Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,733
- 218,322
Ukweli ni Kwamba, lengo la ziara ya Tundu Lissu na Chama chake, kupeleka Oparesheni 255 kwenye maeneo ya hifadhi ya Ngorongoro ilikuwa ni kuitangazia dunia unyama wanaofanyiwa Wamasai na Serikali ya Tanzania, wa kuwahamisha kwenye maeneo yao mithili ya nguruwe ama mifugo mingine.
Lissu alifahamu Jinsi viongozi walivyohongwa pesa na kukubali kuwaswaga Wamasai na kuwapeleka Handeni, na alijua kwamba aking'ang'ania ziara ile angekamatwa, na kukamatwa kwake kungeiamsha dunia kuelewa zaidi kuhusu yanayotendwa Ngorongoro , Mtego huu umefanikiwa kirahisi sana!
Ikumbukwe kwamba Tundu Lissu ni MTU WA 3 KWA UMAARUFU NCHINI TANZANIA tangu kuumbwa kwa Taifa hili , Wa kwanza ni Julius Nyerere , sasa unapokamata mtu kama huyu kwa sababu za kijinga kama hizi zilizotolewa na Polisi wa Tanzania , unakuwa moja kwa moja umeiamsha dunia na kuifanya ianze kuitupia Jicho Jambo hili kwa nguvu zaidi.
Lissu alijua kila kitu ila aliamua kujitoa Muhanga ili kuokoa Wamasai , Yaani ni kama Vile Yesu Kristo alivyosulubiwa Msalabani ili kuwaokoa wanadamu , Kimsingi Lissu amefanikiwa Malengo yake kwa 100% , Hii ndio tofauti kati ya Akili ndogo na Akili kubwa.
Lissu alifahamu Jinsi viongozi walivyohongwa pesa na kukubali kuwaswaga Wamasai na kuwapeleka Handeni, na alijua kwamba aking'ang'ania ziara ile angekamatwa, na kukamatwa kwake kungeiamsha dunia kuelewa zaidi kuhusu yanayotendwa Ngorongoro , Mtego huu umefanikiwa kirahisi sana!
Ikumbukwe kwamba Tundu Lissu ni MTU WA 3 KWA UMAARUFU NCHINI TANZANIA tangu kuumbwa kwa Taifa hili , Wa kwanza ni Julius Nyerere , sasa unapokamata mtu kama huyu kwa sababu za kijinga kama hizi zilizotolewa na Polisi wa Tanzania , unakuwa moja kwa moja umeiamsha dunia na kuifanya ianze kuitupia Jicho Jambo hili kwa nguvu zaidi.
Lissu alijua kila kitu ila aliamua kujitoa Muhanga ili kuokoa Wamasai , Yaani ni kama Vile Yesu Kristo alivyosulubiwa Msalabani ili kuwaokoa wanadamu , Kimsingi Lissu amefanikiwa Malengo yake kwa 100% , Hii ndio tofauti kati ya Akili ndogo na Akili kubwa.