya ukombozi walikuwa na makazi na ofisi zao Dsm na makambi ya kijeshi ktk maeneo mbalimbali ya Tz.

..Eduardo Mondlane wa Frelimo aliuawa nyumbani kwake Dsm kwa bomu lililofichwa ktk barua.


..Mwalimu Nyerere alitaifisha migodi, mabenki, viwanda, mashamba makubwa, yaliyokuwa yakimilikiwa na wawekezaji mbalimbali wengi wakiwa raia wa nchi za mabeberu.

..Wakati wa Mwalimu Nyerere pia kulikuwa na askari wetu waliotumwa Comoro, na Seychelles. Na bila kusahau wetu na Kamuzu Banda wa Malawi.


..Pia ongeza mgogoro wa muda mrefu na VITA dhidi ya Iddi Amini wa Uganda.

..Halafu kulitokea majaribio ya kupindua serekali zaidi ya mawili, pamoja na kesi za UHAINI. Na machafuko ya hali ya kisiasa ya Zanzibar.

..Pamoja na hayo yote, sikuwahi kushuhudia ULINZI mkubwa na wa kutisha kama huu tunaoushuhudia miaka hii.

..MWALIMU NYERERE aliwahi kuandika hata hotuba akilalamika kuwa ana msafara mkubwa ambao alikuwa hauhutaji kwani hakutaka kuwa kero na kituko kwa wananchi.

CC Nguruvi3, Pascal Mayalla, tindo
 
Wazungu tuliozuia wasiondoke na mchanga, wauza unga na mitandao yao, wa meno ya tembo na mitandao yao, wapiga dili sekta za umma na matajiri mafisadi na wakwepa kodi huwa ni watu hatari sana unapoendesha vita vya uchumi
Duh. Anapiga vita uchumi? Hili unalosema linawezekana kwa sababu inasemwa uchumi umewekwa juani, unakauka na kusinyaa.

Wafanyakazi wa umma nao ni mafisadi au wapiga dili? Hata nyongeza halali, annual increment, nayo haiwezekani kulipwa?

Kwa uendeshaji huu wa vita ya uchumi lazima uchumi ukue kwa asilimia 7%. Only in Bongolala.
 
Angalia kinachotokea Venezuela kisa Maduro anazuia mafuta kama mtangulizi wake Hugo Chavez ambaye inasemekana walimpa sumu ya kufa taratibu alipoenda mikutano ya kimataifa kwao. Hata Kim Jong Un, usipozuia maslahi yao huna haja hata ya ulinzi seriously, malawi wana tumbaku na Chai tu umeona wazungu wanahangaika nao??, Hata ziara za kuelekea Malawi hakuna. Inafaa kuwaangalia wazungu kwa upeo mkubwa, hapo Uganda kabla jamaa hajagundua mafuta kelele kila siku umekaa muda mrefu ustaafu, alivyogundua mafuta kelele Imeisha wanajua bora wanaemmudu kuliko aje mpya kama Magufuli. Unatakiwa kuwa na upeo kuwaelewa wale jamaa

Peleka ujinga mbali. Kwa kipi kilichoko Tanzania ambapo hakipo pengine?
 
Jana msafara wake ulienda kuaga mwili wa "afisa" mmoja wa TISS, kila kona ya bara bara kukawa na askari wenye mitutu ya bunduki. Leo pia vivyo hivyo.

Nimejikuta najiuliza hivi ni adui au maadui gani hawa wanamtisha na kumuogofya Mkuu wetu wa nchi anayependwa na wananchi wake kiasi hiki?

Isije tokea siku tukapoteza risasi zetu kwa kuua Inzi..!
unajuwa ukiwa unatenda uovu lazima uwe mwoga kwani unanuwa wale unao watendea uovu nao wanajipanga kulipiza kisasi. hakuna anaye mtisha ila uovu wake ndio unao mnyima usingizi.
 
Huku na yeye akizivunja..... mpaka katiba aliyoapa kuilinda anaivunja
Ningetamani kama ungetumia maneno mengine juu ya kiongozi wako. Nikuulize swali; Hivi unamjua dikteta au hilo neno wadhani ni wadhifa wa mtu?? Unawezaje mtu kumlinganisha kiongozi wako na dikteta?? Mimi sijawahi kuishi chini ya dikteta ila, nisingelipenda kuonja maisha chini ya dikteta. Huyu wangu naweza sema, Ni mkali kwa wavunja sheria tu.
 
Sikuwahi kushuhudia ULINZI mkubwa na wa kutisha kama huu tunaoushuhudia miaka hii.

..MWALIMU NYERERE aliwahi kuandika hata hotuba akilalamika kuwa ana msafara mkubwa ambao alikuwa hauhutaji kwani hakutaka kuwa kero na kituko kwa wananchi.

CC Nguruvi3, Pascal Mayalla, tindo
The guilty one's are always afraid.
"Fire on his ayes and fear is a weapon on his heart".

Hata maofisini ukiona Boss haendi kabisa likizo kwa kisingizio cha kuwa bize na uchapa kazi, ujue sii bure!.
Yaani mtu husafiri tena safari nyingine za maana sana kuhudhuria mikutano muhimu, nchi tuna Gulfstream yetu, unaweza kwenda na kurudi the same day.

Niliwahi kufanya kiji psychoanalysis humu kuhusu mambo kadhaa




P
 
"JokaKuu, post: 31350849, member: 221"]
..natofautiana kidogo na mtizamo wako.

..wakati wa utawala wa Nyerere manowari za makaburu wa afrika kusini zilifika mpaka Dsm na kushambulia.
Watu wengi hawakumbuki jinsi Mreno alivyosumbua Nachingwea n.k.
Wakati huo huo makaburu walikuwa pamoja na Mreno kuhakikisha Nyerere anazimwa
Viongozi wote wa vyama vya ukombozi walikuwa na makazi Tanzania na kambi zao
..Mwalimu Nyerere alitaifisha migodi, mabenki, viwanda, mashamba makubwa, yaliyokuwa yakimilikiwa na wawekezaji mbalimbali wengi wakiwa raia wa nchi za mabeberu.
Na pia kuzuia uchimbaji wa madini hovyo ''hadi Watanzania watakpokuwa tayari''
..Wakati wa Mwalimu Nyerere pia kulikuwa na askari wetu waliotumwa Comoro, na Seychelles. Na bila kusahau wetu na Kamuzu Banda wa Malawi.
..Pia ongeza mgogoro wa muda mrefu na VITA dhidi ya Iddi Amini wa Uganda.

..Halafu kulitokea majaribio ya kupindua serekali zaidi ya mawili, pamoja na kesi za UHAINI. Na machafuko ya hali ya kisiasa ya Zanzibar.

..Pamoja na hayo yote, sikuwahi kushuhudia ULINZI mkubwa na wa kutisha kama huu tunaoushuhudia miaka hii.[/USER], Pascal Mayalla, tindo
Kulikuwa na mgogoro wa Nyang'au wa Kenya

Mwalimu alikuwa ''vulnerable' zaidi kutokana na mazingira yaliyokuwepo.
Majirani walikuwa na bifu, kuna Mreno, Kaburu na mabeberu n.k.

Kitu kisichoonekana kwa urahisi, Mwalimu alikuwa na ulinzi mkali sana

Ulinzi wake haukuwa wa makundi kubeba silaha au kukingwa na kifusi cha ''watu''

Ulinzi wa Mwalimu ulikuwa katika idara ya usalama wa Taifa ambayo iliweza kutafuta, kuchambua, kutathmini na kubaini matukio au mipango ovu kabla ya kutokea

Idara ilichukua hatua mapema hivyo hakukuwa na haja ya kuwa na lundo la watu wenye silaha.

Kwa maneno mengine Mwalimu alikuwa na intelligence kali sana iliyomfanya awe huru popote alipo

Ukitaka kujua intelligence unit ya wakati wa Mwalimu kawaulizeni akina Kapteni Tamim, Hat Mcghee, Oswald Mbogoro n.k. ambao wakati wanafanya mipango Ikulu ilikuwa na script ya movie yote mpaka meli za mabeberu zilipotia nanga, zina silaha gani n.k.
 
Na zaidi, kila mwananchi alikuwa ni mwanausalama. Kwa sisi tuliokuwa vijijini, wageni walitolewa taarifa kwa balozi wa nyumba 10. Kulikuwa na uzalendo wa kweli. Sasa hivi tunadanganyana tu. Na kila mtu anajua hivyo. Na ndio maana unaona watu wanajizungushia batallion nzima ikiwa na silaha nzito ili kujilinda wenyewe. Wanajua kuwa wameharibu uzalendo.
Ulinzi wa Mwalimu ulikuwa katika idara ya usalama wa Taifa ambayo iliweza kutafuta, kuchambua, kutathmini na kubaini matukio au mipango ovu kabla ya kutokea
 
Back
Top Bottom