Ngoma ya Diamond na Ne-yo imevuja

Ngoma ya Diamond na Ne-yo imevuja

Msitokwe na mipovu wapenz wa diamond naona baadhi washapandwa na blood pressure, tukosoane kistaarabu na kwa facts.....mimi sina tatizo nae kuhusu mafanikio yake kimziki binafs namkubali ila nyimbo ya marry you ni mbovu...labda kama nasoma humu kua sio nyimbo yenyewe kwamba imeunganishwa vipande na wahuni..how comes?,
 
Kwa kawaida msanii anayetokea sehemu ambazo ladha zake haziko kimataifa hua inambidi abadilishe mtindo wa kuimba/ kurap na hata beat hubadilishwa ili kumpa nafasi yule mwenye ladha ya kimataifa atambe.

Mfano AY alivyoimba na Lil Romeo ilibidi asirap kabisa ili kumpa nafasi Romeo, 2 Face alivyoimba na T pain ikabidi beat iwe ya reggae ili T pain apate pa kuhemea. Drake alijikaza kwenye Ojuelegba ya Wizkid lakini kama unajua rap utajua tu pale hakua Drake wa siku zote.

Kwa vyovyote Diamond ilibidi awe na beat ambayo Neyo angekaa na yeye angekaa, matokeo yake imewekwa beat ambayo haiwezi kukubalika Afrika wala huko Marekani na hata mashairi hayako poa, hii beat ni ya klabu tena uwe umelewa, wimbo hauko poa kwa kifupi katika nyanja zote (labda video ikitoka).

mkuu uko sahii inabidi afuatilie collabo za AY aone alivyowafanya akina SEAN KINGSTONE,LIL ROMEO,LAMYA,MISS TRINITY,P.SQUARE
 
DIAMOND KAMUANGALIE ALIKIBA NA NEYO KWENYE ONE STAND WALIVYOIMBA BEAT KALI SAUTI TAMU AU AKAANGALIE ONE 8 ALIKIBA NA R.KELLY WALIVYOIMBA,YEYE ANALETA BEAT ZA MATARUMBETA KWA MSANII ANAYEIMBA RNB NA POP NI JAMBO LA AJABU SANA
 
Hata Best Naso pia nae anahitaji mashabiki, mbona kila siku Diamond tu? Kama mziki wake mbaya achana nae huna haja ya kumfungulia uzi. Akina Ben Poh, Jux, Kiba, Mo music, Baraka, na wengineo wanatosha sio lazima Mondi tu
 
  • Thanks
Reactions: ovi
Weka akiba ya maneno..hizo unazozisikia ni Demo tu ya kuwaweka watu wakae tayari,.wimbo wenyewe hauna melody hiyo.

Utakuja kutamani kuufuta huu Uzi siku nyimbo itakapoachiwa mkuu
Ndugu labda useme hyo bado ni demo tu kwa hyo track yenye mixing kamili inakuja, ila kuhusu instrumental,verses na hizo melodi ndiyo hvyohivyo. Mleta mada ana uchungu wa kweli kwa kuwa anaamini wimbo aliousikia ndio hivyohivyo ulivyo ilihali anaamini wimbo ni mzuri ila haukustahili kuwa kwenye level hizo hasa hasa upande wa mixing. Labda ulivyomwambia hyo ni demo laweza kuwa jibu sahihi,ila masikitiko yake yupo sahihi pia!
 


Usikilize nakuahidi hatajutia kuusikiliza, ni noumeeerrr!! Chibu kama kawaida yake ametupia mistari kuntu;

"Ooohh baby hadithi hadithi utamu kolea, ooohh baby mi najihisi hamu kuongea, ooohh baby yale yaliyo ndani ya mtimaaa nikuelzeee.......... I want to marry you ooohh la la la ooh la la la, I want to marry you oohh la la la ooh la la la.."



Kama vipi nikutumie aisee! Nimeuweka repeate toka Jana.. Hii ngoma Balaaaa

When I look at you...
.......
Niko mzima sababu yako wewe tu...

When you talk to me I hear the angels I can't even see.

I want to marry yo....o lalalalalaalaaaaa
Olalalalaaaaaa

Venye kupenda maradhi ya moyo nitampenda nani
Sio mfupa mwenzio kibogoyo...
Kutwa wanakumendea mi pressure kizunguzungu...

When you smile....when you smile...

Oooooh japo kidogo...eeeeh nideke deke...
Nidekeze mama...


Ooooh I want to marry you...o lalalalalalaaaaaa
Twende kwa mama baba...o lalalalalaaaaaa
Ah twende kwa baba na mama yanguuuu

Umenifanya nikausikiliza huu wimbo zaidi ya mara 3!
Unbelievable!
 
Aisee...watu wanatetea hata wasicho kijua, mwenyewe mwenye nyimbo anasema nyimbo ineshatoka na inasambazwa ulaya (tunayo isikiliza) lakini wateja ndio ma producer na wana dai eti ni vipande vimeunganishwa/demo mara sio yenyewe...kwa maana hii ina maanisha kwa wanavyo dai ni vipande ni kuwa wana aknowledge kua nyimbo ni mbovu so wanasubiri imaliziwe ...ushabiki unahitaji moyo
 
Hata Best Naso pia nae anahitaji mashabiki, mbona kila siku Diamond tu? Kama mziki wake mbaya achana nae huna haja ya kumfungulia uzi. Akina Ben Poh, Jux, Kiba, Mo music, Baraka, na wengineo wanatosha sio lazima Mondi tu
Best naso?? Anyway Mzik wa diamomd sio mbaya lakkn nyimbo aliyoimba na neyo ndio mbovu tofaut na expectations zangu.
 
Ndugu labda useme hyo bado ni demo tu kwa hyo track yenye mixing kamili inakuja, ila kuhusu instrumental,verses na hizo melodi ndiyo hvyohivyo. Mleta mada ana uchungu wa kweli kwa kuwa anaamini wimbo aliousikia ndio hivyohivyo ulivyo ilihali anaamini wimbo ni mzuri ila haukustahili kuwa kwenye level hizo hasa hasa upande wa mixing. Labda ulivyomwambia hyo ni demo laweza kuwa jibu sahihi,ila masikitiko yake yupo sahihi pia!
Thanks mkuu umenielewa vizuri sawia.
 
Humu kila kona ni domo tu,leteni na wengine tuwape kiki jameni
Hadi mtakapomuheshimu kwa kumuita kwa jina lake la kisanii ama jina lake halsi ndio tutaleta za wengine na sio kumuita hayo majina yenu ya dharau tutaendelea kutupia tu haabar za diamond platnumz hadi internet i-break down
 
Back
Top Bottom