Ngoja niropoke

Ngoja niropoke

Huwezi mbadilsha mwanamke msomi mwenye misimamo yake akubaliane na mambo ya kiboya(according to wao).
Solution ni muache kuwaoa...
mnalalamika as if mmelazimishwa kuwaoa...there are so many good girls wasiosoma sijui kwanini hamtaki kuwaoa.
Hao wasomi hawatabadilika na miaka inavyoenda itakuwa worse zaidi.
Acheni kiherehere bwana. Mnalalamika sana Mshana tatizo nini?

IMG_0669.jpg


dada yangu kaa kimya tu.

yanaanza yakiwa na ndoto ndefu,lakini kumbe ndani ni bua lenye wadudu,haukui muhindi.

tunafanya haya kushauri,maana ndoa ni hitaji la watu wote sio wasiosoma peke yao.
utakwenda shule,utapata pesa,utapata cheo na umaarufu,ukikosa ndoa au mahusiano rasmi lazima utajiona wewe ni kenge tu
 
Takwimu zinaonesha Wakala wa usajili, ufilisi na udhamini (RITA), kwa mwaka unapokea maombi ya talaka yasiyopungua 500+ Tanzania nzima.

Kilichonishangaza ni kwamba asilimia 78% ya Ndoa zinazovunjika ni wanawake ndio wanaoomba talaka na kupeleka maombi hayo.

Kilichonishangaza na Kunimaliza zaidi ni kwamba asilimia 89% ya wanawake wanaoomba talaka ni WANAWAKE WASOMI (Intellectual Women)

Swali; Wanawake wasomi wana SHIDA GANI, kwanini kwao talaka ziwe nyingi, kwanini wengi wanasumbuka na mahusiano na kwanini wengi ni single mothers?

Honestly kuna kitu hakiko sawa kwa hawa Intellectual women, kwa takwimu hizi tunaweza kusema elimu zimewaharibu badala ya kuwatengeneza wawe wake bora.

Ndio, haiwezekani asilimia 89% ya maombi ya talaka yakaliwe na wao pekeao, ina maana elimu zao zinawaambia kwamba solution pekee ni talaka, nawaza sana yani

Ngoja niropoke; wanawake wengi wasomi wana kakiburi ka maarifa kanaitwa "INTELLECTUAL ARROGANCE"

Haka kakiburi kanawaambia hivi "wewe ni msomi, una akili, unajiweza na mwanaume hatakiwi kukusumbua kwa lolote lile"

Haka kakiburi kamewafanya wengi washindwe kuwa wanyenyekevu kwa sababu wanajiona ni classy and high, inafika hatua wanaanza kuvimba.

Wengi walifanikiwa sana kielimu kiasi cha kupata fedha, vyeo na status katika jamii vichwa vikaelemewa sifa na kujiona wanajua na kuweza kila kitu.

Pengine ofisini kwao yeye ndo Managing Director na ana watu wengi wakiume wako chini yake kikazi, anataka na mumewe awe chini yake pia.

Elimu yake, cheo na fedha vinamwambia "Unastahili kunyenyekewa na sio kunyenyekea na unaweza kila kitu" wengi hapa ndipo wanapofeli sasa na kuleta mabalaa.

Pengine walipokuwa wanasoma waliambiwa maneno kama "Soma sana, tafuta fedha zako ili mwanaume asikusumbue kwa lolote lile" (hii ndo shida kubwa)

Kwahiyo wengi kuanzia hapo wakawa wanatembea na competetive mentality (fikra za kishindani) na muda wote wapo kinyume na jinsia ya kiume.

Kinachotokea, wakiolewa wanafanya mambo kama washindani (competetors) kwa wanaume wao na sio wapambanaji wenza (teammates)

Kitu kingine kinachowaharibu ni hizi FEMINISTS MOVEMENTS (harakazi zinazodaiwa kumpa nguvu mwanamke na kumkomboa kifikra)

Ukizifuatilia vizuri hizi harakati zinawafanya wanawake wahisi kwamba hata wao wanaweza kuwa kama wanaume since they can pay bills na ada za watoto.

Sikatai, ni kweli kabisa kuna majukumu mwanamke anaweza kuyaperform kama mwanaume lakini haitatokea hata siku moja akawa kichwa cha familia.

Elimu walizopata wengi wao zimewasababishia kakitu kanaitwa "Control Freak Disorder" (unajua ni kanini haka, soma hapa chini)

Ni kale ka akili ka kumtaka mwanamke amcontrol mwanaume na kumfanya mwanaume aenende vile mwanamke anataka (amuweke chini)

Na hii inatokana na ukweli kwamba wengi wameweza kuongoza kakundi ka watu, wengi wameweza kufanya vitu vikubwa katika academic fields zao.

Kitendo cha kufanikiwa kuongoza kakundi ka watu kinawafanya hata kwenye ndoa nafasi ya kuongoza ambayo ni ya mwanaume aitake mwanamke, yaani yeye ndo awe kichwa.

Msuguano unaanzia hapo, mwanaume yeyote yule anataka yeye ndo awe top, ikitokea mwanamke akataka kumshusha mwanaume ili mwanamke awe top balaa linaanza.

Fuatilia, wanawake ninaowazungumzia hapa wengi wana kakiburi, wanajiona, na wanaamini kwamba hakuna kitu wanahitaji kutoka kwa wanaume na wanaweza kila kitu pekeao.

Wanaume wengi wanatafuta fedha ili wahudumie familia zao na kuwatimizia mahitaji, ila kwa wanawake mambo yako kinyume kabisa!

Wengi wanasoma na wanatafuta fedha ili waweze kuthibitisha kwamba wanaweza kufanya kama wanaume, wanaweza kuishi bila wanaume na hawawezi kusumbuliwa kwa lolote.

Ndio maana, kukiibuka kaugomvi kadogo wengi solution inakuwa ni kuachana ili kuthibitisha kwamba "NINAWEZA KUISHI MWENYEWE NA KAMA NI MTOTO/WATOTO NITALEA COZ NINA FEDHA"

Dear ladies, black brother wenu nawakubali kinoma na nafurahi kuwaona vile mnastrugle kupambania ndoto zenu (hongereni kwa hilo)

Lakini, jitahidi kadri uwezavyo fedha zako, elimu yako na cheo ulichonacho/utakachopata visikutie Kiburi mbele ya mumeo uliyenae/utakaekuwa nae.

Ni kweli umefanikiwa kielimu, pengine una mshahara mkubwa, au biashara zako zinaenda safi, una cheo/position fulani somewhere lakini WEWE BADO NI MWANAMKE.

Wakati wowote uwapo mke, mpe nafasi mwanaume awe mume, awe baba, awe kuongozi, awe dereva wa familia huku wewe ukiwa kwake msaidizi.

Hata kama ofisini kwenu una wanaume wengi unaowaongoza na wananyenyekea mbele yako usitake na mumeo akunyenyekee..

Mpe yeye nafasi ya kuwa king, mtii, msikilize na panapohitajika ushauri mpe ushauri kwa upole huku ukionesha kwamba unamuheshimu na kuamini..

Kwanini wanawake wa sahivi wamesoma lakini hawadumu kwenye ndoa kama mama na bibi zetu walioishia darasa la nne/la saba.

Kadri mwanamke anavyoanda juu kielimu, kuna namna anapoteza WIFE TRAITS umakini unahitajika sana ndo mana wengi wanabaki single/single mothers.

Fuatilia wanawake woote unaowajua Tanzania ambao wana vyeo vikubwa, wamefanikiwa kibiashara au wapo top kwenye eneo lolote lile.

Wengi utagundua kwamba hawajawahi kuolewa, waliolewa wakaachika, walizalishwa na wakabaki hapo.

Elimu sio mbaya, fedha sio mbaya..lakini inakuwa mbaya pale inapoanza kumfanya Quuen atake kuwa king, haiwezekani!

[Nimemaliza kuropoka

Credit: WhatsApp forwarded msg
Author: Unknown
Mwanamke msomi hayuko tayari kutumikishwa kwa mujibu wa Mila za mfumo dume zinazokumbatiwa na Wanaume wa Kiafrika..

Huu ndio ukweli mchungu ikizingatiwa kwamba wao sio tegemezi kama wale wasioenda shule so wanaume ndio wa kubadili Mtizamo..
 
Tuongee ukweli tu.
Mwanamke akipata mchumba msomi ukoo mzima utajua, masifa kibao...mwisho wa siku ndo hivi mnashindwa kuishi nao.
.
.
Na wewe ukipata mtoto wa kike mpeleke shule mwisho form four, mnawasomesha hadi chuo degree mbili utegemee aje aishi na mume kwa kunyenyekea kama mtumwa? Hata wewe baba yake hutakubali awe boya.

Ndoa za kiafrika ni utumwa kwa mwanamke kwasababu ya mfumo dume.
Kwenye ndoa kuna uboya mwingi na mnategemea mke ndo auvumilie. Sio kwa zama hizi kaka yangu..
Ingawa kwa bahati nzuri wapo wasichana wanyenyekevu lakini hamuwataki.

Pambaneni tu na hali zenu kwa kweli. Mambo ni bam bam!
Pambaneni tu na hali zenu kwa kweli. Mambo ni bam bam!
 
Wanataka wasomi sababu Wanataka kusaidiwa majukumu, lakini Sasa kukubaliana na yaliyomo chini ya kapeti ndipo shughuli ilipo.

si bora hata hayo majukumu wasaidike sasa.


mwanamke ananunua magauni na viati vya laki nane nane kila wakati hakuna cha maana anachofanya.

unajiuliza huyu na yule wa kukaa tu ndani bora yupi!!!!
 
Mi mwenyewe hapo pa 'ishini nao kwa akili' sielewagi,maana unakuta mke wa mtu anagawa kinoma hadi anafumaniwa,ila mumewe hamuachi,ndo hizo akili?
Hapo mwanaume hana akili
 
View attachment 2364050

dada yangu kaa kimya tu.

yanaanza yakiwa na ndoto ndefu,lakini kumbe ndani ni bua lenye wadudu,haukui muhindi.

tunafanya haya kushauri,maana ndoa ni hitaji la watu wote sio wasiosoma peke yao.
utakwenda shule,utapata pesa,utapata cheo na umaarufu,ukikosa ndoa au mahusiano rasmi lazima utajiona wewe ni kenge tu
Mimi sikatai mtu kuoa anayemtaka awe amesoma au hajasoma. Tatizo ni wao kuoa wasomi halafu wategemee mke abehave kama asiyesoma kama bibi zao.

Elimu inakuja na mambo yake tukubali hilo. Na ukipenda mwenyewe kuoa msomi basi usilalamike pambana na hali yako ni Chaguo lako maana walikuwepo wasio soma na ni wife material lkn hukuwataka.
 
Inawezekana sana tu, nina Rafiki zangu zaidi ya 6 waliwaachisha Ke zao kazi wanaishi vizuri tu na hadi sasa wameshawini sana kiuchumi wakiwa na Watoto wao.

NB:

MAISHA HAYANA KANUNI ILA YANAHITAJI NIDHAMU SANA.
Kuachishwa kazi na Mme nacho kipaji, wanaume wenyewe nyie hawa hawa, kumbuka naye kazaliwa ana ndugu pia, sio unamwachisha kisha manyanyaso yanaanza.
 
Kaka mkubwa mliambiwa ishini nao kwa akili, tatizo wenye elimu ya kawaida wanaume huwa wanawadharau wanataka wale wanao ongea nao kidhungu sasa pambaneni na hali zenu
Nashukuru sana Mungu nilicheza kama Pele kumuoa Ke aina ya Ulweso, sasa hivi nafurahia amani ya roho ktk ndoa kwa zaidi ya miaka mitano
 
Na wenyewe watalipuuza kuendekeza ubabe wao. Na wamesahau kwamba huyu mke anayelalamikiwa leo ndio huyu anayewalea watoto wao wa kike.

Imagine huyu mtoto wa kike mwenye miaka 6 sasa hivi abahatike kusoma kufikia degree ya pili miaka 20 ijayo.
Aje kuolewa na mwanaume mwenye mentality ya kiafrika asiyetaka kubadilika kama ndugu yangu Mshana Jr .
Balaa lake si la kitoto.
mwanaume mwenye mentality ya kiafrika asiyetaka kubadilika kama ndugu yangu Mshana Jr .
Balaa lake si la kitoto. hiki kijembe nimekielewa sana..
 
Back
Top Bottom