NEC: Jina la Tundu Lissu liko mwisho wa karatasi ya kupiga kura kwasababu alirejesha fomu akiwa wa mwisho

Mathias Byabato

JF-Expert Member
Nov 24, 2010
1,020
691
Akihojiwa na kituo cha redio Kagera Community Radio(KCR FM) leo asubuhi Ofisa elimu kwa umma kutoka Tume ya uchaguzi (NEC Bw Titus Mwanzalila amesema kigezo kilichotumika ni urejeshwaji wa fomu za wagombea Urais ambapo mgombea wa Urais kupitia CCM John Magufuli alirejesha fomu akiwa wa kwanza na Tundu Lissu alirejesha akiwa wa mwisho.

Ameongeza kuwa kwa ngazi za ubunge na udiwani wagombea walipangwa katika karatasi za kura kwa maelekezo ya Tume

Hata hivyo amesema hiyo si sababu ya mpiga kura kutompigia kura mgombea anayemtaka.

Katika hatua nyingine amesema tume imejipanga kikamilifu kuondoa changamoto katika mchakato huu wa uchaguzi.

Nikipata nafasi nitawawekea audio clip
mbarikiwe

Byabato
Bukoba.
 
Aaaa Wapi! Hii sababu haijitoshelezi hata kidogo, yaani wanataka kusema kuwa walikua wanaanda karatasi ya kupigia kura kufuatana na jinsi mgombea alivyowasilisha form!???
Ni sababu za kizamani kabisa, wenye akili wameshang'amua, hilo sio bure ni sehemu ya mkakati sababu hata Mgombea wa CCM hakuwa wa kwanza kupeleka form, hata Lissu aliwahi mapema tu lakini akakalishwa na kuhifadhiwa kwenye chumba mpaka saa moja usiku, halafu leo unakuja hadharani na kijisababu cha kumatamata kama hiki, watanzania wa leo sio wa jana!
 
Back
Top Bottom