Mkogoti
TAPELI Mkubwa
- May 3, 2020
- 2,416
- 3,911
Watu 10 Wamefariki dunia na Wengine watano kujeruhiwa na kupelekwa hospital teule ya Nyamiaga wilayani Ngara, baada ya gari la abiria mali ya kampuni ya Emirates kuanguka likitokea Ngara kwenda Bukoba.
Mganga mfawidhi wa hospital hiyo, David Mapunda amethibitisha.
Dar es Salaam. Rais wa Tanzania, John Magufuli leo Jumamosi Oktoba 24, 2020 ametuma salamu za rambirambi kufuatia ajali ya basi iliyosababisha vifo vya watu 15.
Ajali hiyo imetokea leo wilayani Ngara Mkoa wa Kagera baada ya basi la kampuni ya Emirates lililokuwa likitokea Ngara kwenda Bukoba kupinduka katika mteremko wa Kumnyange wilayani Ngara Mkoa wa Kagera. Katika ajali hiyo watu 18 wamejeruhiwa.
Taarifa iliyotolewa leo na mkurugenzi wa mawasiliano ya rais Ikulu, Gerson Msigwa inaeleza kuwa Magufuli amemtumia salamu za rambirambi mkuu wa Mkoa wa Kagera, Brigedia Jenerali Marco Gaguti na amemtaka kufikisha salamu za rambirambi kwa familia na wote walioguswa na vifo hivyo na kuwatakia majeruhi wapone haraka.
“Nimesikitishwa na vifo vya Watanzania wenzetu waliopoteza maisha katika ajali hii, nawapa pole wafiwa wote na nawaomba wawe na moyo wa uvumilivu na ustahimilivu katika kipindi hiki kigumu cha majonzi,” amesema Magufuli.
Taarifa hiyo imesema Rais amewataka watumiaji wa barabara hasa madereva wa magari kuzingatia sheria zote za usalama barabarani ili kuepusha ajali zinazoweza kuzuilika.
“Pia amevitaka vyombo vinavyosimamia usalama barabarani kuchukua hatua dhidi ya watumiaji barabara wanaokiuka sheria za barabarani,” imeeleza taarifa hiyo.
Chanzo: Mwananchi
Mganga mfawidhi wa hospital hiyo, David Mapunda amethibitisha.
Ajali hiyo imetokea leo wilayani Ngara Mkoa wa Kagera baada ya basi la kampuni ya Emirates lililokuwa likitokea Ngara kwenda Bukoba kupinduka katika mteremko wa Kumnyange wilayani Ngara Mkoa wa Kagera. Katika ajali hiyo watu 18 wamejeruhiwa.
Taarifa iliyotolewa leo na mkurugenzi wa mawasiliano ya rais Ikulu, Gerson Msigwa inaeleza kuwa Magufuli amemtumia salamu za rambirambi mkuu wa Mkoa wa Kagera, Brigedia Jenerali Marco Gaguti na amemtaka kufikisha salamu za rambirambi kwa familia na wote walioguswa na vifo hivyo na kuwatakia majeruhi wapone haraka.
“Nimesikitishwa na vifo vya Watanzania wenzetu waliopoteza maisha katika ajali hii, nawapa pole wafiwa wote na nawaomba wawe na moyo wa uvumilivu na ustahimilivu katika kipindi hiki kigumu cha majonzi,” amesema Magufuli.
Taarifa hiyo imesema Rais amewataka watumiaji wa barabara hasa madereva wa magari kuzingatia sheria zote za usalama barabarani ili kuepusha ajali zinazoweza kuzuilika.
“Pia amevitaka vyombo vinavyosimamia usalama barabarani kuchukua hatua dhidi ya watumiaji barabara wanaokiuka sheria za barabarani,” imeeleza taarifa hiyo.
Chanzo: Mwananchi