mwanaone
JF-Expert Member
- Apr 2, 2011
- 637
- 760
Naunga mkono . Wa kulaumiwa Ktk Hili ni Maalim kwa kuchukua muda mrefu kuitisha mkutano mkuu wa kuchagua Mwenyekiti na badala Yake akaweka kaimu ili kupata kumcontrol.Itakumbukwa baada ya uchaguzi mkuu huko Zanzibar, CUF ilikuwa na viti vya ubunge vya kutosha lakini baada ya uchaguzi huo kufutwa na ukaitishwa mpya
Maalim na genge lake la Chadema waligomea uchaguzi huo hivyo wabunge waliokuwa wameshinda katika uchaguzi wa awali wakakosa ajira ya ubunge huko zanzibar
Hali imeendelea maalim kawasomesha namba wabunge wengine nane wasio na hatia na hawahusiani na mgogoro wake na Lipumba, ila anawachonganisha na sasa wamekwenda na maji!
Maalim ni mtu wa kuogopwa! Anajali sana maslahi yake kuliko ya watu wengine, ikumbukwe anafanya hivi lakini yeye anakula pesa ya serkali kama makam mstaafu wa rais kwa mujibu wa katiba