Ni haki kufunga mitaa ya umma kwa ibada binafsi?

Ni haki kufunga mitaa ya umma kwa ibada binafsi?

Nimetoa mfano wa Mwananyamala kwa kopa ambapo nikiwa naelekea nikakuta turubai katikati ya barabara. Mita zisizozidi MIA pana uwanja kwa nini sherehe isifanywe uwanjani ?

Wamewaka turubai na kuziba barabara wakati waliokaa kwenye mikeka ndani ya turubai watu watatu tu.

Hureeeee!!! baelezeee.
 
Kiukweli ufungaji holela wa barabara unaudhi

Regardless waliofunga ni dini gani au shughuli gani.... angalau kitu kama msiba ni cha ghafla....

Lakini shughuli za kidini hapana inaudhi....... kusali/kuswali kwako kusiwe kero kwa wengine...na wala shughuli zako za kidini zisiwe kero kwa wengine

Hapa pia kuna wale wanaopiga mahubiri usiku kucha..... mispika mikubwa sauti za juu...walaah... sasa usiombee sauti za mahubiri + kufunga barabara
 
usitoe kauli usizokuwa unaupeo wa kutatua jambo zaid ya kutangaza chuk na ghiriba angalia pia ufinyu wa maeneo nani anapenda kufunga barabara? kwani hizo mambo mikoani zipo? kama zipo ni chache kutokana na eneo husika lilivyofinyu sasa kila mtu anawaza kwenda dar hayo maeneo ya shughuli yanapatikana wap?

Huna hoja ndugu yangu, suala la kufunga barabara alihusiani na kukua kwa miji, ina maana miji inakuwa akili zetu ndio zinadumaa?
 
Duh, tunakoenda sasa siko kwanini tusilalamike barabara inapofungwa kwa
Msafara wa kiongozi fulani Tena unakuta hata saa moja kabla watu hawaruhusiwi
kwanini hukulalamika siku aliyokuja Obama jinsi tulivyonyanyaswa ndani ya nchi yetu
hizo chuki hazina maana.
 
Sawa ....hebu pitia hapo kkoo unaposema waambie tu kwa lugha nzuri watakuelewa.Lakini lingine ni pale lilipo kanisa la kkkt opposite na bahari lilikuwa la waislamu..tuwarudishie.
 
radika
Iwe pande yoyote ile au mpagani kufunga barabara sio vizuri kwanini wasiende sehemu nyingine uko.
 
Last edited by a moderator:
Iwe pande yoyote ile au mpagani kufunga barabara sio vizuri kwanini wasiende sehemu nyingine uko.
Mkihamia miji ya watu,mheshimu taratibu za miji husika.
Mzaliwa wa mji husika,asingeshangaa,angeona ni jambo la kawaida.Barabara ukiona imefungwa ujuwe imeombewa kibali.
 
Msijali mheshimiwa aliahidi atajenga barabara za juu nadhani hili litawekwa kwenye ilani ya chama cha *** then awamu ya tano watalishughulikia ahsante sana...je una jingine leta mezani ya sera

wako mtiiifu **** katika ujenzi wa nchi
 
Mkihamia miji ya watu,mheshimu taratibu za miji husika.
Mzaliwa wa mji husika,asingeshangaa,angeona ni jambo la kawaida.Barabara ukiona imefungwa ujuwe imeombewa kibali.

Nadhani kuhamia sehemu flani au mji hakuhalilishi kufunga barabara ndo mana huwa kuna maeneo yaliyotengwa maalumu. Na sio kugeuza barabara eti kwa kisingizio sijui mji wa wote kwanza ukiwa Mtanzania unaruhusiwa kuishi popote pale. Sasa hyo ya uenyeji haina mashiko kwangu.
 
Mkihamia miji ya watu,mheshimu taratibu za miji husika.
Mzaliwa wa mji husika,asingeshangaa,angeona ni jambo la kawaida.Barabara ukiona imefungwa ujuwe imeombewa kibali.

Mkuu unajua hujajibu hoja, hii point yako sijui ya hao wanaopinga ni wa mkoani haina maana hata kidogo.
Siku yakikukuta, una emergency ya maana halafu barabara imefungwa ndo utaelewa nan wa mkoani na nani wa pwani.
In short kufunga barabara just kwa shughuli binafsi za kikundi flani au watu flani si sahihi hata kidogo.
 
Ukweli ni kuwa sehemu za ibada zilijengwa miaka ya zamani kulingana na idadi ya waumini, sasa watu wameongezeka na kusalia nje.
Ni kuvumiliana tu au kuja na solution nyingine ingawa tatizo halitaisha kamwe kwani kuna mapungufu ya parking pia na miundombinu.

Haya matatizo yapo duniani kote wakati watu wanapotaka kukutana kwa jambo lolote lile liwe ibada au mahubiri. Hata kwa mfano uingereza wakati wa ligi huwezi kupita Chelsea au Tottenham na kwingine itakuchukuwa masaa zaidi ya matatu kuvuka kwa hiyo unashauriwa usipite maeneo hayo, lakini bado watu wanavumilia au kuepuka maeneo hayo.

Tuwe wavumilivu maana tunavumilia mengi zaidi ya ibada kama wauzaji walioibuka siku hizi wa madawa ya jadi na vispika kelele mtindo mmoja na watu wako kimya ingekuwa kwingine huo ndio usumbufu wa hali ya juu. Au mziki usiku mzima wakijua fika kuna wazee na wagonjwa na wanaoenda makazini, hivi hizi kero hatuzioni.

Najiuliza mengi acha niishie hapo tu
 
GeeM
Yes, historia inasema pale ndipo palipokuwa na msikiti wa kwanza ambao ulitumiwa na waarabu wanapofika au kuondoka huku bara.
 
Last edited by a moderator:
Iwe pande yoyote ile au mpagani kufunga barabara sio vizuri kwanini wasiende sehemu nyingine uko.

kumbuka hizo mambo ni za watu wa wapwani na watu wamezikikuta na ni ngumu kuwapangia
 
Point ni kuwa msizibe barabara hata mkiwa watu 100 hio ni public road kila mtu akifanya kama hivyo tutapita wapi?!

wazee wa mzizima wanajua chimbuko lao na kwa nn wanafanya hivyo ila tuliokulia bara tutapata shida sna na waliokulia mzizima na sio wahamiaji kwao kawaida mradi maisha yanasonga
 
Nadhani kuhamia sehemu flani au mji hakuhalilishi kufunga barabara ndo mana huwa kuna maeneo yaliyotengwa maalumu. Na sio kugeuza barabara eti kwa kisingizio sijui mji wa wote kwanza ukiwa Mtanzania unaruhusiwa kuishi popote pale. Sasa hyo ya uenyeji haina mashiko kwangu.
Wewe utakuwa hujatembea kwenye miji tofauti tofauti,sehemu nyingi za bara wanapokuwa na matambiko yao,au shughuli zozote za kimila,maeneo hayo ya nje kidogo ya mji,hakuruhusiwi wasiohusika kupita au kufika maeneo hayo.
 
Wewe utakuwa hujatembea kwenye miji tofauti tofauti,sehemu nyingi za bara wanapokuwa na matambiko yao,au shughuli zozote za kimila,maeneo hayo ya nje kidogo ya mji,hakuruhusiwi wasiohusika kupita au kufika maeneo hayo.

Nimetembea ila huo ujinga haupo kabisa. Kuna specific area na sio barabarani.
 
Back
Top Bottom