Red Giant
JF-Expert Member
- Mar 9, 2012
- 15,650
- 20,997
hapo zamani za kale palikuwa na mti mmoja mkubwa sana ili kuukumbatia unahitaji watu watano warefu! sasa mti huo ukatokeza matawi na tawi moja likawa kubwa sana ukubwa wake ukiwa nusu ya ya mti wenyewe. sasa tawi hilo likawa linatoa maua ambayo nayo yanatoa matunda, matunda hayo yakidondoka yanaanza kuchipusha miti mingine, pia tawi hilo lilikuwa limebeba matawi mengine mengi na makubwa. siku zilivyoenda tawi hilo likaanza kuwa na majivuno na kuanza kujifananisha na mti uliolibeba maana halikuona tofauti maana wote wana matawi, wote wantoa maua na wote wanatoa matunda. baada ya kibiri kuzidi mti ukaamua kulikatia maji na virutubisho toka udongoni! maskini tawi lenye kiburi likafa kwa majivuno yake.
meaning: binadamu tunapokuwa na hela, umaarufu na kufanikiwa sana maishani tunaanza kusahau mungu wetu kama tawi lililoanza kudharau mti
meaning: binadamu tunapokuwa na hela, umaarufu na kufanikiwa sana maishani tunaanza kusahau mungu wetu kama tawi lililoanza kudharau mti