NEW SONG; Utaniua by Jux

NEW SONG; Utaniua by Jux

Diamond na kiba nyimbo wanazotoa ni za kawaida tu, ila beef linawabeba, kinachoniuma zaidi media na watangazaji nao wameingia ktk mkumbo huu na baadhi ya wasanii wengine wapumbavu nao wana chagua pande. Inatakiwa hawa waachwe wenyewe wawili wapambane wenyewe na hali zao kwani likiendekezwa beef litaua mziki wetu, kwani wasanii wengine hata watoe nyimbo kali namna gani hazitosikika, ww nyimbo kama ya Jux bonge la nyimbo lkn media na watangazaji wamelikaushia. Hata mwaka jana nyimbo kama samaki ya galatone, lover boy barnaba, sisikii maua sama na nyinginezo nyingi hazikupewa airtime za kutosha kutokana na media na watangazaji kuwa ktk timu hizi . yaani tunapoelekea tukiendelea na ushabiki huu mziki utakuwa wa kiba na mondi.
 
Uyu kawakosea nini watanzania katoa nyimbo nzuri tamu lakini kwa visa na chuki na ubinafsi na wivu lakini hata hamumsapot watu tisa tu wameingia ku comment veemoney pia katoa hit song kisela mpo kimyaa apo nani anaua soko mpo bize na matakataka hawa sio wasanii? Wakijitahidi watusue kwa juhudi zao mtaanza kuwapambanisha na vipusa [emoji23][emoji23] watz kiboko yenu baba jesca tu
 
Dah bonge moja la nyimbo, sometime hili beef la watu wawili (kiba na mondi) linatuharibia gemu watangazaji na radio nao wamekuwa mashabiki, mpaka nyimbo kama hizi zinakosa airtime

Sure ngoma kali sana thou ina sound kama nitasubiri ki melody kwa mbaaali ila hata mimi nimewaza hili bifu la kiba na diamond linaua mziki mzuri maana hii ngoma kali kuliko ngoma zao
 
Ngoja nami nifanye utafiti kwa nini pia simkubali!
Kuna demu mmoja huwa ananidediketia wimbo ule wa wivu, sijui ndo unaitwa hivyo!
Hata siujui ayseee..
Mi nakudediketia seduce me

invest what you are willing to lose
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom