unavyolalamikia mataifa ya kiarabu je hamas alipoivamia Israel October 7 akaua,akachukua mateka aliwashirikisha hayo kiarabu kama Hamas walilikoroga wenyewe halafu wakategemea waarabu wawasaidie walinywe wenyewe
Sent from my Infinix X663 using
JamiiForums mobile app
Hivi ukija nyumbani kwangu ukaua familia yangu, ukaiba mali zangu, ikapita miaka 30, nikaja kwako nikakuvamia nikaua familia yako, nikachukua mali zangu ulizoniibia hapo unapaswa kulia na kusema nimekuonea?
Kabla ya october 2023, Israel ilishaua maelfu ya Wapalestina na kuchukua ardhi yao kimabavu. Hamas walikuwa kwenye haki.
Israel ni invaders... wanaiba ardhi ya wenza kwa kusema waliahidiwa miaka 3000 iliyopita... hao ni sawa na makaburu ambao hadi sasa wanang'ang'ania South Africa na kusema pale ni kwao.
Wayahudi wengi waliopo Israel ukiwauliza babu yako anatokea wapi, utasikia Germany, UK, US, Morocco, Spain n.k.. ila wale Palestinians ukiwauliza babu zao hata vizazi vinne nyuma watakuambia wametokea pale Palestine...
Kwanini Israel inakataa two state solution? cha ajabu na kushangaza wanarudi nchi yao ya ahadi walioahidiwa na Mungu wanavyodai, walipofika tu serikali imetambua LGBTQ, taifa gani hilo la MUngu linakubaliana na sera za LGBTQ, je hio ISrael ya kale ilikuwa na sera za LGBTQ?
Kwanini hamtumii akili ndogo tu kufahamu ukweli na kuweka mahaba pembeni?
Israel ipi hio ambayo ina sera za kishetani wakati huo huo wanadai maandiko yanasema pale ni kwao? Israel ipi hio ya Mungu inaruhusu wanalenga watoto vichanga kichwani na risasi? hao Hamas hadi kuingia Israel kuua si kwa sababu ni magaidi...
Walichoka kuonewa huku dunia isiwasaidie, mashirika ya umoja wa mataifa walishindwa, mashirika ya haki za binadamu walishindwa... UN ilipigwa kura kuitambua Palestine kama Taifa, kura nyingi zikakubali watambulike... Israel na US wakakataa na kutishia kuzuia misaada kwenda UN.. maana donor mkubwa ni US.
Palestine wamenyanyaswa muda mrefu, mfano mdogo hivi sasa wanavyoteswa hakuna anayeingilia kati hata waarabu wenzao kwa kuhofia kununua ugomvi japo roho zinawauma. Ndipo ujue hawa watu hawana support sehemu yeyote duniani toka miaka na miaka, Israel kabla ya october 7 kuingia Gaza au west bank na kuua Palestianians kwao ilikuwa kawaida miaka na miaka.
Sasa acheni Palestinians wajipambanie kiume, wameamua kutumia damu yao kudai haki yao, na Mungu yupo pamoja nao.
Waafrika tumetawaliwa miaka na miaka, Uingereza imetutawala na kudai ardhi yetu ni mali yao, wameingia hadi vitani wao kwa wao wakigombania mali asili za Africa hadi tulipopambania uhuru wakaondoka. hiko ndicho kinaikuta Palestine dunia ya sasa..