New Release Diamond ft Mr. Flavor

Kuimba na kucheza kama wanaigeria ndiyo wanachompendea wanaona kama mnaigeria mwenzao. Kuna rafiki yangu Mghana yeye ndiye jana amenitumia hiyo nyimbo huku akisema hachoki kucheza na kuimba hiyo nyimbo hivyo huko West africa wanamkubadili kwa ubunifu wake wa kuimba kama wao.

Binafsi sina tatizo na mafanikio ya Diamond ila mie kugeza sana kwa kuimba au kucheza kama taifa lengine huwa sipendelei sana.
 
Mimi nafikiri tuache kuanza kwenda studio sijui kuchana na nini tuendelee na ngoma zetu za MGANDA ndo asili yetu
 
Machozi ya furaha yamenilenga lenga. Safi kuona mtanzania mwenzetu akifanya mambo!
 
Duh Huyu jamaa hawezekaniki tena wanaosubiri ashuke ndo wapande wao, mbona watasubiri sana. Yaani unaweza angalia hata mara 100 haichoshi. Safi sana presidaa wa wasafi
 
Mimi nafikiri tuache kuanza kwenda studio sijui kuchana na nini tuendelee na ngoma zetu za MGANDA ndo asili yetu

Kaka ncha ya mkuki haipigwi konzi. Mwenzenu huyooo mtabaki kuweka nahau tu. Piga pesa kijana, waache wacheze ndondo karume wakisubiri mbeleko.
 
 
Wabongo mnaniacha hoi na kusema asili asili, asili ujinga gani! kwa hiyo mnataka kama ni mkurya basi abaki anatoa single za ritungu?? au wamasai zile ngoma zao wanarukaruka au??? Sioni kitu ambacho kinafanya huu wimbo uwe wa kinigeria au wakibongo au wakizungu,

Its just a song, nyimbo hua tunaziclassify kwenye genre kama rnb, hiphop, jazz, sio bongo, nigerian, blah blah!! Ndo maana wengi mnabaki nyuma kwenye kila kitu kukomaa na mambo ya kizamani hamtaki mabadiliko.
Wasanii kama kumi bongo wangekua na vision kama ya huyu jamaa wangekua mbali tu na full kulipa ushuru...

Kuna rule moja kwa entrepreneurs ya muhimu sana inasema ukipata something that works! kimbia nacho hicho hicho unakiboresha hadi siku something better comes along... Ndio huyu jamaa anavofanya, kaona style yake inalipa anakomaa nayo hiyohiyo na ndo kinachomuweka mjini hadi leo...
 
 
Wasanii wengine nao washaanza kuimba kama wanaigeria,maana kuna muda unakuta zinapigwa nyimbo kwenye radio ukajua zinapigwa ngoma za Nigeria tupu kumbe na za kibongo humohumo usiposikiliza vizuri huwezijua.
 
Nilijaribu kupitia account ya Flavour na mtvbase..nimegundua kua tatzo lipo kwa baadhi ya watanzania...lakin wanaijeria wenyew wameikubali ngoma hiyo..viteam×2 vya kijinga vinatusumbua...
Kwa kweli jamaa c wakushndanishwa na Kiba na wengneo wa hapa hom...richa ya Kiba kua na kipaji na sauti nzur..kafanya nn kwa Taifa lake Tanzania...?
Tuache ushabik wa kijinga....Jamaaa anaweza...!!
 
Last edited by a moderator:
Machozi ya furaha yamenilenga lenga. Safi kuona mtanzania mwenzetu akifanya mambo!

Nilipotizama hii nyimbo sikuamini kama ni mtanzania amefanya haya mambo kiukweli,amefanya mambo ya kipekee sana,audio na video ya hii nyimbo ni ya kiwango cha kimataifa,tutegemee mazuri zaidi kutoka kwa Nassibu
 
 
Hongera zake... ingawa katika kazi zake binafsi naona hii ya kawaida, maybe its my taste.., mpaka leo kwangu naona Ukimwona is one of his best work
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…