Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Ngoma CCM, CHADEMA Arusha bado mbichi
*Mbunge kutoka Tanga ashiriki tena uchaguzi
*CHADEMA waususia, wasema hawashiriki uhuni
Na Glory Mhiliwa, Arusha
MBUNGE wa Viti Maalumu mkoa wa Tanga kupitia CCM, Bi. Mary Chatanda jana alizidi kuleta mvutano wa
kisiasa baada ya kushiriki kwenye uchaguzi Jumuia ya Serikali za Mitaa Tanzania (ALAT) mkoa wa Arusha na kusababisha wajumbe wa CHADEMA kuususia.
Hii ni mara pili kwa mbunge huyo kupitia Mkoa wa Tanga kuzua tafrani kama hiyo baada ya kushiriki uchaguzi wa meya na naibu wake katika Manipaa ya Arusha, hatua iliyopingwa na madiwani wa CHADEMA, huku CCM wakisisitiza kuwa ni halali kufanya hivyo.
Kutokana na kitendo cha Bi. Chatanda ambaye pia ni Katibu wa CCM Mkoa wa Arusha, wajumbe wa CHADEMA waliondoka katika mkutano huo wakisema wasingewe kushiriki kuchakachua sheria kwa kuchagua wajumbe wa ALAT, huku akimshirikishwa mjumbe haramu.
Hata hivyo, vigogo wa CCM ambao ni wabunge mkoani Arusha na wajumbe wa kikao hicho, Bw. Edward Lowassa (Monduli), Lekule Laizer (Longido), Bw. Goodluck Ole Medeye (Arumeru Magharibi), Bw. Jeremiah Sumari (Arumeru Mashariki) pamoja na Meya anayelalamikiwa wa Manispaa ya Arusha, Bw. Gaudence Lyimo hawakuhudhuria.
Kikao hicho kiliendeshwa na mwenyekiti wa muda, Bw. Ismail Katamboi, ambaye ni diwani wa Kata ya Kisongo, ambaye alisema kukuwapo kwa wajumbe sita wa CHADEMA siyo sababu ya kuwazuia kuendelea na uchaguzi huo.
Akizungumza na waandishi wa habari nje ya ukumbi, Mbunge wa Arusha Mjini, Bw. Godbles Lema alisema, "Sisi tumetoka ndani ya kikao hiki kwa sababu ya huyu Bi. Mary Chatanda ambaye ni mbunge wa Tanga, iweje leo apige kura za kuchagua wawakilishi wa mkoa Arusha," alisema Lema.
Alisema kuwa kinachofanyika sasa kwa Mkoa wa Arusha ni uhuni na siyo demokrasia, hivyo bora wawaachie wenye chama tawala wafanye kila wanachotaka, ila wao hawako
tayari kushiriki kuchakachua sheria kwa kuchagua wajumbe, huku wakimshirikisha mjumbe haramu.
Kikao hicho kilitakiwa kuchagua, mwakilishi ALAT Taifa, Mwenyekiti na makamu wake mkoa, katibu na Mweka hazina.
Pamoja na Bw. Lema wajumbe wengine wa CHADEMA waliosusa uchaguzi huo ni Bi. Cecilia Paleso, Diwani Viti Maalum- Karatu, Lazaro Maasai, Mwenyekiti Halmashauri ya Karatu, Joyce Mukya, Mbunge Viti maalumu Arusha, Winner Kitembe, Diwani wa Karatu na Mchungaji Israel Natse ambaye ni Mbunge Karatu.
Kikao hicho kilitakiwa kuwa na wajumbe halali 40, lakini baada ya wajumbe sita wa CHADEMA kutoka na wengine ambao hawakuhudhuria, walibaki 28 wa CCM ambao waliendelea, na kumchagua Bw. Godfrey Majola, mwenyekiti wa Halmashauri ya Meru kuwa Mwenyekiti wa ALAT mkoa.
Msuguano huo umeendelea kutoka mkoani Arusha wakati vumbi lililotimka kutokana na polisi kuzima maandamano wa CHADEMA kupinga uchaguzi wa meya likiwa halitatua.
Katika tukio hilo, watu watatu waliripotiwa kuuawa na polisi kwa risasi na wengine zaidi ya 30 kujeruhiwa, na chama hicho kimendaa mazishi ya 'kitaifa' yatakayofanyika katika viwanja vya NMC kesho.
Katika hatua nyingine, Anneth Kagenda anaripoti kuwa Baraza la Wazee wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, limewataka viongozi wa dini kukaa kimya na kutojiingiza kwenye siasa kwa kutoa msimamo kuhusu suala hilo la Arusha kwa madai kuwa kufanya hivyo kunaweza kuleta maafa makubwa nchini.
Hayo yalisemwa jijini Dar es Salaam jana, na Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Bw. Mohamed Mtulia wakati akitoa tamko la kukemea vurugu za Mkoani Arusha zilizotokea Januari 5, 2011.
Alisema kuwa wamesikitishwa na kauli hizo ambazo zinaashiria matakwa ya kidini katika masuala ya kisiasa, kwa kuwa jambo hilo likiachiwa litaitumbukiza nchi katika machafuko ya kidini.
"Sisi wazee tunawaomba maaskofu na viongozi wengine wote wa kidini kuiacha siasa kwa wanasiasa, kwani kitendo cha maaskofu wa Arusha kukataa kumtambua Meya wa Jiji hilo ambaye pia amekataliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinaleta wasiwasi wa kujitokeza viongozi wengine wa kidini na kujipa mamlaka ya kutowatambua viongozi wasiowakubali kama walivyofanya maaskofu hao," alisema Katibu Mtulia.
Alisema kuwa wanaamini kwamba Dkt. Willibrod Slaa aligombea urais katika uchaguzi uliopita wa mwaka 2010 na kama angekuwa 'chaguo la Mungu' basi angekuwa Rais na Amiri Jeshi Mkuu wa nchi, na bila shaka asingeridhia Mwenyekiti au Katibu wa chama chochote cha siasa apinge kwa maneno na vitendo, amri halali za mamlaka za kisheria zilizoundwa kwa mujibu wa katiba na sheria za nchi.
"Pamoja na kusikitishwa na nguvu iliyotumika ni wajibu wetu kuitafakari nguvu hiyo na je, ilikuwa lazima itumike au haikuwa lazima, hivi kikundi cha raia kinachoelekea kituo cha polisi kwa ajili ya kuwatoa watuhumiwa kwa nguvu kimedhamilia nini, na je, jamii inafahamu nguvu waliyonayo raia hao na wanaowaunga mkono?" alihoji Bw. Mtulia.
Aidha alisema kuwa wazee hao wanaamini kuwa endapo uvamizi wa kituo cha polisi ambacho kinawahifadhi watuhumiwa, pamoja na silaha na nyaraka muhimu ungefanikiwa na silaha zikaangukia mikononi mwa raia wa kawaida wasio na nia njema, kungekuwa na uwezekano mkubwa wa kutumika vibaya na kuleta madhara makubwa.
"Ni dhahiri kuwa waliokusudia kuvamia kituo hicho wangefanikiwa na kupora silaha ili zisaidie kuwatoa watuhumiwa, hali ingekuwa mbaya sana na pia kama angalizo la Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) lingefuatwa, yaliyotokea yasingetokea," alisema.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza hilo Bw. Athuman Mwinyimvua alisema kuwa wanatoa pole kwa wale wote walioathiriwa na vurugu zile kwa kupoteza mali huku wengine wakipoteza maisha na wale waliojeruhiwa.
25 Maoni:
Anonymous said... Mohamed Mtulia, acha kuongea upuuzi kama huu wakati raia wasio na hatia wameuawa kwa uroho wa madaraka ya viongozi wa CCM. Unaleta dhana y akufikirika kuwa eti CHADEMA walikwenda kuvamia kituo cha polisi ili wapore silaha? Hayo ni mawazo mgando. Halafu kumbuka wewe huna hadhi ya kuwaelekeza maaskofu na mapadre ni nini cha kufanya. Wewe na mashekh wenzako fanyeni yenu ya Koran misikitini, yanayowahusu wa Biblia waachieni wenyewe. Excuse me!
January 10, 2011 8:34 PM
Anonymous said... RIP nyie wazee njaa. Majina yote yanaja ulikana ni dini gani? Hivi kwa nini hatuna shule za maana au hospital za maana za kiislam? angalia vyuo vikuu vingapi, huduma ngapi zinazotolewa na waislam. Badala ya kujenga shule, hospital mnajenga misikiti tena barabani!!!! Ujinga muda wenu wa kufikiri umekwisha sanda zinawasubiri. Hivi da ndo kuna wazee?? kazi kunywa kahawa basi. Narudia RIP
January 10, 2011 8:39 PM
Anonymous said... hivi hawa niwazee au uchwala msome madarasa hayata wakomboa ukisikia tu jina limeanzia na mzee wa barakashee utajua nipumbu tu zinazo fuata ooo udini hivi hamna hoja wa kristu wangekuwa wadini wangewachagua hawa ndg zenu wanaolipeleke taifa kudidimia kiuchumi mjue kuongoza hamwezi ni jaziba ya udini tu kila kukicha.
January 10, 2011 9:08 PM
Anonymous said... Kwa kweli kwa hili serkali ya sisiemu haiwezi kukwepa lawama.wamaona kabisa kuwa kuna tatizo bado wanaendelea kuruhusu chaguzi za namna hiyo kufanyika,wanataka wao tu ndio wawe madarakani hata kama hawakuwekwa na nguvu ya wananchi.kwani uchaguzi ukirudiwa Arusha kwa uangalizi na kufuata sheria zote za uchaguzi na ikaonekana ccm wameshida chadema haiwezi lalamika.lakini kwa uroho wa madaraka wanapindisha sheria na kuonekana wameshinda,pia hembu liwekeni wazi nani anaestahili kupiga kura ktk kumchagua meya wa jiji???mtu mbaya sana anaeharibu amani nchini ni pamoja na Yusufu Makamba,pia hata jeshi la polisi,huyu mama pia mbunge wa tanga aangaliwe pia,
January 10, 2011 9:38 PM
Anonymous said... Hawa ndio wazee wanaomshauri Rais na kula mapochopocho ya Ikulu. Wanafikiri TZ ni mali yao. Au wanafikiri wangealikwa kwenda kula maharagwe. Kwa taarifa yenu hakuna maharagwe ni majonzi. Huo udini ni nyinyi mnao kama kawaida yenu, na ndio maana nchi zote zenye waislam ni matatizo matutpu. Kama sio kuwasaidia kwenye Elimu sijui mngefa je. Mnachukua kuvuli cha udini muanze kufunga mabomu kiunoni na kutumia makwanja yenu yaliyoko humo msikitini.
January 10, 2011 9:49 PM
Anonymous said... Chadema (Chama Cha Demokrasia na Maandamano) Nyie ndio wa kulaumiwa kwa nini hamkutii amri halali ya kutokuandamana iliyotolewa na IGP>. Nyie ndio mmesababisha mambo yote haya. Namsihi Hakimu awafunge wote walioshutakiwa kwa kutotii sheria miaka 10 kila Mmoja nyie ndio mlisababisha watu wakauawa kama mngeenda tu kwenye mkutano kistaarabu yote hayao yasingetokea lakaini mkaandamana kinyime cha sheria mnataka mfnaye mambo yenu manavyotaka nyinyi ili jumuia ya kimataifa iwaone CCm wabaya nyie ndio wabaya. Haya na hao maaskofu nduguze Slaa hawamtambui Meyawa Arusha ni maajabu wao ni kina nanai au walitaka Slaa awe rais ili nchi iwe ya kikirito hatukubali siye waislamu
January 10, 2011 9:49 PM
pETRO eUSEBIUS mSELEWA said... Chatandaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaeeeeeeeeeeeeeeee! Ondooooooooooooooooooookaaaaaaaa kwa jina la Yesu!
January 10, 2011 9:50 PM
Anonymous said... Huyo mama Chatanda damu iliomwagika imwangukie yeye,na akatubu makosa hayo vinginevyo dhamira itamshtaki,
January 10, 2011 9:59 PM
Anonymous said... Chatanda kaombe radhi watakunyang'anya ukristo wako. Kumbuka yaliowafika wakristo wa sumbawanga walioikataa Chadema Kanisa limewafanya nini? Umemsikia Malecela alivyokuita mtovu wa nidhamu.
Hivi kwa nini chama cha CHADEMA kisifutwe kwa kuubeba udini. Kwa nini Mbowe na Padre Slaa wasijiuzulu kwa kushindwa kuwachunga kondoo zao na kuwasabibishia maafa ambayo yanaepukika.
Balaa la umasikini la Nchi hii limeletwa na Nyerere. Tuwe w Kweli. Ilifikia watu wanakwenda uchi, wakalazimishwa kula sembe la Yanga, wakakosa hata sabuni ya kuogea na dawa ya meno,tukawa tutanunua chakula kwa kadi na kiwango alichoweka yeye.Maovu matupu. Watu kuwekwa ndani bila ya kufikishwa mahakamani. Ubabe mtupu. Lakini hatawasikia Maaskofu kulaani au kukosoa utawala huwo. Ni Unafiki wa kikatoliki na Udini tu ndio uliotawala nchi hii hivi sasa, Nayote kwa sababu CHADEMA chama cha Maaskofu kimeshindwa uchaguzi na kitaendelea kushindwa maisha. Kwa vile dhamira zao zinajuulikana sasa na kila mpenda amani
January 10, 2011 10:18 PM
Anonymous said... Nimependa maoni yoote leo ah. Ntalala kwa raha sana.
January 10, 2011 10:20 PM
Anonymous said... sasa nimeelewa kwa nini tunaambiwa viongozi wa dini wasijiingize kwenye siasa. Wakitaka wavue majoho waingie kwenye ulingo.
Matoeo ni haya hapa.soma wachangiaji.Mgogoro wa Chadema na CCM umekiwa matusi baina ya wakristo na waislamu. Vitone vya matusi aina hii vinaweza kuleta mfarakano usiotegemewa kwenye jamii.
Na hili limekuja baada ya viongozi wa dini kuanza kuleta chokochoko au kuegemea upande mmoja.
hatari mti na macho
January 10, 2011 10:25 PM
Anonymous said... Hili limekuja baada ya CCM kutaka kwa nguvu kutawala bila kufuata kanuni. Ntu yeyote anao uhuru wa kuhimiza amani; na zaidi sana viongozi wa dini. Maoni ya kuleta amani yasichukuliwe kama maoni ya udini. Udini sasa unaletwa na Chatanda na mashekh wanaojibu maaskofu kana kwamba hawapaswi kukemea maovu ili kudumisha amani nchini. Tunapotoa maoni tufikirie kwa kichwa si kwa tumbo!
January 10, 2011 10:36 PM
Anonymous said... HIVI NYIE WAFUASI WA CHADEMA MMEKUWA WEHU? WENGINE WAKITOA MAONI MNAWATUKANA NA KUWAKEBEHI LAKINI MAASKOFU WAKISEMA SAWA,HUO NI UJINGA WA KUPINDUKIA,KAMA MAASKOFU WAKISEMA NI HAKI YAO KUTOA MAONI,KAMA WAISLAMU WA MKOA WA ARUSHA WALISEMA NI HAKI YAO YA KUTOA MAONI NA KAMA HAO WAZEE WA DAR-ES-SALAAM WALISEMA PIA NI HAKI YAO YA KUTOA MAONI,LEO KUNA GAZETI LINASEMA MWANZA KIKUNDI FULANI CHA WATU WANATAKA KIKWETE AJIUZULU NAO NI HAKI YAO KUTOA MAONI,NYIE MKISHA ONA JINA LA KIISLAMU TU TAYARI VICHAA VINAWAPANDA. KOMENI WAACHIENI WENYE MAONI YAO WATOE.
January 10, 2011 10:38 PM
Anonymous said... Wewe mbunge wa Arusha unaoongoza kihuni hapo,waeleze watu sheria za nchi zinasemaje kuhusu diwani wa kuteuliwa kutoka katika vyama na haki zake sio kila siku kuleta migongano isiyo na tija kwa jiji letu la Arusha. weka sheria wazi inasemaje? kutuambia tu huyu ni mtu wa Tanga wakati ni katibu wa CCM wa Arusha na anaishi Arusha haitoshi,wewe kwenu ni Moshi na sio Arusha basi nenda kwenu Moshi.
January 10, 2011 10:45 PM
Anonymous said... Mary Chatanda ni muislamu? Acha ujuha wewe, watu wanaotoa maoni yao, nao piani haki yao kufanya hivyo. Upo hapo!
January 10, 2011 10:59 PM
Anonymous said... MNALOLILETEA MZAHA LEO KWA KUANDIKA UTUMBO KWA KUTAKA MJIFURAHISHE, KESHO LITAWALIZA. NA MTALIA NYOTE BILA KUJALI KUWA WANA CCM AU CHADEMA. NG'ANG'ANIENI TU MADARAKA DAWA YA WOTE SASA IKOJIKONI. NA TUKANENI SANA WACHUNGAJI TENA KWANGUVU ZOTE, CHAMOTO KITAKUJA IKIWA TU NIDHAMU YA NNCHI HAITARUDISHWA NA VIONGOZI WA CCM WENYE UROHO WA MADARAKA. NANYI CHADEMA ACHENI MAMBO HAYA YA KUPIGANIA UKOMBOZI WA MTANZANIA, KWANI KWASASA SI WAKATI WAKE, MTAJICHOSHA BURE NA HAKUNA LITAKALOSAIDIA, MWAJUA FIKA KUWA SERIKALI YA TZ IMOMIKONONI MWA KIKWETE NA AMEMILIKI HATA JESHI LA POLISI NA KWAO SASA KUUWA WATANZANIA WA FUASI WA VYAMA VYA UPINZANI NI KUTAKA WAPANDISHWE VYEO KILA MTU ANAJUA KWA SERA SASA YA CCM NI KUUWA WATANZANIA WASIO WAFUASI WA CCM. CHADEMA TULIENI WAACHIENI CCM WAENDELEE KULA MPAKA WAPASUKE
January 10, 2011 11:10 PM
Kiduku said... Kwanini CCM wanaogopa maandano kuliko mahakama? Jibu ni rahisi, mahakama zetu sio huru, anayeteua majaji woooote nchini ni mwenyekiti wao wa CCM taifa, hivyo ni sawa na kesi ya nyani kula mahindi kumpelekea ngedere akaamue. Maandamano yanaogopewa na serikali zote kandamizi duniani, maana ni maandamano pekee nyenye nguvu ya kukusanya watu wanyonge ili waende wakakusanyike pahala ili wajulishwe ukweli halisi wa mambo, matukio na ubaya wa watawala na hatua za kuchukua.
Kamwe msikimbilie mahakamani, hamtapata kitu huko, kimbilieni maandamano na mikutano ya hadhara sio mahakamani, ona kesi ya mgombea binafsi ya mch. Mtikila ilivyoamuliwa na mahakama ya juu, ona kesi ya Ditopile, ona kesi ya zombe, ona dowans, ona kesi ya mzee wa vijisenti ya kuua, ona, ona, ona,.........
Ndiyo maana makamba na wenzake hawaishi kusema muende mahakamani ili mkakatwe shigo zenu kwa panga butu ya kijani ya mwenyekiti wao wa CCM.
Maandamano ndiyo mwiba wa madhalimu, andamaneni hadi mfe wote, sio kwenda mahakamani mtavuliwa huko kwa nyavu zenye rangi ya kijani ndiyo maana wanawasakizia mahakamani. Tuchukue uwamuzi mgumu hata ikididi kupoteza maisha ili kuzikomboa njia kuu za demokrasia na utawala wa sheria ili watu tuishi kwa amani na utulivu wa kweli
January 10, 2011 11:35 PM
Anonymous said... Hawa wazee wa Dar siku zote tunawajua, wameshapungukiwa hekima!!! Mawazo yao ni yaleyale ya chama kimoja. Binafsi siwezi kuwashangaaa, ndio hao waliomshangilia Rais wakati anatishia wafanyakazi na kukataa kura zao!!! Sidhani kama leo wanaweza kubadilika na kuwakemea CCM na Serikali yake.
January 11, 2011 12:37 AM
Anonymous said... Basi tugawane nchi tupige kura sehemu ipi ya Tanzania iwe serikali ya kiislamu na sehemu gani serikali ya kikristo. Maana mnakazania udini udini kana kwama ni Mgawo wa umeme. ACHENi UPUZI Ninyi nyote mnaoingiza udini kwenye mijadala ni Wapumbavu kabisa.
January 11, 2011 12:46 AM
Anonymous said... Mtaji wa CCM ni Ujinga na umasisikini, jinsi ujinga unavyopungua na ndio mwisho wao unavyofika, sisi wenye akili hatuwezi kumisikiliza huyo mtulia mpuuzi atakuwa amepewa hela kidogo ili aongee agange njaa
January 11, 2011 1:07 AM
Anonymous said... Jamani sasa watanzania na ukiristo umevuka mpaka.matusi mpaka kwa raisi sasa yanavuka mpaka.ni bora mkawatukana maaskofu wanaoingilia mambo ya siasa badala ya kumtukana raisi.nyie wakiristu mnasema mmesoma kuliko nani?wacheni kujigamba wakati ujui ni chuo gani ambacho wewe umesoma na waislamu atujasoma.huo ni ulimbukeni wa karne tuu.wacheni kujigamba wakati magamba ujaona.
January 11, 2011 1:17 AM
Anonymous said... hakuna mwenye hati miliki ya siasa nchini. wnasiasa wanafiki hawapendi kukosolewa hata siku moja. mbona hao maaskofu wakiwasifia hamuiti kuingilia siasa na dini ; wakiwakosoa mnasema dini kuingilia siasa. what is your principle then? mbona mko selective? makamba akitumia biblia kutetea oppression hamusemi anachanganya dini na siasa. what is your principle then? what is dini what is siasa? zote ni platform za kumhudumia mwananchi; zote zina uhuru wa kutoa maoni kukosoa na kushauri; hakuna mwenye hati miliki zaidi ya mwingine. zote ni social tools kwa ajili ya mwanadamu. dhana ya kutochanganya Siasa na Dini inatumiwa kama silaha ya oppressive leaders kuendeleza kuwakandamiza wengine. Viongozi wadini msikubali kufungwa midomo wala kuwa maspika wa oppressive leaders. kwanza, askofu, mwalimu, polisi, mbunge, mwanachama cha siasa au NGO wote wana haki ya kikatiba kutetea maslahi ya mwananchi - hakuna wa kumtukana mwningine. kiongozi akiwa mfano wa kufuata sheria na utaratibu, hatalaumiwa na yeyote. kama sheria hazifai tuzibadilishe kwa demokrasia ya wazi. asijifanye mtu mmoja alizaliwa na label au hati miliki juu ya wengine!! Maskofu na mashehe endeleeni kukosoa wote wanaoleta ukorofi wa kisiasa na kijamii. yote hayo ni mauovu. mwanasiasa anayeona kukoselewa hakufai ajisafishe tu awe safi morally and ethically; no manipulation hapa. tukatae kucheza huo mpira wa kinafiki sasa. kiongozi mbovu akosolewe bila woga. na anayejiona mzuri asimame ajitetee mwenyewe. mtu asiwe laudspeaker ya mtuhumiwa. ukiwa na tuhuma zinakujia jibu, tena kama unajiona msafi jibu tu lakini weka wazi usafi wako, usitukane wanaokukosoa, wala kutumia mtu mwingine kukujibia.
January 11, 2011 1:39 AM
Anonymous said... WAKRISTO KUWENI MACHO YALITOKEA EGYPTI YATAWAKUTA. SIMLISIKIA WIKI MBILI ZILIZOPITA WAKRISTO ZAIDI YA ISHIRINI WALIUWAWA KANISANI. MAMBO HAYA MABOMU KIUNONI YANAKUJA. SASA WAMESHTUA IRINGA. HILO NI LA MGAMBO LIMESHALIA.
January 11, 2011 2:08 AM
Anonymous said... Namjibu ndugu wa pili juu. Kiongozi wa dini akikosoa taratibu za uchaguzi na maangamzi yalitokea; au ukitoa maoni yake kuhusu mwelekeo unaofaa - hajajiingiza katika siasa. Lakini akisema "hamtambui Meya" basi amejiingiza katika siasa kwa sababu he has taken a political stand. Amechukua msimamo wa kisiasa na hiyo ni kijiingiza katika siasa. Hapo atakuwa open kuhujumiwa kwamba alitumia criteria gani kutomtambua Meya. Ni wazi atakuwa amejitosa katika mgogoro wa siasa kinyume na maadili ya uongozi wa kidini.Narudia: wanahaki ya kusema kwamba chaguzi zifanyike kwa haki na uadilifu. Lakini hawana haki ya kusema fulani kashinda/kashindwa au fulani nina mtambua/simtambui. Their calling (as religious leaders) requires them to steer clear of partisan positions. Wako, Mwendapole
January 11, 2011 3:46 AM
Anonymous said... By the way, Maaskofu pia ni raia wa Tanzania, wanaposhiriki siasa ni kama raia wngine, tena wao wanaona mbele zaidi kuliko akina Makamba.
Makamba anaona leo tu, hajui ya kesho na mtondo. Ndio maana anapofumbua kinywa chake haoni aibu wala hatari ya maneno yake. Hajui hayo maneno yatawaandama watoto wake na wajukuu zake hadi kaburini. Kama ambavyo leo mtu akijitambulisha kuwa yeye ni mjukuu wa Hitler wa ujerumani, wengi watastuka wakisikia ni mjukuu wa Makamba.
Tusiwe wanafiki, CCM ina udini, na wanautumia kuwatishia wengine ili waogope kuitwa wadini. Hakuna mtanzania asiye na dini. Kama si muislam au mkristo atakuwa na imani ya kimila. Ila watu wanapokwepa kusema ukweli ili wasionekane wadini, wanakuwa waongo.
Hawa wanaojiita wazee wa DSM hawajui kuwa CCM wamecheza rafu? Acheni unafiki. Hawa ni wazee wa CCM sio wa DSM.
Viongozi wa serikali wanatakiwa wawatumikie wananchi wote, sio wanaCCM. Haki itendeke kwa watu wote. Hata CCM wangekuwa wanaonewa wangeandamana tu.
January 11, 2011 4:48 AM
*Mbunge kutoka Tanga ashiriki tena uchaguzi
*CHADEMA waususia, wasema hawashiriki uhuni
Na Glory Mhiliwa, Arusha
MBUNGE wa Viti Maalumu mkoa wa Tanga kupitia CCM, Bi. Mary Chatanda jana alizidi kuleta mvutano wa
kisiasa baada ya kushiriki kwenye uchaguzi Jumuia ya Serikali za Mitaa Tanzania (ALAT) mkoa wa Arusha na kusababisha wajumbe wa CHADEMA kuususia.
Hii ni mara pili kwa mbunge huyo kupitia Mkoa wa Tanga kuzua tafrani kama hiyo baada ya kushiriki uchaguzi wa meya na naibu wake katika Manipaa ya Arusha, hatua iliyopingwa na madiwani wa CHADEMA, huku CCM wakisisitiza kuwa ni halali kufanya hivyo.
Kutokana na kitendo cha Bi. Chatanda ambaye pia ni Katibu wa CCM Mkoa wa Arusha, wajumbe wa CHADEMA waliondoka katika mkutano huo wakisema wasingewe kushiriki kuchakachua sheria kwa kuchagua wajumbe wa ALAT, huku akimshirikishwa mjumbe haramu.
Hata hivyo, vigogo wa CCM ambao ni wabunge mkoani Arusha na wajumbe wa kikao hicho, Bw. Edward Lowassa (Monduli), Lekule Laizer (Longido), Bw. Goodluck Ole Medeye (Arumeru Magharibi), Bw. Jeremiah Sumari (Arumeru Mashariki) pamoja na Meya anayelalamikiwa wa Manispaa ya Arusha, Bw. Gaudence Lyimo hawakuhudhuria.
Kikao hicho kiliendeshwa na mwenyekiti wa muda, Bw. Ismail Katamboi, ambaye ni diwani wa Kata ya Kisongo, ambaye alisema kukuwapo kwa wajumbe sita wa CHADEMA siyo sababu ya kuwazuia kuendelea na uchaguzi huo.
Akizungumza na waandishi wa habari nje ya ukumbi, Mbunge wa Arusha Mjini, Bw. Godbles Lema alisema, "Sisi tumetoka ndani ya kikao hiki kwa sababu ya huyu Bi. Mary Chatanda ambaye ni mbunge wa Tanga, iweje leo apige kura za kuchagua wawakilishi wa mkoa Arusha," alisema Lema.
Alisema kuwa kinachofanyika sasa kwa Mkoa wa Arusha ni uhuni na siyo demokrasia, hivyo bora wawaachie wenye chama tawala wafanye kila wanachotaka, ila wao hawako
tayari kushiriki kuchakachua sheria kwa kuchagua wajumbe, huku wakimshirikisha mjumbe haramu.
Kikao hicho kilitakiwa kuchagua, mwakilishi ALAT Taifa, Mwenyekiti na makamu wake mkoa, katibu na Mweka hazina.
Pamoja na Bw. Lema wajumbe wengine wa CHADEMA waliosusa uchaguzi huo ni Bi. Cecilia Paleso, Diwani Viti Maalum- Karatu, Lazaro Maasai, Mwenyekiti Halmashauri ya Karatu, Joyce Mukya, Mbunge Viti maalumu Arusha, Winner Kitembe, Diwani wa Karatu na Mchungaji Israel Natse ambaye ni Mbunge Karatu.
Kikao hicho kilitakiwa kuwa na wajumbe halali 40, lakini baada ya wajumbe sita wa CHADEMA kutoka na wengine ambao hawakuhudhuria, walibaki 28 wa CCM ambao waliendelea, na kumchagua Bw. Godfrey Majola, mwenyekiti wa Halmashauri ya Meru kuwa Mwenyekiti wa ALAT mkoa.
Msuguano huo umeendelea kutoka mkoani Arusha wakati vumbi lililotimka kutokana na polisi kuzima maandamano wa CHADEMA kupinga uchaguzi wa meya likiwa halitatua.
Katika tukio hilo, watu watatu waliripotiwa kuuawa na polisi kwa risasi na wengine zaidi ya 30 kujeruhiwa, na chama hicho kimendaa mazishi ya 'kitaifa' yatakayofanyika katika viwanja vya NMC kesho.
Katika hatua nyingine, Anneth Kagenda anaripoti kuwa Baraza la Wazee wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, limewataka viongozi wa dini kukaa kimya na kutojiingiza kwenye siasa kwa kutoa msimamo kuhusu suala hilo la Arusha kwa madai kuwa kufanya hivyo kunaweza kuleta maafa makubwa nchini.
Hayo yalisemwa jijini Dar es Salaam jana, na Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Bw. Mohamed Mtulia wakati akitoa tamko la kukemea vurugu za Mkoani Arusha zilizotokea Januari 5, 2011.
Alisema kuwa wamesikitishwa na kauli hizo ambazo zinaashiria matakwa ya kidini katika masuala ya kisiasa, kwa kuwa jambo hilo likiachiwa litaitumbukiza nchi katika machafuko ya kidini.
"Sisi wazee tunawaomba maaskofu na viongozi wengine wote wa kidini kuiacha siasa kwa wanasiasa, kwani kitendo cha maaskofu wa Arusha kukataa kumtambua Meya wa Jiji hilo ambaye pia amekataliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinaleta wasiwasi wa kujitokeza viongozi wengine wa kidini na kujipa mamlaka ya kutowatambua viongozi wasiowakubali kama walivyofanya maaskofu hao," alisema Katibu Mtulia.
Alisema kuwa wanaamini kwamba Dkt. Willibrod Slaa aligombea urais katika uchaguzi uliopita wa mwaka 2010 na kama angekuwa 'chaguo la Mungu' basi angekuwa Rais na Amiri Jeshi Mkuu wa nchi, na bila shaka asingeridhia Mwenyekiti au Katibu wa chama chochote cha siasa apinge kwa maneno na vitendo, amri halali za mamlaka za kisheria zilizoundwa kwa mujibu wa katiba na sheria za nchi.
"Pamoja na kusikitishwa na nguvu iliyotumika ni wajibu wetu kuitafakari nguvu hiyo na je, ilikuwa lazima itumike au haikuwa lazima, hivi kikundi cha raia kinachoelekea kituo cha polisi kwa ajili ya kuwatoa watuhumiwa kwa nguvu kimedhamilia nini, na je, jamii inafahamu nguvu waliyonayo raia hao na wanaowaunga mkono?" alihoji Bw. Mtulia.
Aidha alisema kuwa wazee hao wanaamini kuwa endapo uvamizi wa kituo cha polisi ambacho kinawahifadhi watuhumiwa, pamoja na silaha na nyaraka muhimu ungefanikiwa na silaha zikaangukia mikononi mwa raia wa kawaida wasio na nia njema, kungekuwa na uwezekano mkubwa wa kutumika vibaya na kuleta madhara makubwa.
"Ni dhahiri kuwa waliokusudia kuvamia kituo hicho wangefanikiwa na kupora silaha ili zisaidie kuwatoa watuhumiwa, hali ingekuwa mbaya sana na pia kama angalizo la Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) lingefuatwa, yaliyotokea yasingetokea," alisema.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza hilo Bw. Athuman Mwinyimvua alisema kuwa wanatoa pole kwa wale wote walioathiriwa na vurugu zile kwa kupoteza mali huku wengine wakipoteza maisha na wale waliojeruhiwa.
25 Maoni:
Anonymous said... Mohamed Mtulia, acha kuongea upuuzi kama huu wakati raia wasio na hatia wameuawa kwa uroho wa madaraka ya viongozi wa CCM. Unaleta dhana y akufikirika kuwa eti CHADEMA walikwenda kuvamia kituo cha polisi ili wapore silaha? Hayo ni mawazo mgando. Halafu kumbuka wewe huna hadhi ya kuwaelekeza maaskofu na mapadre ni nini cha kufanya. Wewe na mashekh wenzako fanyeni yenu ya Koran misikitini, yanayowahusu wa Biblia waachieni wenyewe. Excuse me!
January 10, 2011 8:34 PM
Anonymous said... RIP nyie wazee njaa. Majina yote yanaja ulikana ni dini gani? Hivi kwa nini hatuna shule za maana au hospital za maana za kiislam? angalia vyuo vikuu vingapi, huduma ngapi zinazotolewa na waislam. Badala ya kujenga shule, hospital mnajenga misikiti tena barabani!!!! Ujinga muda wenu wa kufikiri umekwisha sanda zinawasubiri. Hivi da ndo kuna wazee?? kazi kunywa kahawa basi. Narudia RIP
January 10, 2011 8:39 PM
Anonymous said... hivi hawa niwazee au uchwala msome madarasa hayata wakomboa ukisikia tu jina limeanzia na mzee wa barakashee utajua nipumbu tu zinazo fuata ooo udini hivi hamna hoja wa kristu wangekuwa wadini wangewachagua hawa ndg zenu wanaolipeleke taifa kudidimia kiuchumi mjue kuongoza hamwezi ni jaziba ya udini tu kila kukicha.
January 10, 2011 9:08 PM
Anonymous said... Kwa kweli kwa hili serkali ya sisiemu haiwezi kukwepa lawama.wamaona kabisa kuwa kuna tatizo bado wanaendelea kuruhusu chaguzi za namna hiyo kufanyika,wanataka wao tu ndio wawe madarakani hata kama hawakuwekwa na nguvu ya wananchi.kwani uchaguzi ukirudiwa Arusha kwa uangalizi na kufuata sheria zote za uchaguzi na ikaonekana ccm wameshida chadema haiwezi lalamika.lakini kwa uroho wa madaraka wanapindisha sheria na kuonekana wameshinda,pia hembu liwekeni wazi nani anaestahili kupiga kura ktk kumchagua meya wa jiji???mtu mbaya sana anaeharibu amani nchini ni pamoja na Yusufu Makamba,pia hata jeshi la polisi,huyu mama pia mbunge wa tanga aangaliwe pia,
January 10, 2011 9:38 PM
Anonymous said... Hawa ndio wazee wanaomshauri Rais na kula mapochopocho ya Ikulu. Wanafikiri TZ ni mali yao. Au wanafikiri wangealikwa kwenda kula maharagwe. Kwa taarifa yenu hakuna maharagwe ni majonzi. Huo udini ni nyinyi mnao kama kawaida yenu, na ndio maana nchi zote zenye waislam ni matatizo matutpu. Kama sio kuwasaidia kwenye Elimu sijui mngefa je. Mnachukua kuvuli cha udini muanze kufunga mabomu kiunoni na kutumia makwanja yenu yaliyoko humo msikitini.
January 10, 2011 9:49 PM
Anonymous said... Chadema (Chama Cha Demokrasia na Maandamano) Nyie ndio wa kulaumiwa kwa nini hamkutii amri halali ya kutokuandamana iliyotolewa na IGP>. Nyie ndio mmesababisha mambo yote haya. Namsihi Hakimu awafunge wote walioshutakiwa kwa kutotii sheria miaka 10 kila Mmoja nyie ndio mlisababisha watu wakauawa kama mngeenda tu kwenye mkutano kistaarabu yote hayao yasingetokea lakaini mkaandamana kinyime cha sheria mnataka mfnaye mambo yenu manavyotaka nyinyi ili jumuia ya kimataifa iwaone CCm wabaya nyie ndio wabaya. Haya na hao maaskofu nduguze Slaa hawamtambui Meyawa Arusha ni maajabu wao ni kina nanai au walitaka Slaa awe rais ili nchi iwe ya kikirito hatukubali siye waislamu
January 10, 2011 9:49 PM
pETRO eUSEBIUS mSELEWA said... Chatandaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaeeeeeeeeeeeeeeee! Ondooooooooooooooooooookaaaaaaaa kwa jina la Yesu!
January 10, 2011 9:50 PM
Anonymous said... Huyo mama Chatanda damu iliomwagika imwangukie yeye,na akatubu makosa hayo vinginevyo dhamira itamshtaki,
January 10, 2011 9:59 PM
Anonymous said... Chatanda kaombe radhi watakunyang'anya ukristo wako. Kumbuka yaliowafika wakristo wa sumbawanga walioikataa Chadema Kanisa limewafanya nini? Umemsikia Malecela alivyokuita mtovu wa nidhamu.
Hivi kwa nini chama cha CHADEMA kisifutwe kwa kuubeba udini. Kwa nini Mbowe na Padre Slaa wasijiuzulu kwa kushindwa kuwachunga kondoo zao na kuwasabibishia maafa ambayo yanaepukika.
Balaa la umasikini la Nchi hii limeletwa na Nyerere. Tuwe w Kweli. Ilifikia watu wanakwenda uchi, wakalazimishwa kula sembe la Yanga, wakakosa hata sabuni ya kuogea na dawa ya meno,tukawa tutanunua chakula kwa kadi na kiwango alichoweka yeye.Maovu matupu. Watu kuwekwa ndani bila ya kufikishwa mahakamani. Ubabe mtupu. Lakini hatawasikia Maaskofu kulaani au kukosoa utawala huwo. Ni Unafiki wa kikatoliki na Udini tu ndio uliotawala nchi hii hivi sasa, Nayote kwa sababu CHADEMA chama cha Maaskofu kimeshindwa uchaguzi na kitaendelea kushindwa maisha. Kwa vile dhamira zao zinajuulikana sasa na kila mpenda amani
January 10, 2011 10:18 PM
Anonymous said... Nimependa maoni yoote leo ah. Ntalala kwa raha sana.
January 10, 2011 10:20 PM
Anonymous said... sasa nimeelewa kwa nini tunaambiwa viongozi wa dini wasijiingize kwenye siasa. Wakitaka wavue majoho waingie kwenye ulingo.
Matoeo ni haya hapa.soma wachangiaji.Mgogoro wa Chadema na CCM umekiwa matusi baina ya wakristo na waislamu. Vitone vya matusi aina hii vinaweza kuleta mfarakano usiotegemewa kwenye jamii.
Na hili limekuja baada ya viongozi wa dini kuanza kuleta chokochoko au kuegemea upande mmoja.
hatari mti na macho
January 10, 2011 10:25 PM
Anonymous said... Hili limekuja baada ya CCM kutaka kwa nguvu kutawala bila kufuata kanuni. Ntu yeyote anao uhuru wa kuhimiza amani; na zaidi sana viongozi wa dini. Maoni ya kuleta amani yasichukuliwe kama maoni ya udini. Udini sasa unaletwa na Chatanda na mashekh wanaojibu maaskofu kana kwamba hawapaswi kukemea maovu ili kudumisha amani nchini. Tunapotoa maoni tufikirie kwa kichwa si kwa tumbo!
January 10, 2011 10:36 PM
Anonymous said... HIVI NYIE WAFUASI WA CHADEMA MMEKUWA WEHU? WENGINE WAKITOA MAONI MNAWATUKANA NA KUWAKEBEHI LAKINI MAASKOFU WAKISEMA SAWA,HUO NI UJINGA WA KUPINDUKIA,KAMA MAASKOFU WAKISEMA NI HAKI YAO KUTOA MAONI,KAMA WAISLAMU WA MKOA WA ARUSHA WALISEMA NI HAKI YAO YA KUTOA MAONI NA KAMA HAO WAZEE WA DAR-ES-SALAAM WALISEMA PIA NI HAKI YAO YA KUTOA MAONI,LEO KUNA GAZETI LINASEMA MWANZA KIKUNDI FULANI CHA WATU WANATAKA KIKWETE AJIUZULU NAO NI HAKI YAO KUTOA MAONI,NYIE MKISHA ONA JINA LA KIISLAMU TU TAYARI VICHAA VINAWAPANDA. KOMENI WAACHIENI WENYE MAONI YAO WATOE.
January 10, 2011 10:38 PM
Anonymous said... Wewe mbunge wa Arusha unaoongoza kihuni hapo,waeleze watu sheria za nchi zinasemaje kuhusu diwani wa kuteuliwa kutoka katika vyama na haki zake sio kila siku kuleta migongano isiyo na tija kwa jiji letu la Arusha. weka sheria wazi inasemaje? kutuambia tu huyu ni mtu wa Tanga wakati ni katibu wa CCM wa Arusha na anaishi Arusha haitoshi,wewe kwenu ni Moshi na sio Arusha basi nenda kwenu Moshi.
January 10, 2011 10:45 PM
Anonymous said... Mary Chatanda ni muislamu? Acha ujuha wewe, watu wanaotoa maoni yao, nao piani haki yao kufanya hivyo. Upo hapo!
January 10, 2011 10:59 PM
Anonymous said... MNALOLILETEA MZAHA LEO KWA KUANDIKA UTUMBO KWA KUTAKA MJIFURAHISHE, KESHO LITAWALIZA. NA MTALIA NYOTE BILA KUJALI KUWA WANA CCM AU CHADEMA. NG'ANG'ANIENI TU MADARAKA DAWA YA WOTE SASA IKOJIKONI. NA TUKANENI SANA WACHUNGAJI TENA KWANGUVU ZOTE, CHAMOTO KITAKUJA IKIWA TU NIDHAMU YA NNCHI HAITARUDISHWA NA VIONGOZI WA CCM WENYE UROHO WA MADARAKA. NANYI CHADEMA ACHENI MAMBO HAYA YA KUPIGANIA UKOMBOZI WA MTANZANIA, KWANI KWASASA SI WAKATI WAKE, MTAJICHOSHA BURE NA HAKUNA LITAKALOSAIDIA, MWAJUA FIKA KUWA SERIKALI YA TZ IMOMIKONONI MWA KIKWETE NA AMEMILIKI HATA JESHI LA POLISI NA KWAO SASA KUUWA WATANZANIA WA FUASI WA VYAMA VYA UPINZANI NI KUTAKA WAPANDISHWE VYEO KILA MTU ANAJUA KWA SERA SASA YA CCM NI KUUWA WATANZANIA WASIO WAFUASI WA CCM. CHADEMA TULIENI WAACHIENI CCM WAENDELEE KULA MPAKA WAPASUKE
January 10, 2011 11:10 PM
Kiduku said... Kwanini CCM wanaogopa maandano kuliko mahakama? Jibu ni rahisi, mahakama zetu sio huru, anayeteua majaji woooote nchini ni mwenyekiti wao wa CCM taifa, hivyo ni sawa na kesi ya nyani kula mahindi kumpelekea ngedere akaamue. Maandamano yanaogopewa na serikali zote kandamizi duniani, maana ni maandamano pekee nyenye nguvu ya kukusanya watu wanyonge ili waende wakakusanyike pahala ili wajulishwe ukweli halisi wa mambo, matukio na ubaya wa watawala na hatua za kuchukua.
Kamwe msikimbilie mahakamani, hamtapata kitu huko, kimbilieni maandamano na mikutano ya hadhara sio mahakamani, ona kesi ya mgombea binafsi ya mch. Mtikila ilivyoamuliwa na mahakama ya juu, ona kesi ya Ditopile, ona kesi ya zombe, ona dowans, ona kesi ya mzee wa vijisenti ya kuua, ona, ona, ona,.........
Ndiyo maana makamba na wenzake hawaishi kusema muende mahakamani ili mkakatwe shigo zenu kwa panga butu ya kijani ya mwenyekiti wao wa CCM.
Maandamano ndiyo mwiba wa madhalimu, andamaneni hadi mfe wote, sio kwenda mahakamani mtavuliwa huko kwa nyavu zenye rangi ya kijani ndiyo maana wanawasakizia mahakamani. Tuchukue uwamuzi mgumu hata ikididi kupoteza maisha ili kuzikomboa njia kuu za demokrasia na utawala wa sheria ili watu tuishi kwa amani na utulivu wa kweli
January 10, 2011 11:35 PM
Anonymous said... Hawa wazee wa Dar siku zote tunawajua, wameshapungukiwa hekima!!! Mawazo yao ni yaleyale ya chama kimoja. Binafsi siwezi kuwashangaaa, ndio hao waliomshangilia Rais wakati anatishia wafanyakazi na kukataa kura zao!!! Sidhani kama leo wanaweza kubadilika na kuwakemea CCM na Serikali yake.
January 11, 2011 12:37 AM
Anonymous said... Basi tugawane nchi tupige kura sehemu ipi ya Tanzania iwe serikali ya kiislamu na sehemu gani serikali ya kikristo. Maana mnakazania udini udini kana kwama ni Mgawo wa umeme. ACHENi UPUZI Ninyi nyote mnaoingiza udini kwenye mijadala ni Wapumbavu kabisa.
January 11, 2011 12:46 AM
Anonymous said... Mtaji wa CCM ni Ujinga na umasisikini, jinsi ujinga unavyopungua na ndio mwisho wao unavyofika, sisi wenye akili hatuwezi kumisikiliza huyo mtulia mpuuzi atakuwa amepewa hela kidogo ili aongee agange njaa
January 11, 2011 1:07 AM
Anonymous said... Jamani sasa watanzania na ukiristo umevuka mpaka.matusi mpaka kwa raisi sasa yanavuka mpaka.ni bora mkawatukana maaskofu wanaoingilia mambo ya siasa badala ya kumtukana raisi.nyie wakiristu mnasema mmesoma kuliko nani?wacheni kujigamba wakati ujui ni chuo gani ambacho wewe umesoma na waislamu atujasoma.huo ni ulimbukeni wa karne tuu.wacheni kujigamba wakati magamba ujaona.
January 11, 2011 1:17 AM
Anonymous said... hakuna mwenye hati miliki ya siasa nchini. wnasiasa wanafiki hawapendi kukosolewa hata siku moja. mbona hao maaskofu wakiwasifia hamuiti kuingilia siasa na dini ; wakiwakosoa mnasema dini kuingilia siasa. what is your principle then? mbona mko selective? makamba akitumia biblia kutetea oppression hamusemi anachanganya dini na siasa. what is your principle then? what is dini what is siasa? zote ni platform za kumhudumia mwananchi; zote zina uhuru wa kutoa maoni kukosoa na kushauri; hakuna mwenye hati miliki zaidi ya mwingine. zote ni social tools kwa ajili ya mwanadamu. dhana ya kutochanganya Siasa na Dini inatumiwa kama silaha ya oppressive leaders kuendeleza kuwakandamiza wengine. Viongozi wadini msikubali kufungwa midomo wala kuwa maspika wa oppressive leaders. kwanza, askofu, mwalimu, polisi, mbunge, mwanachama cha siasa au NGO wote wana haki ya kikatiba kutetea maslahi ya mwananchi - hakuna wa kumtukana mwningine. kiongozi akiwa mfano wa kufuata sheria na utaratibu, hatalaumiwa na yeyote. kama sheria hazifai tuzibadilishe kwa demokrasia ya wazi. asijifanye mtu mmoja alizaliwa na label au hati miliki juu ya wengine!! Maskofu na mashehe endeleeni kukosoa wote wanaoleta ukorofi wa kisiasa na kijamii. yote hayo ni mauovu. mwanasiasa anayeona kukoselewa hakufai ajisafishe tu awe safi morally and ethically; no manipulation hapa. tukatae kucheza huo mpira wa kinafiki sasa. kiongozi mbovu akosolewe bila woga. na anayejiona mzuri asimame ajitetee mwenyewe. mtu asiwe laudspeaker ya mtuhumiwa. ukiwa na tuhuma zinakujia jibu, tena kama unajiona msafi jibu tu lakini weka wazi usafi wako, usitukane wanaokukosoa, wala kutumia mtu mwingine kukujibia.
January 11, 2011 1:39 AM
Anonymous said... WAKRISTO KUWENI MACHO YALITOKEA EGYPTI YATAWAKUTA. SIMLISIKIA WIKI MBILI ZILIZOPITA WAKRISTO ZAIDI YA ISHIRINI WALIUWAWA KANISANI. MAMBO HAYA MABOMU KIUNONI YANAKUJA. SASA WAMESHTUA IRINGA. HILO NI LA MGAMBO LIMESHALIA.
January 11, 2011 2:08 AM
Anonymous said... Namjibu ndugu wa pili juu. Kiongozi wa dini akikosoa taratibu za uchaguzi na maangamzi yalitokea; au ukitoa maoni yake kuhusu mwelekeo unaofaa - hajajiingiza katika siasa. Lakini akisema "hamtambui Meya" basi amejiingiza katika siasa kwa sababu he has taken a political stand. Amechukua msimamo wa kisiasa na hiyo ni kijiingiza katika siasa. Hapo atakuwa open kuhujumiwa kwamba alitumia criteria gani kutomtambua Meya. Ni wazi atakuwa amejitosa katika mgogoro wa siasa kinyume na maadili ya uongozi wa kidini.Narudia: wanahaki ya kusema kwamba chaguzi zifanyike kwa haki na uadilifu. Lakini hawana haki ya kusema fulani kashinda/kashindwa au fulani nina mtambua/simtambui. Their calling (as religious leaders) requires them to steer clear of partisan positions. Wako, Mwendapole
January 11, 2011 3:46 AM
Anonymous said... By the way, Maaskofu pia ni raia wa Tanzania, wanaposhiriki siasa ni kama raia wngine, tena wao wanaona mbele zaidi kuliko akina Makamba.
Makamba anaona leo tu, hajui ya kesho na mtondo. Ndio maana anapofumbua kinywa chake haoni aibu wala hatari ya maneno yake. Hajui hayo maneno yatawaandama watoto wake na wajukuu zake hadi kaburini. Kama ambavyo leo mtu akijitambulisha kuwa yeye ni mjukuu wa Hitler wa ujerumani, wengi watastuka wakisikia ni mjukuu wa Makamba.
Tusiwe wanafiki, CCM ina udini, na wanautumia kuwatishia wengine ili waogope kuitwa wadini. Hakuna mtanzania asiye na dini. Kama si muislam au mkristo atakuwa na imani ya kimila. Ila watu wanapokwepa kusema ukweli ili wasionekane wadini, wanakuwa waongo.
Hawa wanaojiita wazee wa DSM hawajui kuwa CCM wamecheza rafu? Acheni unafiki. Hawa ni wazee wa CCM sio wa DSM.
Viongozi wa serikali wanatakiwa wawatumikie wananchi wote, sio wanaCCM. Haki itendeke kwa watu wote. Hata CCM wangekuwa wanaonewa wangeandamana tu.
January 11, 2011 4:48 AM