Mgibeon
JF-Expert Member
- Aug 7, 2011
- 11,141
- 20,787
Dear Comrades kwanza poleni sana kwa majukumu mazito na changamoto zilizopo mbele yetu, pia Tuendelee kumchangia Ndg yetu Tundu Lissu kwa chochote tunachobarikiwa na Mwenyezi Mungu pasi na kusahau Maombi na Dua zetu juu take.
Iko hivi, ukifuatilia kwa undani mawazo na matumaini ya wengi wetu ni kwamba HATUWEZI kushinda kiti cha urais katika uchaguzi ujao, ila wengi tunajifariji kwamba tutaongeza viti vya wawakilishi wetu pale Bungeni, na mpango-kazi ni kua tukishakua na wawakilishi wengi basi maamuzi mengi yatafanywa kutoka kwa wabunge wa upande wetu, HUU NI UPUUZI wa kiwango cha lami.
Binadamu tunatofautiana sana kwa mawazo na misimamo, Mimi binafsi siwezi kushiriki katika pambano au mtihani au kazi ambayo najua wazi kabisa kwamba SITOFAULU. Ukiangalia rekodi zilizopo utagundua kitu kimoja kwamba CCM inashinda si kwasababu inapendwa sana au inawafuasi wengi ila ni kwa MBINU CHAFU TU. Hata humu JF ukifuatilia vizuri wanaoitetea CCM Hata 50 hawafiki, wengi wanazidi kujiengua kutoka huko na asilimia kubwa waliobaki huko ni wanufaika wa mfumo.
Hatuwezi kushinda bila TUME HURU, na hatuwezi kupata Tume huru bila KATIBA MPYA ambayo Serikali iliyopo haiwezi kukubali ipatikane maana itakua ni sawa na kujichoma kisu. Tafsiri yake ni kwamba tutaendelea kubaki kuwa wapinzani labda mpaka kizazi chetu kiishe, na amini nawaambieni ndugu zangu kama 2020 kutakua na uchaguzi basibasi msishangae tubaki na majimbo matano(5) tu na tena tutayapata kwa mbinde sana.
Kila nikiwaza figisu figisu za uchaguzi uliopita ambao kwa maoni ya wengi ni uliongozwa na Mwanademokrasia Mzee wetu Jakaya sipati picha huu unaokuja utakuaje!!! Fikirieni watu kama akina Mdee, Bulaya, Lema na wengine wengine wapo bungeni kwa nguvu ya ziada siyo kwasababu TUME ilikua fair kwao achilia mbali wale waliopoteza viti vyao.
Sasa namna gani huu uongozi uliopo sasa? Ukimtazama mwenyekiti wao wa sasa na aina ya siasa anayoitaka nchini kwetu unaona kabisa kaburi letu halipo mbali. Kumbuka zile kauli zake kwamba MTU analipwa mshahara, posho, kodi, na gharama mbali mbali kutia ndani usafiri halafu anatangaza mpinzani kashinda, au nachukia wanasiasa huku akijitanabaisha kua yeye siyo mwanasiasa, unaona kabisa kua uchaguzi ujao afe beki afe kipa hakuna mpinzani kushinda.
Sasa ndiyo hapo ninapokumbuka kauli ya mhenga wa sikuzetu Mrisho Mpoto alipomwambia mjomba'ake kwamba "Kufumbatia maji kama jiwe ni ujinga". Kushiriki uchaguzi kwa mbinu zile zile huku tukijua matokeo yake ni UPUUZI wa ajabu sana. Sijui kamati kuu imejipangaje ila inahitaji AKILI na mbinu za hali ya juu sana kushinda uchaguzi ujao, kumbuka issue siyo HOJA za kuwapa wananchi, issue ni MBINU CHAFU, Hilo TU!!! Ni lazima tutengeneze mikakati madhubuti ya kupambana na hizo mbinu CHAFU ambazo na uhakika zitatumika kuliko uchaguzi wowote uliowahi kutokea Tanzania na hayumkini kuliko uchaguzi wowote utakao kuja kutokea!
" mwerevu huona dhoruba na kujificha, mpumbavu huendelea kwenda tu"(edited)
Iko hivi, ukifuatilia kwa undani mawazo na matumaini ya wengi wetu ni kwamba HATUWEZI kushinda kiti cha urais katika uchaguzi ujao, ila wengi tunajifariji kwamba tutaongeza viti vya wawakilishi wetu pale Bungeni, na mpango-kazi ni kua tukishakua na wawakilishi wengi basi maamuzi mengi yatafanywa kutoka kwa wabunge wa upande wetu, HUU NI UPUUZI wa kiwango cha lami.
Binadamu tunatofautiana sana kwa mawazo na misimamo, Mimi binafsi siwezi kushiriki katika pambano au mtihani au kazi ambayo najua wazi kabisa kwamba SITOFAULU. Ukiangalia rekodi zilizopo utagundua kitu kimoja kwamba CCM inashinda si kwasababu inapendwa sana au inawafuasi wengi ila ni kwa MBINU CHAFU TU. Hata humu JF ukifuatilia vizuri wanaoitetea CCM Hata 50 hawafiki, wengi wanazidi kujiengua kutoka huko na asilimia kubwa waliobaki huko ni wanufaika wa mfumo.
Hatuwezi kushinda bila TUME HURU, na hatuwezi kupata Tume huru bila KATIBA MPYA ambayo Serikali iliyopo haiwezi kukubali ipatikane maana itakua ni sawa na kujichoma kisu. Tafsiri yake ni kwamba tutaendelea kubaki kuwa wapinzani labda mpaka kizazi chetu kiishe, na amini nawaambieni ndugu zangu kama 2020 kutakua na uchaguzi basibasi msishangae tubaki na majimbo matano(5) tu na tena tutayapata kwa mbinde sana.
Kila nikiwaza figisu figisu za uchaguzi uliopita ambao kwa maoni ya wengi ni uliongozwa na Mwanademokrasia Mzee wetu Jakaya sipati picha huu unaokuja utakuaje!!! Fikirieni watu kama akina Mdee, Bulaya, Lema na wengine wengine wapo bungeni kwa nguvu ya ziada siyo kwasababu TUME ilikua fair kwao achilia mbali wale waliopoteza viti vyao.
Sasa namna gani huu uongozi uliopo sasa? Ukimtazama mwenyekiti wao wa sasa na aina ya siasa anayoitaka nchini kwetu unaona kabisa kaburi letu halipo mbali. Kumbuka zile kauli zake kwamba MTU analipwa mshahara, posho, kodi, na gharama mbali mbali kutia ndani usafiri halafu anatangaza mpinzani kashinda, au nachukia wanasiasa huku akijitanabaisha kua yeye siyo mwanasiasa, unaona kabisa kua uchaguzi ujao afe beki afe kipa hakuna mpinzani kushinda.
Sasa ndiyo hapo ninapokumbuka kauli ya mhenga wa sikuzetu Mrisho Mpoto alipomwambia mjomba'ake kwamba "Kufumbatia maji kama jiwe ni ujinga". Kushiriki uchaguzi kwa mbinu zile zile huku tukijua matokeo yake ni UPUUZI wa ajabu sana. Sijui kamati kuu imejipangaje ila inahitaji AKILI na mbinu za hali ya juu sana kushinda uchaguzi ujao, kumbuka issue siyo HOJA za kuwapa wananchi, issue ni MBINU CHAFU, Hilo TU!!! Ni lazima tutengeneze mikakati madhubuti ya kupambana na hizo mbinu CHAFU ambazo na uhakika zitatumika kuliko uchaguzi wowote uliowahi kutokea Tanzania na hayumkini kuliko uchaguzi wowote utakao kuja kutokea!
" mwerevu huona dhoruba na kujificha, mpumbavu huendelea kwenda tu"(edited)