Ni aibu kwa Serikali ya Tanzania na ni fedheha mbele ya Wageni kushindwa kuwatambua wapinzani kwenye msiba wa Dkt. Magufuli

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,660
218,147
Nafahamu kwamba siasa za CCM kwa vyama vya upinzani zimejaa uadui na uhasama wa kutisha sana , na ndio maana vyama vya upinzani kwa miaka 6 sasa vimepigwa marufuku kufanya siasa za majukwaa kinyume cha Sheria na Katiba ya nchi.

Lakini hatukutarajia chuki hizo zifike hadi kwenye Msiba wa Rais wa nchi kwa kushindwa kuwatambua viongozi wa upinzani na hasa Chama kikuu kama Chadema ambacho zaidi ya nusu ya Watanzania ni wafuasi wake, huu utamaduni haukuwepo kwenye nchi hii tangu enzi na enzi, ni nani ameuleta na kuusimika?

Natambua kwamba kwenye Maombolezo ya Zanzibar ACT WAZALENDO imetajwa na kutambuliwa kuwepo kwenye msiba huo , lakini itambulike kwamba ACT ni sehemu ya Serikali hasa baada ya kujumuika na ccm kwenye serikali ya umoja wa kitaifa, hivyo chama hiki huwezi kukipa jukumu la kuwakilisha wapinzani.

Mwisho: Ijulikane kwamba tunapoandika haya hatuna maana ya kugombania haki za msiba, la hasha, bali ni lazima tufahamu kwamba Msiba wa Rais ni Msiba wa Kitaifa ni vizuri kushirikisha wadau wote ili kuonyesha mshikamano, ingekuwa aliyekufa ni Katibu Mkuu wa CCM au labda Katibu Mwenezi basi bila shaka msiba huo ungebaki kuwa wa CCM na washirika wao tu.

Kamati ya Mazishi ya Msiba wa Dr Magufuli ijitafakari.

Nitasema kweli daima , Fitna kwangu mwiko .
 
Kwanza Tanzania kwa sasa hatuna chama Kikuu cha Upinzani kama jinsi kusivyo na Kambi RASMI ya Upinzani Bungeni. Hili pamoja na kuonekana linakwaza lakini ni Ukweli UNAOUMA.

Pili Chuki siyo ya CCM kwa Upinzani tu Bali pia Ni CHUKI YA UPINZANI KWA CCM. Ni Matatizo pande zote mbili.

Tatu Unaowaita Chama Kikuu Cha Upinzani Ungewashauri/Ulipaswa Kuwaonyesha wao kwanza kujua kuwa Magufuli alikuwa Rais wa Tanzania, na Kwamba Sherehe waliyoiweka na Furaha waliyoionyesha kupitia Viongozi wao waandamizi wa Chama juu ya Kifo cha Rais haikuwa na Faida zaidi sana ilionyesha Chuki kiasi gani waliyokuwa nayo kwa Rais.

Mwisho ni wachache sana au hawapo kabisa ambao wangeweza Kuvumilia Upuuzi/Ujinga/Upumbavu waliofanya Chadema halafu utegemee kuhusishwa katika Msiba huo.

TWENDE HIVYO HIVYO HADI HAPO KILA UPANDE UTAKAPOTAMBUA HATUNA NCHI NYINGINE ZAIDI YA HII TULIYO NAYO.
 
Aibu kwa nani?

Unapolielezea Jambo kwa kulipima kwa aibu maana yake, Jambo Hilo halina misingi ya kisheria Bali Ni Jambo la mazoea tu.

Halafu kuogopa aibu kwa wageni ni kushindwa kuelewa mnataka Nini.

Kung'ang'ania kuhudhuria mikusanyiko Kama hii Ni kuukana msimamo wenu juu ya Corona.
 
Nafahamu kwamba siasa za CCM kwa vyama vya upinzani zimejaa uadui na uhasama wa kutisha sana , na ndio maana vyama vya upinzani kwa miaka 6 sasa vimepigwa marufuku kufanya siasa za majukwaa kinyume cha Sheria na Katiba ya nchi .

Lakini hatukutarajia chuki hizo zifike hadi kwenye Msiba wa Rais wa nchi kwa kushindwa kuwatambua viongozi wa upinzani na hasa Chama kikuu kama Chadema ambacho zaidi ya nusu ya Watanzania ni wafuasi wake , huu utamaduni haukuwepo kwenye nchi hii tangu enzi na enzi , ni nani ameuleta na kuusimika ?

Natambua kwamba kwenye Maombolezo ya Zanzibar ACT WAZALENDO imetajwa na kutambuliwa kuwepo kwenye msiba huo , lakini itambulike kwamba ACT ni sehemu ya Serikali hasa baada ya kujumuika na ccm kwenye serikali ya umoja wa kitaifa , hivyo chama hiki huwezi kukipa jukumu la kuwakilisha wapinzani .

Mwisho : Ijulikane kwamba tunapoandika haya hatuna maana ya kugombania haki za msiba , la hasha , bali ni lazima tufahamu kwamba Msiba wa Rais ni Msiba wa Kitaifa ni vizuri kushirikisha wadau wote ili kuonyesha mshikamano , ingekuwa aliyekufa ni Katibu Mkuu wa CCM au labda Katibu Mwenezi basi bila shaka msiba huo ungebaki kuwa wa CCM na washirika wao tu .

Kamati ya Mazishi ya Msiba wa Dr Magufuli ijitafakari .

Nitasema kweli daima , Fitna kwangu mwiko .
Jaribuni kutafakari hayo kwa makini mnapokutana wenyewe huko kwenye chama.
Aliyeaga dunia alitangaza adhma yenu kutowepo baada ya 2020.
Inawezekana sana kutotambuliwa kwenu kwenye msiba wake ni kuenzi aliyoyasimamia yeye, kama ilivyo kwa "kutovaa Barakoa" kwa viongozi wote waliokuwa chini yake.

Jitafakarini wenyewe.

Wananchi pekee ndio wenye mamlaka ya kuwafuta msiwepo, kwa hiyo lengo lenu kuu liwe ni kuwashirikisha wananchi kuyajadili haya bila ya mihemuko, wataelewa na mtaendelea na kazi zenu.

Msisababishe mioyo ya hawa walioachiwa ngwe kuwa migumu. Wapeni nafasi wamalize msiba. Wakitulia, wakumbusheni, na someni vyema vitendo vyao.
Sidhani, na kwa kweli niseme kuwa nina hakika; kati yao hayupo mwenye "ujasiri"(?) wa kufanya aliyokuwa anayafanya Marehemu Magufuli.

Kwa hiyo tafuteni njia bora ya kufanya nao kazi, huku mkiendelea na juhudi zenu za kuwafikia wananchi.

Achaneni na kulialia - hakuwafikishi popote, na wala wananchi hawatawaonea huruma kwa kushindwa kwenu.
 
Nafahamu kwamba siasa za CCM kwa vyama vya upinzani zimejaa uadui na uhasama wa kutisha sana , na ndio maana vyama vya upinzani kwa miaka 6 sasa vimepigwa marufuku kufanya siasa za majukwaa kinyume cha Sheria na Katiba ya nchi .

Lakini hatukutarajia chuki hizo zifike hadi kwenye Msiba wa Rais wa nchi kwa kushindwa kuwatambua viongozi wa upinzani na hasa Chama kikuu kama Chadema ambacho zaidi ya nusu ya Watanzania ni wafuasi wake , huu utamaduni haukuwepo kwenye nchi hii tangu enzi na enzi , ni nani ameuleta na kuusimika ?

Natambua kwamba kwenye Maombolezo ya Zanzibar ACT WAZALENDO imetajwa na kutambuliwa kuwepo kwenye msiba huo , lakini itambulike kwamba ACT ni sehemu ya Serikali hasa baada ya kujumuika na ccm kwenye serikali ya umoja wa kitaifa , hivyo chama hiki huwezi kukipa jukumu la kuwakilisha wapinzani .

Mwisho : Ijulikane kwamba tunapoandika haya hatuna maana ya kugombania haki za msiba , la hasha , bali ni lazima tufahamu kwamba Msiba wa Rais ni Msiba wa Kitaifa ni vizuri kushirikisha wadau wote ili kuonyesha mshikamano , ingekuwa aliyekufa ni Katibu Mkuu wa CCM au labda Katibu Mwenezi basi bila shaka msiba huo ungebaki kuwa wa CCM na washirika wao tu .

Kamati ya Mazishi ya Msiba wa Dr Magufuli ijitafakari.

Nitasema kweli daima , Fitna kwangu mwiko .
Planner wa yote haya ni stone, katelephone akiwa kama mwenyekiti wa kamati anayaendeleza tu.
 
Nafahamu kwamba siasa za CCM kwa vyama vya upinzani zimejaa uadui na uhasama wa kutisha sana , na ndio maana vyama vya upinzani kwa miaka 6 sasa vimepigwa marufuku kufanya siasa za majukwaa kinyume cha Sheria na Katiba ya nchi .

Lakini hatukutarajia chuki hizo zifike hadi kwenye Msiba wa Rais wa nchi kwa kushindwa kuwatambua viongozi wa upinzani na hasa Chama kikuu kama Chadema ambacho zaidi ya nusu ya Watanzania ni wafuasi wake , huu utamaduni haukuwepo kwenye nchi hii tangu enzi na enzi , ni nani ameuleta na kuusimika ?

Natambua kwamba kwenye Maombolezo ya Zanzibar ACT WAZALENDO imetajwa na kutambuliwa kuwepo kwenye msiba huo , lakini itambulike kwamba ACT ni sehemu ya Serikali hasa baada ya kujumuika na ccm kwenye serikali ya umoja wa kitaifa , hivyo chama hiki huwezi kukipa jukumu la kuwakilisha wapinzani .

Mwisho : Ijulikane kwamba tunapoandika haya hatuna maana ya kugombania haki za msiba , la hasha , bali ni lazima tufahamu kwamba Msiba wa Rais ni Msiba wa Kitaifa ni vizuri kushirikisha wadau wote ili kuonyesha mshikamano , ingekuwa aliyekufa ni Katibu Mkuu wa CCM au labda Katibu Mwenezi basi bila shaka msiba huo ungebaki kuwa wa CCM na washirika wao tu .

Kamati ya Mazishi ya Msiba wa Dr Magufuli ijitafakari.

Nitasema kweli daima , Fitna kwangu mwiko .
Ushauri na ukweli mtupu Matukio Makubwa kama haya siasa ziwekwe kando
 
Back
Top Bottom