Ni halali ndg Edward Lowassa kuitwa 'Waziri Mkuu mstaafu'?

Hii si hoja ya kipuuzi hata kidogo kwa mwenye akili timamu. Waandishi wa habari wanamapungufu makubwa katika kuandika na kuchuja habari.
Alhaji Jumbe hajaitwa rais mstaafu, bali aliyekuwa rais wa Zanzibar. Edwin Mtei haitwi waziri wa fedha mstaafu, bali aliyekuwa waziri wa fedha. Mwinyi hakuwahi kuitwa waziri wa mambo ya ndani mstaafu, bali aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani. Lowasa hakustaafu, alijiuzulu tena baada ya kuhisi balaa la kura ya maoni bungeni. Ni makosa makubwa kumpa hadhi ya ustaafu ili hali aliondoka madarakani kwa aibu kubwa. Haki yake ni kuitwa aliyekuwa waziri mkuu, au waziri mkuu aliyejiuzulu ili kumtofautisha na Mawaziri wakuu waliofanya kazi kwa heshima kama Marehemu Mwalimu Nyerere, Marehemu Kawawa, Marehemu sokoine, Mzee Msuya, Mzee Malecela, Mzee Warioba na Sumaye.
 
Hili swali limekuwa likinitatiza siku nyingi, lakini nadhani sijui neno "kustaafu" maana yake ni nini. Hivi ni kweli pamoja na kashfa zote alizofanya na anazoendelea kufanya mpaka akalazimika kujiuzulu tunapashwa kumwita EL kwamba ni PM Mstaafu?

Nilidhani atafutiwe sifa nyingine, siyo hiyo. Je, tukimwita mstaafu, tutatumia sifa gani kwa Marehemu Baba wa Taifa, Mzee Mwinyi, Marehemu Kawawa, Warioba, Sumaye nk.

Naomba michango yenu ya mawazo ili hatimaye tupate sifa inayoendana na na ufisadi wake.

Nawakilisha.



What is the contrast between Dismissal and Retirement.
 
Ila ninachojua ni kwamba hata hao tunaowaita 'wastaafu PM'...sidhani kama kweli walistaafu. Kiukweli katiba yetu si nzuri.
Kustaafu ni hali ya mtumishi kufikia ukingo wa kutumika (kiumri) na kwamba hastahili kuendelea na nafasi yake hivyo kuhitajika 'kustaafu'. Ukitazama kwa undani...mawaziri wakuu wote hakuna hata mmoja katika nchi hii (PM) aliyefikia hatua ya kwamba mimi ninastaafu, NI BABA WA TAIFA TU NDIE ALIYEFIKIA HATUA AKIWA RAIS KUTAMKA KUWA SASA 'ANANG'ATUKA', waliosalia ni aidha muda wao wa ukomo umefika (kwa mujibu wa aliyemteua) au wamebadilishwa na wakuu wao kwa sababu za kiutendaji kwa manufaa ya UMMA na si kustaafu.

naombeni mnisahihishe kama nimepotoka,

NAWASILISHA.
 
Hili swali limekuwa likinitatiza siku nyingi, lakini nadhani sijui neno "kustaafu" maana yake ni nini. Hivi ni kweli pamoja na kashfa zote alizofanya na anazoendelea kufanya mpaka akalazimika kujiuzulu tunapashwa kumwita EL kwamba ni PM Mstaafu?

Nilidhani atafutiwe sifa nyingine, siyo hiyo. Je, tukimwita mstaafu, tutatumia sifa gani kwa Marehemu Baba wa Taifa, Mzee Mwinyi, Marehemu Kawawa, Warioba, Sumaye nk.

Naomba michango yenu ya mawazo ili hatimaye tupate sifa inayoendana na na ufisadi wake.

Nawakilisha.

kumuita EL waziri mkuu mstaafu ni sawa na kumuita kikwete Dokta.

ni kufuru
 
Ila ninachojua ni kwamba hata hao tunaowaita 'wastaafu PM'...sidhani kama kweli walistaafu. Kiukweli katiba yetu si nzuri.
Kustaafu ni hali ya mtumishi kufikia ukingo wa kutumika (kiumri) na kwamba hastahili kuendelea na nafasi yake hivyo kuhitajika 'kustaafu'. Ukitazama kwa undani...mawaziri wakuu wote hakuna hata mmoja katika nchi hii (PM) aliyefikia hatua ya kwamba mimi ninastaafu, NI BABA WA TAIFA TU NDIE ALIYEFIKIA HATUA AKIWA RAIS KUTAMKA KUWA SASA 'ANANG'ATUKA', waliosalia ni aidha muda wao wa ukomo umefika (kwa mujibu wa aliyemteua) au wamebadilishwa na wakuu wao kwa sababu za kiutendaji kwa manufaa ya UMMA na si kustaafu.

naombeni mnisahihishe kama nimepotoka,

NAWASILISHA.
Mkuu,

Kwa maoni yangu ni kuwa wewe upo juu ya msitari, ni sahihi kabisa uyasemayo.
Kwa vile Tanzania ni nchi yenye heshima ya woga, hawa waliotumikia vipindi wa uteuzi au muda waliochaguliwa au waliojichaguwa ,waliojiporea nafasi za uonngozi na sisi tukakubali yaishe basi tuwaache tu watumie hiyo sifa kama walitumika hadi pale ukomo wa kazi, nafasi unavyotaka.

Lakini hata kwa kulazimisha hii ya Lowassa kuwa ni Waziri Mkuu mstaafu ni bu.ll s.hit!
Lowassa hakutumika hadi ukomo wa ajira. Alichofanya ni kukimbia fedheha ya kufukuzwa kazi .Kitu kilichokuwa wazi kabisa kuwa kingetokea. Kama Rais asingemfukuza basi bunge lingepiga kura ya kutokuwa na imani nae. Kwa maana nyengine angestaafishwa kwa manufaa ya umma.

Sasa kustaafu na kustaafishwa ni vitu tofauti.

Hastahili kuitwa waziri mkuu mstaafu na kama anakula jasho la mlalahoi ni ufisadi mwengine!

Tembelea hapa ufurahi.
http://pambazuko.blogspot.com/2005/08/ni-nini-maana-ya-kustaafu.html
 
Tuna hitaji wau wa Baraza la Kiswahili watupe neno sahihi, tujuavyo kwa viongozi kama:-
Mwl. Nyerere......Aling'atuka urais
Sokoine ............Alikufa kwa 'ajali' "Hayati .... aliyekuwa PM"
Mwinyi, Mkapa ....Rais Mstaafu wa awamu ya .... (Ingawa siyo sahihi sana)
Salimu, Sumaye...MaPM (anyway) wastaafu
Lowassa........Waziri Mkuu aliyejiuzuru
fulani bin flani .....Aliyestaafishwa kwa manufaa ya umma! Hivi inaelewekw vizuri1

Baraza la Kiswahili watusaidie maana wana maneno mengi yanayojitegemea.
 
Siyo Waziri Mkuu Mstaafu. Unapomtaja unasema Wziri Mkuu wa Zamani au Waziri Mkuu wa tisa, kumi, ishirini, n.k.
 
E.L sio waziri mkuu mstaafu kwani hakustaafu ila alistaafishwa kwa manufaa ya uma.Kustaafu maana yake ni kufikia kikomo cha ajira kwa mujibu wa sheria.E.L namfananisha na mtu aliefukuzwa kazi kwa fedhea.Kumweka E.L kwenye orodha ya wastaafu ni mbinu za ccm kuendelea kumpa ulaji fisadi huyo mkubwa ili aendelee kupata benefits za ma PM wastaafu kama mshahara,ulinzi etc
 
Hi jamii forum members!
Sory jaman naomben mnisaidie utata huu nlionao ktk kichwa juu ya uhalali wa Edward lowasa kuitwa waziri mkuu mstaafu wa tz na km ni halali ni kwa vigezo vp?km sio ni kwa vigezo vp?pia katiba yetu ya nchi inasemaje juu ya hilo?
THANK YOU ALL IN ADVANCE!
 
Si halali. Simply because hakustaafu bali alijiuzulu! At least hata aitwe waziri mkuu wa zamani au aliyewahi kua waziri mkuu
 
mtu anaejiuzulu sio mstaafu...! Lowasa hapaswi kujiita waziri mkuu mstaafu haswa ukizingatia alijiuzulu tena kwa kashfa...! Watu wanaojiuzulu kwa kashfa tena kashfa ya rushwa halafu apewe heshima ya kuitwa mstaaafu naona sio sawa kabisaaa...!

kama ni hivyo, je tutaweza kumuita Karamagi nae waziri wa nishati na madini mstaafu?
 
Back
Top Bottom