Ngurumo: Mahakama na kikwete, nani mpuuzi?

Ngurumo: Mahakama na kikwete, nani mpuuzi?

Mzito Kabwela

Platinum Member
Joined
Nov 28, 2009
Posts
18,908
Reaction score
7,751
"....................Takrima iliasisiwa na serikali ya Mkapa. Baadhi ya wenzetu wakadhani JK aliye ‘chaguo la Mungu’ hataweza kuivumilia; ataifuta. Mahakama Kuu ilipoifuta, mashabiki wake wakaeneza propaganda kwamba, “imefutwa kwa amri na matakwa ya JK.” Miaka minne baadaye, sasa JK mwenyewe ametangaza urafiki na takrima.

Pale pale, akavunja sheria yake mwenyewe; na akaenda mbali zaidi kupinga uamuzi wa mahakama kuu – akatetea takrima.
Kitendawili ni hiki: mahakama imelaani takrima. Rais anasifia takrima. Ni nani mpuuzi kati ya hawa wawili?..............................."

Ngurumo
Tanzania Daima16/05/2010
 
Mtoto hata akiwa jeuri kiasi gani hawezi kumtukana baba yake. Kikwete ni zao la takrima hivyo hawezi kuilaani lazima ataipamba tu. Fedha ya epa iliyochotwa na kampuni zimwi ya kagoda ndiyo ilitumika kumuuza jk kwa wapiga kura mwaka 2005, hivyo jk akiwa na akili timamu ni lazima asifu takrima. Na ndiyo maana sasa wanatafuta bilioni 50 za kutoa takrma ndiyo maana ana andaa mazingira ya kutoa rushwa wakati wa uchaguzi baadae mwaka huu.
 
Yaani muungwana wetu, pamoja na huo uungwana na rekodi yake ya miaka mi5 hawezi kurudi Ikulu hadi kwa njia ya hongo tena?
 
Tunayakuza tu haya kwa uandishi wetu hafifu na uwezo mdogo wa kufikiri na kuchambua mambo hasa hotuba za JK. Najiuliza mara nyingi kwa nini hotuba za Rais wetu zinapindishwa mara kwa mara. Hii ni kwa manufaa na madhumuni gani hasa?
 
Tunayakuza tu haya kwa uandishi wetu hafifu na uwezo mdogo wa kufikiri na kuchambua mambo hasa hotuba za JK. Najiuliza mara nyingi kwa nini hotuba za Rais wetu zinapindishwa mara kwa mara. Hii ni kwa manufaa na madhumuni gani hasa?

Broda! gimme a break!!!!! Do you want to tell me tht JK do present such philosophical speeches ambazo zinahitaji uwezo mkubwa wa kuchambua ili kuzielewa? Yaani kama ile hotuba ya juzi ya TUCTA imekuzwa?
Mapenzi gani haya????
 
Tunayakuza tu haya kwa uandishi wetu hafifu na uwezo mdogo wa kufikiri na kuchambua mambo hasa hotuba za JK. Najiuliza mara nyingi kwa nini hotuba za Rais wetu zinapindishwa mara kwa mara. Hii ni kwa manufaa na madhumuni gani hasa?
Mkuu hotuba zake hazipindishwi, tatizo kubwa ni yeye mwenyewe. Huwa hajui wapi pa kuweka masihara na wapi pakuonyesha anayezungumza ni Rais. Kauli ni za hovyo hovyo tuu.
 
Broda! gimme a break!!!!! Do you want to tell me tht JK do present such philosophical speeches ambazo zinahitaji uwezo mkubwa wa kuchambua ili kuzielewa? Yaani kama ile hotuba ya juzi ya TUCTA imekuzwa?
Mapenzi gani haya????

Imekuzwa mno. Imepata tafsiri nyingi kama mistari iliyomo kwenye Biblia au Quran. Kwa nini inakuwa hivi?
 
Mkuu hotuba zake hazipindishwi, tatizo kubwa ni yeye mwenyewe. Huwa hajui wapi pa kuweka masihara na wapi pakuonyesha anayezungumza ni Rais. Kauli ni za hovyo hovyo tuu.

Labda mnataka ahutubie kama Makamu wa Rais, Dr AM Shain? Mnamchukia mno Rais wetu sote.
 
Hotuba za hovyohovyo zinajadiliwa hovyohovyo hakuna kosa. Mbona za kambarage hazijajadiliwa hovyohovyo hadi leo.abadilike la sivyo tunae.
 
Labda mnataka ahutubie kama Makamu wa Rais, Dr AM Shain? Mnamchukia mno Rais wetu sote.
Uko wrong mkuu,hakuna anayeweza kumchukia Rais wa nchi yake kama atakuwa anafanya yale aliyopaswa kufanya wakati anaomba hiyo kazi. Tunaipenda zaidi nchi yetu, na yeyote anayeitendea nchi hii mambo ya hovyo hovyo anaitafuta chuki ya wazalendo wa Tanzania.
 
Tunayakuza tu haya kwa uandishi wetu hafifu na uwezo mdogo wa kufikiri na kuchambua mambo hasa hotuba za JK. Najiuliza mara nyingi kwa nini hotuba za Rais wetu zinapindishwa mara kwa mara. Hii ni kwa manufaa na madhumuni gani hasa?

Nani anapindisha Hotuba?
Muwasilishaji (Kikwete) ama wanaomnukuu neno kwa neno?
 
Mkuu hotuba zake hazipindishwi, tatizo kubwa ni yeye mwenyewe. Huwa hajui wapi pa kuweka masihara na wapi pakuonyesha anayezungumza ni Rais. Kauli ni za hovyo hovyo tuu.

Haswaaa!
Hovyo kweli kweli!
Wildcard, ungekuwa umesikiliza hotuba aliyoitoa Mei 3 akiwajibu wafanyakazi wa Tanzania, au mwaka juzi alipokuwa anaisagia filamu ya Sauper ya Darwin's Nightmare (mapanki) ndipo ungejua kwamba hatuna raisi makini.
Hovyo kabisa!
 
Back
Top Bottom