Ndugu zangu wananichukia


ndio tofauti ya kusoma na kutosoma....vitabia vya ajabu kwa dada yako kunachangiwa na akili mbovu....sasa weweumesoma unajitambua cha muhimu fanya yako kwani ushaona kila kitu kimewekwa wazi sasa mambo ya kuwshirikisha yatakukost zaidi...hata mama yako kwa stage hiyo haaminiki kwa kuwa anamezwa na dada na baba wa dada yako yani mume wake mama yako...so fanya yako kabisaa wao waneachiwa mali wewe huna...yani achana nao
 
ndio tofauti ya kusoma na kutosoma....vitabia vya ajabu kwa dada yako kunachangiwa na akili mbovu....sasa weweumesoma unajitambua cha muhimu fanya yako kwani ushaona kila kitu kimewekwa wazi sasa mambo ya kuwshirikisha yatakukost zaidi...hata mama yako kwa stage hiyo haaminiki kwa kuwa anamezwa na dada na baba wa dada yako yani mume wake mama yako...so fanya yako kabisaa wao waneachiwa mali wewe huna...yani achana nao
 
Nyakati ngumu kwenye maisha yetu...haziji kwa nia ya kutuadhibu bali huja kwa nia ya kutufunza jambo fulani muhimu....hayo wanayokutendea nduguzo ni moja ya masomo muhimu sana kwenye maisha jambo la msingi ni kumshukuru kwa kuweza kusimama mwenyewe kwenye maisha yako na kuhangaikia maisha yako....

Mwanadamu mwenye akili timamu hujifunza kutokana na makosa...huna sababu a kujilaumu wala kunungunika kwa wakati bali unatakiwa kufungua ukuras mpya kwenye maisha yako na kuufunga ukurasa wa zamani......

Maisha yetu ni mafupi hivyo hatupaswi kuishi kwa kusononeka na kukosa raha bali tunatakuwa kuyafurahia maisha kwa kadri ya uwezo wetu.......usiwatenge nduguzo kwani hata wao hawajui walitendalo na ipo siku watajutia kile wakutendeacho pindi maruhani wa chuki watakapo waacha huru.....


DONT TRUST NO ONE...DONT EVEN TRUST YOURSELF......
 

Acha kabisa kuna wamama wamepinda , Kuna mmoja mdingi kafariki ye ananza kuuza nyumba za urithi na kula maisha na dogodogo badala ya kusomesha watoto.
 
Waafrika ukitaka kukosana nao ni vitu viwili:Muhusishe na mambo ya pesa kwa kimkabidhi au wanawake/wanaume wenu wawe na ukaribu usio na mipaka!

Isha jifunza sana hivi vitu viwili,vimekosanisha watu wengi sana
 
Undugu ndio nini? Piga chini hao wote, kata mawasiliano nao, acha kuwapa hela na concentrate katika kujenga maisha yako badala ya kukaa unaulilia undugu wa kulazimisha. Swala la nyumba ungebadili mipango yake na badala yake tafuta kiwanja karibu na unapofanyia kazi au unapoishi ili uweze kusimamia ujenzi kwa urahisi. Narudia tena, achana na undugu wa kulazimisha kama hutakiwi.
 
Mungu awabariki wote mlionishauri na kunipa moyo,,asanteni sana
Mtunzi mahiri almarhum shaaban Robert anamzungumzia hasidi anasema
Hasidi ale ngano kwa samli
Na vimanda vya mayai
Awe na taa za kandili
Fanusi na karabai
Atahusudu moshi wa koroboi
Unaotoka kwa masikini
Hasidi avae silk hariri
Na mérimeri
Awe na yakuti almasi na johari
Na dhahabu tele zimejaa vidoleni
Atahusudu shaba ilioko shingoni
Mwa masikini
Hasidi umuhusudu alie mtoa tumboni.
Huu ndo ujumbe wangu kwako dada.
 
UKWELI LAZIMA USEMWE UNAISHI NA WACHAWI,NA IKO SIKU WATAKUPOTEZA,JIWEKE MBALI NAO LAKINI MAMA NI MAMA USIMSAHAU KIHALI NA KIMALI.
 
MKUU HAO NI WACHAWI HAKIKA,NA AKICHEZA WANAMUUA.UKUMBUKE ALINYANYASIKA NA MAMA ALIKUWEPO,VIGAGULA HIVYO AVIEPUKE
 
Dada usikate tamaa bado nafasi unayo! Histoshe kwa hayo mambo ni ya kawaida kwa wabongo washio uswahilini mahana wengi yanawatokea.
 
Huwezi mtenga mama ila ningekushauri nenda kauze hicho kiwanja itakupunguzia machungu tena nenda ukiwa huko happy kama walidhani utakonda wakonde wao ukifika hapo wachangamkie vizuri ila wasijue kusudi lako uza kajenge hukouliko dawa ya adui si kumchukia ni kuzidisha upendo kama ni binadamu dhamira itamsuta
 
A
SIMWACHE *****,ADUI HAPENDWAGI ANAEPUKWA SIKU MOJA OKOTA NYOKA UISHI NAE NDANI MKUU
 
Uliza vizuri pia kuhusu kiwanja wasije wakawa wameisha uza??
ulichokosea kuendelea kumuamini b mkubwa wakati alishakuliza.yeye kuwa n mama haina maana kuwa hana mapungufu na si kwamba hakupendi
 
Dah,nimewaza kwa kina saaana baada ya kumaliza kusoma huu uzi wako na comments za wadau wengine!nimeishia kushusha pumzi ndefu tu na kuisindikiza na glass ya maji baridi...pole bi dada,ndo majaribu ya maisha wengi wameshauri ya maana na yenye kujenga,fanyia kazi ushauri wao. Ahsante.
 
Elekeza nguvu zako kwenye kujipanga mwenyewe. Wasiopenda/taka maendeleo yako kua nao makini
 
Wakati naandika uzi huu nilikuwa na huzuni iliyochanganyika na akili kuruka,nilikuwa sijui pa kuanzia wala kumalizia,,ila asante kwa Mungu anaenitia ujasiri na nguvu hadi dakika hii,asanteni pia wana jukwaa wote mnaoendelea kunishauri na kunifanya niendelee kupata ahueni ya majeraha haya,Mungu akijalia nikikaa sawa kiakili nitaanza kujijenga tena upya kiuchumi, I hope cku moja nitaleta mrejesho wa mafanikio humu.MUNGU awabariki sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…