New member

Jaman hodi humu ndani naomba muongozo tafadhali maana nimekua mfatiliaji kimya kimya kwa mda mrefu nikaona nakosa uhondo
SHERIA NA KANUNI ZA JAMIIFORUMS

Tafadhali jiepushe na mambo yafuatayo:

1. Kumvunjia heshima, kumkejeli, kumtukana, mjumbe yeyote.

2. Kuleta katika JAMII FORUMS maelezo yenye maudhui mabaya, au kuweza kuleta maudhi yoyote kwa wajumbe ama kwa wingi wake, ukubwa wake, au mfumo wake.

3. Kuleta makala au kuendeleza mijadala yenye kuleta ugomvi, uchochezi na yenye muelekeo wa kutengenishana badala ya kuungana miongoni mwa wajumbe wa JAMII FORUMS na Watanzania wote kwa ujumla.

4. Kuleta maongezi binafsi baina ya mwanachama na mwanachama (waliojisajili) waliyoongea kwa kuaminiana kutoka katika Private Messages (PM) au barua pepe (Emails) na kuyaanika hadharani kwa nia ya kuchafuana.

5. Kusambaza kwa makusudi au kwa uzembe barua zenye virusi vya kompyuta.

6. Kutoa maelezo au shutuma dhidi ya mwanachama mwenzako, kiongozi wa au watu wenye hadhi kijamii bila kuwa na ushahidi wa kutosha kwa lengo la kuchafua rekodi safi ya mhusika kijamii.

7. Ni sharti kwa kila mwanachama kutoa maelezo au mchango wake kwa uwazi na ukweli na kutomuogopa yeyote wala kumpendelea yeyote bali kuweka mbele maslahi ya taifa.

8. Kila mwanachama yupo huru kutoa maoni yake mradi yaliyotajwa hapo juu yanazingatiwa.

Hatua za kinidhamu zinaweza kuchukuliwa dhidi ya yeyote yule atakayeshindwa kuzingatia maelezo hayo hapo juu.
 
Daa kweli mmempokea kwa kumpa changamoto, hata Mimi nimejiunga Jana ila post yangu ya kwanza nilishambuliwa sana kwakuwa niliunganisha maneno sijui hapa napo nimekosea maana Jana waliniambia Mimi no darasa la 1
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom