Sikonge
JF-Expert Member
- Jan 19, 2008
- 11,550
- 6,062
Pana wakati nikiwa nimekuja kutembelea jamaa zangu pale Dar, nilialikwa na binamu yetu ambaye amezaliwa na kukulia Dar uswahilini na kashakuwa kama Mzaramo.
Siku hiyo alikuwa anatoa wajukuu zake wawili (kutoa mwali) wali.
Wapiga Mchiriku walikuwa wamealikwa siku hiyo. Ila hawa jamaa ni wapuuzi sana maana kila mwaliko wanachukua na kasheshe ni kuwa watafika saa ngapi kwako.
Kwa binamu yangu walikuwa wafike saa 15 mchana ila wazembe wale wakaenda sehemu nyingine kwanza na wakaja zaa 18 jioni. Binamu yangu alikuwa kachukia sana na kuweka mkwara mzito (ndivyo nilivyoona mie) kuwa wakija atawafukuza.
Mie na kijana mmoja tulichaguliwa kutoa wali hao wawili. Baada ya kuwatoa, nilikaa na huyo kijana na akaanza kuniambia tabia ya wapiga Mchiriku. Jamaa ni wazembe sana, wachelewaji na milele usiwaazime vyombo vya mziki maana hawajali kabisa chombo cha mtu hata chombo chao.
Jamaa walipofika, wakafungua vyombo vyao harakaharaka, wakavuta waya wa umeme hadi ndani na binamu yangu muda wote anawaambia waondoke kwani wamechelewa na hana hamu nao kabisa. Wale jamaa hawakujali sana maneno yake na wakaendelea na shughuli zao kama vile hayupo.
Ilipopita dakika tano, MCHIRIKU huoo .... " ehhh, kwa baba na mama ......."
Kuangalia pembeni, namuona binamu yangu anaHAHA. Mwenyewe kaacha mchiriku, yuko pembeni na kajifunga GUNIA lake safi kabisa. Anaondoka Mchiriku kwa zile step za kuchezesha mabega, kubaraza miguu na kurukaruka huku akiangalia kushoto na kulia (MSONDO walikuwa wakaiga hii staili).
Siku hiyo ilikuwa kama vile nimeletwa dunia nyingine kabisa kwa kuangalia vituko hivyo kwa mara ya kwanza. Funga kazi ilikuwa kuona mtoto wa mwaka na miezi kadhaa anayejifunza kusimama dede, alisimama kwa shidashida na kunengua step kadhaa za Mchiriku na akaanguka (miguu ilikuwa haina nguvu bado) ila mchiriku aliurudi.
Toka siku hiyo, huwa nikiuona au kuusikia tu Mchiriku, mie lazima nipite hapo nifurahi kidogo vituko vya Wazaramo.
Kuna mtu anaweza kunipatia habari za ngoma hii? Vyombo wanavyotumia vinaitwaje na kwa nini wanapiga Ki-Stool na kutumia vingoma vidogovidogo? Ni umasikini au uvivu wa Wazaramo?
Kwa wale wapenzi kama mie, Mchiriku kadhaa nawawekea:
Kuna comments nimesoma zinasema "Kulikuwa kuna kundi moja wahuni wanaitwa Hisani hao walikuwa wakipiga ngoma ikisha unakuwa ushaiibiwa."
Siku hiyo alikuwa anatoa wajukuu zake wawili (kutoa mwali) wali.
Wapiga Mchiriku walikuwa wamealikwa siku hiyo. Ila hawa jamaa ni wapuuzi sana maana kila mwaliko wanachukua na kasheshe ni kuwa watafika saa ngapi kwako.
Kwa binamu yangu walikuwa wafike saa 15 mchana ila wazembe wale wakaenda sehemu nyingine kwanza na wakaja zaa 18 jioni. Binamu yangu alikuwa kachukia sana na kuweka mkwara mzito (ndivyo nilivyoona mie) kuwa wakija atawafukuza.
Mie na kijana mmoja tulichaguliwa kutoa wali hao wawili. Baada ya kuwatoa, nilikaa na huyo kijana na akaanza kuniambia tabia ya wapiga Mchiriku. Jamaa ni wazembe sana, wachelewaji na milele usiwaazime vyombo vya mziki maana hawajali kabisa chombo cha mtu hata chombo chao.
Jamaa walipofika, wakafungua vyombo vyao harakaharaka, wakavuta waya wa umeme hadi ndani na binamu yangu muda wote anawaambia waondoke kwani wamechelewa na hana hamu nao kabisa. Wale jamaa hawakujali sana maneno yake na wakaendelea na shughuli zao kama vile hayupo.
Ilipopita dakika tano, MCHIRIKU huoo .... " ehhh, kwa baba na mama ......."
Kuangalia pembeni, namuona binamu yangu anaHAHA. Mwenyewe kaacha mchiriku, yuko pembeni na kajifunga GUNIA lake safi kabisa. Anaondoka Mchiriku kwa zile step za kuchezesha mabega, kubaraza miguu na kurukaruka huku akiangalia kushoto na kulia (MSONDO walikuwa wakaiga hii staili).
Siku hiyo ilikuwa kama vile nimeletwa dunia nyingine kabisa kwa kuangalia vituko hivyo kwa mara ya kwanza. Funga kazi ilikuwa kuona mtoto wa mwaka na miezi kadhaa anayejifunza kusimama dede, alisimama kwa shidashida na kunengua step kadhaa za Mchiriku na akaanguka (miguu ilikuwa haina nguvu bado) ila mchiriku aliurudi.
Toka siku hiyo, huwa nikiuona au kuusikia tu Mchiriku, mie lazima nipite hapo nifurahi kidogo vituko vya Wazaramo.
Kuna mtu anaweza kunipatia habari za ngoma hii? Vyombo wanavyotumia vinaitwaje na kwa nini wanapiga Ki-Stool na kutumia vingoma vidogovidogo? Ni umasikini au uvivu wa Wazaramo?
Kwa wale wapenzi kama mie, Mchiriku kadhaa nawawekea:
Kuna comments nimesoma zinasema "Kulikuwa kuna kundi moja wahuni wanaitwa Hisani hao walikuwa wakipiga ngoma ikisha unakuwa ushaiibiwa."
Last edited by a moderator: