Ndugu zangu wananichukia

Ndugu zangu wananichukia

Dada mwenye akili na maarifa tafuta mume mwema ujenge familia yako utayasahau yote hayo.
 
Are you married miss Jay?
Yaani wanawake wenye traits kama zako ni so rare kufind siku hizi.
 
cha kufanya usiwashirikishe tena na tena ktk biashara zako wala mipango yako.....hata ukitaka kujenga tena nunua kiwanja kimya kimya anza kujenga kimya kimya....achana nao kabisa wasahau ktk ratiba zako wamekutenda vya kutosha. huyo mama wa ajabu sana anamrudisha nyuma maendeleo ya mwanae..
 
anza kufanya mambo yako mwenyewe wasalimie tu hao ndugu zako ila wasiione hata senti moja yako,ingawa ningekuwa mimi ningewapotezea wote moja kwa moja hadi nafa.
 
Pole Sana Miss Jay. Mama ni mama tu hata awe na mapungufu gani ww jitahidi huyakubali tu. Msamehe bure ipo siku atagundua wapi alitenda kosa lake. Kuwaweka katika matabaka anakosea Sana . cha msingi Kama wadau wengine walivyochangia, jitahidi Sana kufanya mambo yako jirani na maeneo ambayo ni rahisi ww MWenyewe kufika na kusimamia kwa u karibu zaidi.
Nilitengwa hivyo na kaka zangu baada ya mama kufariki, sikupewa msaada kielimu tangu darasa la4. Baada ya kuhitim darasa la7 nikakaa miaka2 bila kuendelea na shule zaidi ya wao kunitumia kwa shughuli zao tu. Nikapigania mwnyewe na nikaanza shule 2008(secondary), 2012(diploma), ss nipo mwana wa2 degree ya irrigation na civil (Arusha technical college).
My take: usiache kumsaidia mama yako pale anapohitaji na pale utakapoweza. Pia usiache kuwaombea mema siku zote.
Maendeleo yako yapo mikononi mwako.
 
Hebu simama mwenyewe, fanya hao hawapo kabisa.....
 
Habari wana JF,

Mimi ni kijana wa kike mwenye umri kati ya miaka 25-30. Ninao ndugu zangu wawili ambao tangu nmekua na kujielewa nimekuwa nikiishi nao, ndugu hao ni mama yangu mzazi na dada yangu mkubwa. Mimi ni wa mwisho kuzaliwa lakini bahati mbaya nilipokuwa darasa la pili baba yangu alifariki na inasemekana baba yangu hakuwa na mtoto mwingine zaidi yangu, dada yangu yeye ana baba yake na yuko hai.

Kisa chenyewe ni kwamba hawa ndugu zangu wana maisha mazuri japokuwa dada yangu hakusoma sana kutokana na kutokuwa na akili za darasani lakini baba yake ni mtu mwenye uwezo hivyo alimpa mtaji na huwa anafanya biashara.Tangu baba yangu kufariki nilianza kupata ubaguzi kutoka kwa dada yangu huyu maana alikuwa akiletewa vitu na baba yake mimi hanigawii na tukiwa chumbani basi huniringishia,mimi nilivumilia na kuendelea na maisha.Mama yetu alikuwa akimkemea lakin hakuacha hiyo tabia,mimi nilisoma kwa bidii nikafaulu level zote hadi kufika chuo kikuu.

Baada ya kumaliza chuo na kupata kazi nilipata wazo la kutafuta mali zangu maana baba yangu hakuniachia kitu,kila tunachomiliki kama familia ni cha baba wa dada yangu hadi nyumba tunayoishi.Hivyo nikaamua kujenga kule aliko mama yangu maana mimi nafanya kazi mkoa tofauti na mama anapoishi,mara ya kwanza nikamtumia mil 3 ili anunue matofali 3000 ya block kwa ajili ya ujenzi, nikanunua na ramani kwa mkandarasi nikaituma ili ujenzi uanze.Baada ya mwezi nikaanza kluwa natuma pesa kila mwezi kwa ajili ya vifaa kama cement,mchanga,mawe na gharama za kulipa mafundi ili wajenge,nia yangu ilikua kujenga nusunusu kila mwezi hadi nimalize.

Sasa juzi baada ya kuwasiliana na mama na kuniambia nyumba imefika kwenye lenta niliamua kufanya ziara ya kushtukiza ili nikaione nyumba yangu,cha ajabu nilipofika eneo la tukio nikakuta hakuna nyumba wala msingi, hata miti ambayo niliwahi kutuma pesa ili inunuliwe ipandwe haikuwepo yaani kiwanja kilikuwa cheupe, niliishiwa nguvu na kulia kama nimefiwa, nilienda hadi kwa mama kumuuliza kilichojiri lakini hakuwa na jibu la kueleweka, mara amejnga sehemu nyingine na nilipomuambia anipeleke akasema amepasahau hapakumbuki, niliondoka siku hiyo hiyo kurudi ninakofanyia kazi lakini moyo wangu umeumia pasipo mfano,nimepigana sana kutafuta pesa zangu lakini ndugu zangu wananirudisha nyuma,

Kabla ya hapa pia nimewahi kumkopea huyu dada yangu pesa kwenye vyama kama mil 1 lakin aligoma kulipa nkadaiwa mimi, na pia wakati nasoma nlikua nafanya biashara ya nguo nachukua kariakoo natembeza kwenye hostel za chuo sasa kuna kipindi nikawa bize na research nikampa mama yangu mzigo wa nguo wa laki 8 aniwekee dukani kwake aziuze then ubize ukiisha nitaendelea na biashara lakini mzigo aliuza na pesa hakunipa akidai kuwa alikopesha na hakulipwa.

Nimeshindwa kuelewa hawa ndugu zangu kwanini wananifanyia hivyo wakati vitu vyao na mali zao mimi hawanipi na wananinyanyasia na nikitafuta vyangu wananidhulumu, kwa kweli naumia hata sijui cha kufanya.

Maisha ni darasa. Mshukuru Mungu umehitimu hiyo level na cheti umekabidhiwa.
Sasa ingia mzigoni maana wamekudhulumu pesa ila nguvu, akili uhai bado.

Piga kazi utatoka vizuri tu tena usiwachukie
 
Pole sana dear, wasamehe ila kuanzia wakati huu usiwashirikishe kwenye mambo yako ya maendeleo. Kaa mbali nao. Uende kuwaona mara moja moja tu tena kwa surprise.

Usiwang'ang'anie watu wasiokupenda na kukuthamini. Mkaribie Mungu...atakutetea atakupigania na kukusimamia issue zako pasipo ndugu zako.
 
Masikini weee fanya yako km ww usiendekeze ndugu zako maisha popote na silazima ujenge ulipo kulia unaweza ukaanza hapo ulipo na biashara ukaanza hapohapo ulipo
Unakofanyia kazi unapoona ndugu kikwazo kwako usiwaendekeze fanya yako
 
Mungu awabariki wote mlionishauri na kunipa moyo,,asanteni sana
 
Habari wana JF,

Mimi ni kijana wa kike mwenye umri kati ya miaka 25-30. Ninao ndugu zangu wawili ambao tangu nmekua na kujielewa nimekuwa nikiishi nao, ndugu hao ni mama yangu mzazi na dada yangu mkubwa. Mimi ni wa mwisho kuzaliwa lakini bahati mbaya nilipokuwa darasa la pili baba yangu alifariki na inasemekana baba yangu hakuwa na mtoto mwingine zaidi yangu, dada yangu yeye ana baba yake na yuko hai.

Kisa chenyewe ni kwamba hawa ndugu zangu wana maisha mazuri japokuwa dada yangu hakusoma sana kutokana na kutokuwa na akili za darasani lakini baba yake ni mtu mwenye uwezo hivyo alimpa mtaji na huwa anafanya biashara.Tangu baba yangu kufariki nilianza kupata ubaguzi kutoka kwa dada yangu huyu maana alikuwa akiletewa vitu na baba yake mimi hanigawii na tukiwa chumbani basi huniringishia,mimi nilivumilia na kuendelea na maisha.Mama yetu alikuwa akimkemea lakin hakuacha hiyo tabia,mimi nilisoma kwa bidii nikafaulu level zote hadi kufika chuo kikuu.

Baada ya kumaliza chuo na kupata kazi nilipata wazo la kutafuta mali zangu maana baba yangu hakuniachia kitu,kila tunachomiliki kama familia ni cha baba wa dada yangu hadi nyumba tunayoishi.Hivyo nikaamua kujenga kule aliko mama yangu maana mimi nafanya kazi mkoa tofauti na mama anapoishi,mara ya kwanza nikamtumia mil 3 ili anunue matofali 3000 ya block kwa ajili ya ujenzi, nikanunua na ramani kwa mkandarasi nikaituma ili ujenzi uanze.Baada ya mwezi nikaanza kluwa natuma pesa kila mwezi kwa ajili ya vifaa kama cement,mchanga,mawe na gharama za kulipa mafundi ili wajenge,nia yangu ilikua kujenga nusunusu kila mwezi hadi nimalize.

Sasa juzi baada ya kuwasiliana na mama na kuniambia nyumba imefika kwenye lenta niliamua kufanya ziara ya kushtukiza ili nikaione nyumba yangu,cha ajabu nilipofika eneo la tukio nikakuta hakuna nyumba wala msingi, hata miti ambayo niliwahi kutuma pesa ili inunuliwe ipandwe haikuwepo yaani kiwanja kilikuwa cheupe, niliishiwa nguvu na kulia kama nimefiwa, nilienda hadi kwa mama kumuuliza kilichojiri lakini hakuwa na jibu la kueleweka, mara amejnga sehemu nyingine na nilipomuambia anipeleke akasema amepasahau hapakumbuki, niliondoka siku hiyo hiyo kurudi ninakofanyia kazi lakini moyo wangu umeumia pasipo mfano,nimepigana sana kutafuta pesa zangu lakini ndugu zangu wananirudisha nyuma,

Kabla ya hapa pia nimewahi kumkopea huyu dada yangu pesa kwenye vyama kama mil 1 lakin aligoma kulipa nkadaiwa mimi, na pia wakati nasoma nlikua nafanya biashara ya nguo nachukua kariakoo natembeza kwenye hostel za chuo sasa kuna kipindi nikawa bize na research nikampa mama yangu mzigo wa nguo wa laki 8 aniwekee dukani kwake aziuze then ubize ukiisha nitaendelea na biashara lakini mzigo aliuza na pesa hakunipa akidai kuwa alikopesha na hakulipwa.

Nimeshindwa kuelewa hawa ndugu zangu kwanini wananifanyia hivyo wakati vitu vyao na mali zao mimi hawanipi na wananinyanyasia na nikitafuta vyangu wananidhulumu, kwa kweli naumia hata sijui cha kufanya.
 
Fanya yako kivyako watakutia umasikini.Tafuta sehemu ambayo una uhakika kama utaweza kuja kuishi jenga hapo.Mweke mungu mbele na usimwamini ndugu wala rafiki.Mambo yako yatakuwa unanyotaka pale utakaposimamia wewe mwenyewe
 
''..ndugu hao ni mama yangu mzazi na dada yangu mkubwa..''
Nakupa pole kwa unayopitia ila mama yako sio ndugu yako
 
Pole sana dada yangu, fanya mambo yako achana nao hondoa mikono yako kwa. Na waangalie tu, na kaa kimya ukifanya mwenywe.
 
Back
Top Bottom