Hili swali limekuwa likinitatiza siku nyingi, lakini nadhani sijui neno "kustaafu" maana yake ni nini. Hivi ni kweli pamoja na kashfa zote alizofanya na anazoendelea kufanya mpaka akalazimika kujiuzulu tunapashwa kumwita EL kwamba ni PM Mstaafu?
Nilidhani atafutiwe sifa nyingine, siyo hiyo. Je, tukimwita mstaafu, tutatumia sifa gani kwa Marehemu Baba wa Taifa, Mzee Mwinyi, Marehemu Kawawa, Warioba, Sumaye nk.
Naomba michango yenu ya mawazo ili hatimaye tupate sifa inayoendana na na ufisadi wake.
Nawakilisha.
Nilidhani atafutiwe sifa nyingine, siyo hiyo. Je, tukimwita mstaafu, tutatumia sifa gani kwa Marehemu Baba wa Taifa, Mzee Mwinyi, Marehemu Kawawa, Warioba, Sumaye nk.
Naomba michango yenu ya mawazo ili hatimaye tupate sifa inayoendana na na ufisadi wake.
Nawakilisha.
Nimeshangaa sana na bado nitaendelea kushangaa na isitoshe serikali ya chama cha mapinduzi kwenye taarifa zenu za habari kuupotosha uma wa watanzania kua eti Eduward Ngoyai Lowasa ni waziri mkuu msaatafu hii ni aibu na sintakubaliana na vyombo vya habari TBC1/Gazeti la Uhuru/Gazeti la Habari leo na viombo vyoote vinavyomilikiwa na serikali ya CCM kuupotosha uma wa watanzania kuhusiana na habari hii husika hapo juu!
Taarifa ya habari ya tarehe 23/10/2011 saa mbili ya usiku nimeona na nimeisikiliza na kumuona bwana Lowasa AKA Nywele Nyeupe akiwa kanisani sijui alikua anatoa rambirambi au alikua anapata maombi kama tulivyomzoea kipindi hiki tokea ajiuzulu na sio amestaafu haachi kuhangaika na makanisa tofauti akitafuta maombi kutokana na imani yake sasa hivi! Eti chombo hiki cha habari cha taifa kuutangazia uma kua waziri mstaafu ndugu Eduward Lowasa! Amesema blablabla na sijui nini!
Tafadhali sana watu wa TBC1 na vyombo vyombo vingine natoa tamko kuwa nitavichukulia sheria za kinidhamu kwa kuupotosha uma kwa kutamka kauli hii! kuanzia sasa nitaweka wanasheria wangu kama nitasikia tena kua mnatamka kua bwana Eduward Lowasa ni waziri mstaafu!
Nataka vyombo vya habari vitamke kua Ndugu Edward Lowasa ni aliyekua waziri mkuu katika serikali ya awamu ya kwanza ya raisi Jakaya Kikwete na akajiuzulu kwa kashfa ya Richmond na kuwasababishia watanzania kukaa kwenye kiza kinene mpaka sasa hivi! Wanasheria wangu wako tayari kwa chombo chochote kama nitasikia tena kauli kama hii.
Nimekuwa nikifuatilia vipindi mbalili vya TBC almost zote (radio $ TV),na wamekuwa wakisisitiza ukweli na uhakika pamoja na kuweka utaifa mbele kwa maendeleo ya Tanzania, ijapokuwa makosa mengi yanaonekana lakini hili si kosa ni tatizo ambalo linakinzana na kauli mbiu yai ya ukweli na uhakika.
Kitendo cha kutuambia kila siku Lowassa ni waziri mkuu mstaafu si kweli!
Nani asiyejua Lowassa alijiuzuru kwa kashfa nzito na akaatamka mwenyewe bungeni kuwa anaachia ngazi? Hilo TBC hawalijui au bado wanaamini alisingiziwa?