Kigugumizi cha Spika Ndugai kuhusu maamuzi ya mahakama ya wabunge 8 wa CUF kinatoka wapi?

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,271
NAKUMBUKA.

1. Tarehe 24/7/2017: Baraza kuu (Feki) la uongozi CUF liliwafukuza uanachama wabunge 8 na madiwani 2.

2. Tarehe 25/7/2017: Ofisi ya bunge ilipokea barua ya kufukuzwa kwa wabunge hao, wakati huo Mh. Ndugai akiwa nje ya nchi.

3. Kesho yake tarehe 26/7/2017 ofisi ya bunge ilitoa taarifa kwa maandishi kuwa Spika wa bunge ameridhia barua ya kufukuzwa kwao na kwa sababu hiyo wabunge hao wamekosa sifa za kuwa wabunge na tayari ameitaarifu tume ya uchaguzi ya taifa NEC.

4. Kesho yake yaani tarehe 27/7/2017 NEC ikasema imepokea taarifa kutoka ofisi ya bunge na tayari imeshateua majina 8 ya kujaza nafasi za wabunge wa viti maalumu.

Sitaki kujua hayo majina yalifika lini NEC na yaliteuliwa na chombo gani, lakini lengo langu ni kutaka kujua ni sababu zipi zimemfanya Spika kuwa mzito kutoa maamuzi ya ofisi yake kuhusiana na hukumu iliyotolewa tangu juzi trh 10/11/2017 iliyotengua kuvuliwa uanachama kwa wabunge 8 wa CUF.

Ile spidi aliyotumia wakati ule kuridhia barua ya Lipumba ya kutenguliwa kwao akiwa ughaibuni mbona haionekani wakati huu ambapo yupo nchini, hata tamko tu kutoka ofisi ya bunge kuwa tumesikia lakini hatujapokea hukumu rasmi hakuna?

Ni kitu gani kimeisibu ofisi yetu ya bunge au anasubiri maelekezo toka juu.

====================================
Hawa ndio wabunge 8 halali wa CUF waliofukuzwa kwa hila na Lipumba.
FB_IMG_1510464827068.jpg
 
THE CIVIC UNITED FRONT (CUF-Chama cha Wananchi)

Imetolewa leo 10/11/2017

TAARIFA KWA UMMA
Leo Mahakama kuu ya Tanzania kulikuwa na kesi No. 479 ya 2017 iliyofunguliwa na waliokuwa HV na wabunge wa chama cha wananchi (cuf)

Kesi hiyo ilikuwa imepangiwa leo ili kutolewa uamuzi wa maombi ya kina Miza na wenzie yafuatayo:

1. Wabunge wateule wasiapishwe na Bunge la Jamhuri ya Muungano

2. mchakato wa ufukuzwaji uanachama wa waombaji usiendelee "implementation of the decison to expell the Applicants from the party"

3. Swala la kufukuzwa kwa waombaji lisiendelee kujadiliwa mpaka kesi ya msingi itakaposikilizwa na kutolewa uamuzi

MAAMUZI
1. Mahakama imesema haina uwezo wa kuliingilia bunge kwa kuzuia lisiapishe wabunge wake

2. Mchakato wa ufukuzwaji uanachama wa waombaji usiendelee "implementation of the decison to expell the Applicants from the paarty" mpaka pale

3. Swala la kufukuzwa kwa waombaji lisiendelee kujadiliwa nje ya korti mpaka kesi ya msingi itakaposikilizwa na kutolewa uamuzi

4. Swala la uanachama wa waleta maombi litaamuliwa na mahakama katika kesi ya msingi.

CUF -Chama cha Wananchi kimeridhia uamuzi huo uliotolewa leo na Jaji Mwandambo na kimsingi Cuf haina nia ya kuendeleza mjadala huo nje ya Mahakama na wala haikua nia ya kuchukua tena hatua za ziada dhidi ya Wanachama hao waliofungua Kesi nakuomba mazuio hayo.

Ama kuhusu zuio la Wabunge Wateule ni kama lilivyoelezwa kwenye hukumu hiyo.

CUF-Chama cha Wananchi kinawataka Wanachama wake kujikita katika kuendeleza kampeni za Madiwani ili kujihakikishia Ushindi na kupuuza upotoshwaji unaofanywa na watu wasio na nia njema na Chama chetu.

Hata hivyo kwakua kumeibuka tabia ya upotoshaji wa mara kwa mara kuhusu maamuzi mbali mbali yanayofanywa na Mahakama kwenye Kesi zinazohusu Cuf, Tunawasiliana na Wakili wetu ili aone uwezekano wa kuijulisha Mahakama juu ya upotoshwaji huu kupitia Msajili wa Mahakama kwani unaleta usumbufu kwa Wanachama wetu na Watanzania kwa ujumla wake.

Abdul Kambaya
Mkurugenzi wa Habari,Uenezi na Mahusiano na Umma
 
Nawalia timing, wakiingia wazimawazima naandika barua ya kuwatimua uanachama akina chenge, kibajaji na Kigwangwala.

Hopefully hataangalia nani kaandika barua as usual.
 
NAKUMBUKA.

1. Tarehe 24/7/2017: Baraza kuu (Feki) la uongozi CUF liliwafukuza uanach........kasome katiba ya cuf au subiri kesi ya msingi iishe

(((Sitaki kujua hayo majina yalifika lini NEC na yaliteuliwa na chombo gani, )))
Aliyechukua nafasi ya Sophia Simba jina lake lilifikaje nec
Pia majina hayo yote ni katika aliyopeleka sultan sefu kama karibu mkuu


2kini lengo langu ni kutaka kujua ni sababu zipi zimemfanya Spika kuwa mzito kutoa maamuzi ya ofisi yake kuhusiana na hukumu ilitokoka tangu juzi trh 10/11/2017 iliyotengua kuvuliwa uanachama kwa wabunge 8 wa CUF.

Ile spidi aliyotumia wakati ule kuridhia barua ya Lipumba ya kutenguliwa kwao akiwa ughaibuni mbona haionekani wakati huu ambapo yupo nchini, hata tamko tu kutoka ofisi ya bunge kuwa tumesikia lakini hatujapokea hukumu rasmi hakuna? Ni kitu gani kimeisibu ofisi yetu ya bunge.
Mwisho subiri kesi ya msingi itakapokwisha
 
Game Over Mkuu...kwani mwenyekiti Lipumba kapeleka barua kwa Spika?
 
NAKUMBUKA.

1. Tarehe 24/7/2017: Baraza kuu (Feki) la uongozi CUF liliwafukuza uanachama wabunge 8 na madiwani 2.

2. Tarehe 25/7/2017: Ofisi ya bunge ilipokea barua ya kufukuzwa kwa wabunge hao, wakati huo Mh. Ndugai akiwa nje ya nchi.

3. Kesho yake tarehe 26/7/2017 ofisi ya bunge ilitoa taarifa kwa maandishi kuwa Spika wa bunge ameridhia barua ya kufukuzwa kwao na kwa sababu hiyo wabunge hao wamekosa sifa za kuwa wabunge na tayari ameitaarifu tume ya uchaguzi ya taifa NEC.

4. Kesho yake yaani tarehe 27/7/2017 NEC ikasema imepokea taarifa kutoka ofisi ya bunge na tayari imeshateua majina 8 ya kujaza nafasi za wabunge wa viti maalumu.

Sitaki kujua hayo majina yalifika lini NEC na yaliteuliwa na chombo gani, lakini lengo langu ni kutaka kujua ni sababu zipi zimemfanya Spika kuwa mzito kutoa maamuzi ya ofisi yake kuhusiana na hukumu iliyotolewa tangu juzi trh 10/11/2017 iliyotengua kuvuliwa uanachama kwa wabunge 8 wa CUF.

Ile spidi aliyotumia wakati ule kuridhia barua ya Lipumba ya kutenguliwa kwao akiwa ughaibuni mbona haionekani wakati huu ambapo yupo nchini, hata tamko tu kutoka ofisi ya bunge kuwa tumesikia lakini hatujapokea hukumu rasmi hakuna?

Ni kitu gani kimeisibu ofisi yetu ya bunge au anasubiri maelekezo toka juu.
Kabla wewe hujafikiria kuandika uzi huu, kuna "wataalamu wa sheria" sijui kutoka wapi, wamesambaza upupu kwamba maamuzi yanayofanywa na Bunge hayapaswi kuingiliwa na chombo chochote! Yaani, hawa wajinga wanataka kutuambia kwamba kwa kuwa Bunge lilifanya mambo ya kimhemko wa kisiasa likajifanya kipofu kwa yanayoendelea CUF, sasa lisiguswe tena kwa maamuzi ya hovyo lililofanya!
 
Spika alikuwa mahakamani au unataka atumie taarifa ya JF kutoa kauli ya Spika? Huu ni uzuzu, yaani Spika aseme mambo ya mhimiri mwingine Kama hajapewa barua? Wewe juzi hili jambo tumeongea na wewe na wewe procedure unazijua. Mnakimbilia wapi Kama hiyo ni haki yenu? Dogo watakupoteza be carefully
 
Ndugai anapokea maagizo toka kwa Sizonje. Wakati mahakama inatoa maamuzi haya, Sizonje alikuwa nje ya nchi. Kwa sasa amerejea nchini. Subiri kesho Jumatatu uone Ndug@i atakavyopopoma baada ya kuwa kashapewa maagizo na dikteta.
 
Back
Top Bottom