Ngeleja alilidanganya bunge

mbasajohn

JF-Expert Member
Mar 14, 2009
247
39
Nakumbuka waziri wa nishati na madin Mh. William Ngeleja siku alipokuwa akiwasilisha bajeti yake kwa mara ya pili alitamka kuwa "unafuu wa umeme unao onekana kwa sasa nchini unatokana na kuanza kwa kutekelezwa kwa mpango wa dharula hasa kuongezeka kwa uzalishaji wa Agreco kutoka MGw 20 mpaka 100".

Lakini cha kushangaza siku mbili tu baada ya kupitishwa kwa bajeti hiyo mgao umeongezeka kasi na kuwa maradufu sehemu nyingi hapa Tanzania, mfano Sikonge Wilaya mojawapo ya mkoa wa Tabora mgao kwa sasa ni usiku kwa usiku yaani wanakata saa moja asubuhi na kurudisha saa tano usiku kila siku toka bajeti hii ipitishwe, kabla ya hapo mgao ulikuwa kwa either kuanzia saa 3 asubuhi na kurudisha saa 10 jioni au wanakata saa 10 jioni na kurudisha saa 5 usiku.

Hali hii imejitokeza kwa jiji la Mwanza ambapo umeme umekatika kwa siku tatu mfululizo baada ya bajeti ya ngeleja kupata baraka za mjengoni. Sasa kwa hali hii Ngereja anaposema kuna unafuu anamaanisha unafuu upi ikiwa hali inazidi kuwa mbaya kama si kuwadanganya waheshimiwa ili wapitishe bajeti yake? au siku hizi mawaziri kusema uongo ndio sahihi badala ya kusema ukweli. Kama kuna sehemu unafuu umeanza kupatikana naomba tujuzane ili tuamini maneno ya Ngereja.
Naomba kuwasilisha.
 
Mbona ndiyo staili yao? Umesahau hata waziri mkuu alilidanganya bunge?
 
Arusha umeme ni sawa na kuwa haupo kabisa!! Umeme gani unarudi saa 8 usiku, unakatika saa kumi usiku huo huo! Nchi ilishawashinda hii. Uungwana nao umewashinda, si bora wangekuwa waungwana wakajiweka pembeni.
 
Jamani hakuna unafuu hata kidogo. Naishi Tabata DSM, huwezi amini mara baada ya bajeti ya Ngereja kupita tulianza kupata mgao mkali sana daily! Alidanganya Bunge na Watz ili bajeti yake ipitishwe!


Wanatufanya sisi matoy wao wa kuburuzwa na kurushwarushwa kama watakavyo wao! Viongozi wetu wamekuwa wahuni,waongo,wezi na wanaojipenda wenyewe kuliko wananchi waliowapa mamlaka ya kutawala.
 
Ngeleja kasema mgao utaisha mitambo yote ya dharura ikishafungwa, December. Msifikiri TV mnatazama peke'enu.
 
Ngeleja kasema mgao utaisha mitambo yote ya dharura ikishafungwa, December. Msifikiri TV mnatazama peke'enu.

Jamani kabla hujajibu hoja soma maelezo swala hapa sio kuisha kwa mgao ila ni kusema mgao umepungua wakati ndo kwanza unaongezeka kasi mara dufu.
 
Nduka sijui unatumia utumbo kufikili au nn, swala n kwamba tulitarajia baada ya budget hali iendelee kwa kpnd fulan kama ilivyokuwa baada ya budget na ije improve kadiri siku zinavyokwenda, sasa imekuwa kinyume chake ndo maana tunasema kuna mchezo mchafu wananchi na wabunge tumechezewa hapa na watu kama wewe ndo wanasababsha Tz ifikie mahali hapa
 
HAPA SOWETO ndiyo basi tena unakuja saa 7 mchana na kukatwa saa 12 Jioni hii ndiyo serikali yetu ila kipindi cha nane nane tulisahau habari za mgawo sijui ule umeme ulitoka wapi ?
 
Tatizo hili ni nafasi kwa Wataalamu wetu wa kizalendo kutafuta tiba mbadala ya umeme....Co tunalalamika 2 kila kukicha.Malalamiko ye2 hayawezi kupunguza makali ya umeme...Hebu tujiulize sisi Watanzagiza wengine tunaolalamika sana tumefanya juhudi gani juu ya suala hilo?Au tuonekane tunajua kuongea? Na wataalamu wa masuala ya umeme waliokopeshwa elimu vyuoni wapo wapi?Kama wapo watusaidie kulitatua tatizo,ni kweli mvua zimezingua lakini tuna vyanzo mbadala vingi vya umeme.Mfano:UPEPO,JUAKALI SANA,MAKAA YA MAWE n.k..
 
Kama umetumwa kawaambie nimewakuta wapo. Kazi yako ni kufrustrate mada zinazoanzishwa. Sio lazima uandike kama huna comment.
 
Nakumbuka waziri wa nishati na madin Mh. William Ngeleja siku alipokuwa akiwasilisha bajeti yake kwa mara ya pili alitamka kuwa "unafuu wa umeme unao onekana kwa sasa nchini unatokana na kuanza kwa kutekelezwa kwa mpango wa dharula hasa kuongezeka kwa uzalishaji wa Agreco kutoka MGw 20 mpaka 100". Lakini cha kushangaza siku mbili tu baada ya kupitishwa kwa bajeti hiyo mgao umeongezeka kasi na kuwa maradufu sehemu nyingi hapa Tanzania, mfano Sikonge Wilaya mojawapo ya mkoa wa Tabora mgao kwa sasa ni usiku kwa usiku yaani wanakata saa moja asubuhi na kurudisha saa tano usiku kila siku toka bajeti hii ipitishwe, kabla ya hapo mgao ulikuwa kwa either kuanzia saa 3 asubuhi na kurudisha saa 10 jioni au wanakata saa 10 jioni na kurudisha saa 5 usiku. Hali hii imejitokeza kwa jiji la Mwanza ambapo umeme umekatika kwa siku tatu mfululizo baada ya bajeti ya ngeleja kupata baraka za mjengoni. Sasa kwa hali hii Ngereja anaposema kuna unafuu anamaanisha unafuu upi ikiwa hali inazidi kuwa mbaya kama si kuwadanganya waheshimiwa ili wapitishe bajeti yake? au siku hizi mawaziri kusema uongo ndio sahihi badala ya kusema ukweli. kama kuna sehemu unafuu umeanza kupatikana naomba tujuzane ili tuamini maneno ya Ngereja.
Naomba kuwasilisha.

Naunga nawe katika hoja yako kabisa 100%,

Ntawakumbusha kidogo pale wabunge walipo tia ngumu kutopitisha budget ya Ngeleja na serikali immediately ikapunguza makali ya mgao wa umeme moja kuhofia watu kuandamana pili ili kuwazuga wananchi ili budget ipite tatu hii hali ya mgao wa umeme still ni kizungu mkuti kwani hapa kuna mradi wa mtu unakikingiwa kifua ili tu malengo yao yafikiwe kwanini nasema hayo wataka kuniambia wakati bwawa la mtela linajengwa halikuwa na Preventive Maintenance option kwenye proposal ya hiyo project kweli ??wakati walijua bwawa litakuwa linaingiwa na uchafu matope na kupatwa kwa kutu na marekebisho machache me siwezi amini kuwa haiwezekani kushindwa kupunguza tope ili kina cha maji kiwe kikubwa na cha kuhifadhi maji ya kutosha, bali hapa serikali ilicheza mchezo mchafu na hawa viongozi walio pitia hiyo wizara ya Nishati na Madini kuanzia JK rais wetu he is behind all this scandal lazima tu na waka ibadirisha issue kuwa ya Gutter politics, Kwa wananchi JK anatabia mmoja ya kukuzunguka mbuyu huku uswazi tuna sema unafki ndio hiyo tabia aliyo nayo.

Nachotaka kuwaeleza ni kwamba nchi hii bila kuandamana au kuiwekea serikali ngumu haitotutendea haki tusingoje serikali ituleteee maendeleo bali tujiletee maendeleo yetu sisi wenyewe, Kwani liko wazi nchi imeyumba JK hawezi sema chochote,

Nili kuta na rafiki yangu aksema ataleta hoja mmoja ya kuwa ni Bora Wajerumani warudi kututawala kwa mkataba wa miaka 5 ya kwanza na tukiona mafanikia basi tunawapa tena miaka 15 up to 20 yrs then mkataba unavunjwa kwanini alisema hivyo ni bora Mzungu atutawale na atatuletea maendeleo na tukijua fika atakuwa anatuibia baadhi ya mali zetu kuliko Mwafrika mwenzetu kututawala na kutuibia na kutunyanyasa waafrika wenzake na hatuoni maendeleo yoyote nchi inabaki kuwa masikini wananchi wanakuwa masikini bali viongozi wao wachache ndio matajiri hapo kipi ni bora. Inatupa shaka sana kuwa hawa viongozi wetu kwa maamuzi kama haya ya kupitisha budget after 2day nchi inarudi gizani maradufu ya mgao wa kwanza kweli ntashindwa hoji hawa viongozi ni watanzania kweli wazalendo kweli ni wa hapahapa Tanzania au ??wana matatizo yapi ya akili au?
 
Am waiting watanzania viboko vya uonevu wanavyopigwa na viongoz wao havijawaingia sawa sawa bado.vikiingia hakutakuwa na muda wa kulalamika tena kutakuwa na muda wa kutafuta ufumbuz au kuitana kuingia mtaan kupinga viboko ivyo
 
Tatizo hili ni nafasi kwa Wataalamu wetu wa kizalendo kutafuta tiba mbadala ya umeme....Co tunalalamika 2 kila kukicha.Malalamiko ye2 hayawezi kupunguza makali ya umeme...Hebu tujiulize sisi Watanzagiza wengine tunaolalamika sana tumefanya juhudi gani juu ya suala hilo?Au tuonekane tunajua kuongea? Na wataalamu wa masuala ya umeme waliokopeshwa elimu vyuoni wapo wapi?Kama wapo watusaidie kulitatua tatizo,ni kweli mvua zimezingua lakini tuna vyanzo mbadala vingi vya umeme.Mfano:UPEPO,JUAKALI SANA,MAKAA YA MAWE n.k..
<br />
<br />
hapana malalamiko ila ufinyu wa uelewa wako
 
Tatizo hili ni nafasi kwa Wataalamu wetu wa kizalendo kutafuta tiba mbadala ya umeme....Co tunalalamika 2 kila kukicha.Malalamiko ye2 hayawezi kupunguza makali ya umeme...Hebu tujiulize sisi Watanzagiza wengine tunaolalamika sana tumefanya juhudi gani juu ya suala hilo?Au tuonekane tunajua kuongea? Na wataalamu wa masuala ya umeme waliokopeshwa elimu vyuoni wapo wapi?Kama wapo watusaidie kulitatua tatizo,ni kweli mvua zimezingua lakini tuna vyanzo mbadala vingi vya umeme.Mfano:UPEPO,JUAKALI SANA,MAKAA YA MAWE n.k..
Ndugu yangu wataalamu unaosema hawawezi kuleta chochote bila fedha ambazo zinakusanywa na serikali hii legelege. Serikali iwape hizo hela hao wataalamu halafu washindwe ndo tuseme na siyo kupewa wanasiasa kama RA (Richmond)
 
Back
Top Bottom