Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Kesho Ijumaa aliyekuwa Mwandishi wa ITV huko Mara Bw. George Marato anatarajiwa kuwa na mkutano na waandishi wa habari kujibu madai yaliyotolewa na Jukwaa la Wahariri kuwa alihusika katika upotoshaji wa habari ambazo zilirudiwa na vyombo vingine vya habari, yeye akiwa ni chanzo kikuu.
Ka "nzi" ambako hakajapata usingizi siku ya nne sasa kamedokeza kuwa Bw. Marato ambaye anafadhiliwa na kundi la wanasiasa kadhaa wakiongozwa na Mbunge mmoja wa kanda ya kati ambaye ni mmiliki wa vyombo vya habari ataitishia mkutano huo ili kujibu jukwaa hilo, lakini pia kuendeleza mgongano wa kifikra na kibiashara dhidi ya ITV na mmiliki wa vyombo vya habari vya IPP Bw. Reginald Mengi.
Uchunguzi wa haraka haraka unaonesha kuwa Jukwaa hilo linasubiri kwa hamu mkutano huo wa Bw. Marato....
(stay tuned)....
Ka "nzi" ambako hakajapata usingizi siku ya nne sasa kamedokeza kuwa Bw. Marato ambaye anafadhiliwa na kundi la wanasiasa kadhaa wakiongozwa na Mbunge mmoja wa kanda ya kati ambaye ni mmiliki wa vyombo vya habari ataitishia mkutano huo ili kujibu jukwaa hilo, lakini pia kuendeleza mgongano wa kifikra na kibiashara dhidi ya ITV na mmiliki wa vyombo vya habari vya IPP Bw. Reginald Mengi.
Uchunguzi wa haraka haraka unaonesha kuwa Jukwaa hilo linasubiri kwa hamu mkutano huo wa Bw. Marato....
(stay tuned)....