Uchaguzi 2020 Ndugu Polepole kitendo cha kusema hadharani kuwa Lissu "Siyo mwenzetu" na umepanga kumuanika siku saba za mwisho ni upuuzi mwingine katika siasa!

dikteta2020

JF-Expert Member
Aug 14, 2018
595
3,990
Hizi siasa za kuchafuana utu kwa mambo ya kipuuzi, kumshushia mwenzako hadhi ya ubinadamu wake na huku ukijua alikotokea ni jambo la kipuuzi na linapaswa kukemewa hadharani.

Hii inanifanya niamini kuwa hukumu za jana ndani ya mahakama ya Kisutu zilikusudiwa kupangwa kisiasa.

Watanzania tunajua kuwa Tundu Lissu hakupenda kwenda kuishi huko Ulaya ambapo mnasema ana uraia. Kilichompeleka huko ni gharama za siasa zetu mufilisi za kuwa tayari kuua pale mnapokuwa hamkubaliani kwa hoja. Hivyo ni lazima tuwe na hofu ya Mungu maana Karma ni kweli!

Kitendo cha Polepole kumpakazia Tundu Lissu ushoga hadharani kwa kweli hakikubaliki. Alienda Ulaya kutibiwa baada ya kuumizwa na wasiopenda ushindani wa kisiasa! Kusema hivyo ni kukosa hoja mbadala za ushindani wa kisiasa na kutapelekea matatizo zaidi.

Nakuona unaongea kwa ukali kuhusu kada wenu aliyeuawa huko Njombe, kama wewe ulivyoumia basi kila mmoja wetu linapomfika tatizo anapata kipimo hicho hicho cha maumivu. Lazima tuheshimu uhai wa kila mmoja wetu! Nchi hii siyo ya bata na kuku! Ni ya watu wenye miili sawa, na kila mmoja wetu linapomfika tatizo huumia kwa kiwango kile kile kilichokuumiza wewe! Tafadhali sana!

Mtaanza kuja na ujinga wa kudhalilisha utu wa watu kwakuwa tu mnataka madaraka. Hilo kamwe halikubaliki. Tufanye siasa za hoja zikitolewa tuhuma zijibiwe bila kudhalilishana kwa kiwango unachopanga kufanya. Hiyo ndiyo maana halisi ya siasa.

Polepole, unakoelekea siko!
 
Huo muda aliokuwa anaongea upupu, bora TBC 1 wangeweka hata kipindi cha mziki wa zamani na Chacha Maginga.

Yaani siku zote hizo wamekaa ndani wakijadili hoja za kumjibu Lisu, vichwa vyote ndivyo vimemtuma aongee ujinga?

Kwa mwelekeo wa mazungumzo yake, hizo tarehe 7 za mwisho anajiandaa kumtangaza Lisu kama shoga, rejea kauli yake baada ya kusema anasubiri siku saba za mwisho.
 
Na mimi nilimskiliza kwa muda, nikagundua anaongea ugoro tu hivyo nikaona ni vyema kubadili channel.

Sijui ni kwa nini ccm wanajiona wana haki sana ndani ya nchi yetu kuliko Watanzania wengine.

Mbona yamefanyika mauaji mengi ya kikatili na kujeruhiwa kwa Watanzania wengi! Lakini hatukuwahi kumuona yeye au mwenyekiti wake akikemea! Ila leo kuuwawa kwa huyo kada mwenzao wa ccm, basi wanataka kulazimisha nchi kusimama!

Shame on you Humprey Polepole
 
CCM hawana hoja. Wamebananishwa kwenye kona, hawana pa kukimbilia. Utawasikia, siyo mwenzetu, mabeberu, ukoloni mamboleo... Kauli za jumla jumla tu ambazo hazina msingi. Hawawezi kuongelea ukiukwaji wa haki, Tume huru, wafanyakazi kutokupandishwa mishahara, biashara kufa, lugha chafu kwa akina mama... Hawawezi. Sasa wanategeemea wizi wao kupitia Tume, basi.
 
Ndiyo ana kihalibu chama chetu,hivi tumekosa watu wabobozi wa siasa kweli hadi tunaokoteza wanaharakati kama polepole ndiyo apunguze Kura za Ndugu Magufuli?kukaa kote kimya siku Saba ndiyo chama chetu kimemtuma kusema hoja shaifu hivi? Maana polepole ni msemaji wa chama hakujituma mwenye.
 
Hizi siasa za kuchafuana utu kwa mambo ya kipuuzi, kumshushia mwenzako hadhi ya ubinadamu wake na huku ukijua alikotokea ni jambo la kipuuzi na linapaswa kukemewa hadharani.

Hii inanifanya niamini kuwa hukumu za jana ndani ya mahakama ya Kisutu zilikusudiwa kupangwa kisiasa.

Watanzania tunajua kuwa Tundu Lissu hakupenda kwenda kuishi huko Ulaya ambapo mnasema ana uraia. Kilichompeleka huko ni gharama za siasa zetu mufilisi za kuwa tayari kuua pale mnapokuwa hamkubaliani kwa hoja. Hivyo ni lazima tuwe na hofu ya Mungu maana Karma ni kweli!

Kitendo cha Polepole kumpakazia Tundu Lissu ushoga hadharani kwa kweli hakikubaliki. Alienda Ulaya kutibiwa baada ya kuumizwa na wasiopenda ushindani wa kisiasa! Kusema hivyo ni kukosa hoja mbadala za ushindani wa kisiasa na kutapelekea matatizo zaidi.

Nakuona unaongea kwa ukali kuhusu kada wenu aliyeuawa huko Njombe, kama wewe ulivyoumia basi kila mmoja wetu linapomfika tatizo anapata kipimo hicho hicho cha maumivu. Lazima tuheshimu uhai wa kila mmoja wetu! Nchi hii siyo ya bata na kuku! Ni ya watu wenye miili sawa, na kila mmoja wetu linapomfika tatizo huumia kwa kiwango kile kile kilichokuumiza wewe! Tafadhali sana!

Mtaanza kuja na ujinga wa kudhalilisha utu wa watu kwakuwa tu mnataka madaraka. Hilo kamwe halikubaliki. Tufanye siasa za hoja zikitolewa tuhuma zijibiwe bila kudhalilishana kwa kiwango unachopanga kufanya. Hiyo ndiyo maana halisi ya siasa.

Polepole, unakoelekea siko!
Usihangaike na mtu asiye na msimamo , Polepole si size ya Lissu , huyu ni mchumia tumbo aliyeokotwa barabarani na Kikwete

Hebu mwangalie hapa
 
Hizi siasa za kuchafuana utu kwa mambo ya kipuuzi, kumshushia mwenzako hadhi ya ubinadamu wake na huku ukijua alikotokea ni jambo la kipuuzi na linapaswa kukemewa hadharani.

Hii inanifanya niamini kuwa hukumu za jana ndani ya mahakama ya Kisutu zilikusudiwa kupangwa kisiasa.

Watanzania tunajua kuwa Tundu Lissu hakupenda kwenda kuishi huko Ulaya ambapo mnasema ana uraia. Kilichompeleka huko ni gharama za siasa zetu mufilisi za kuwa tayari kuua pale mnapokuwa hamkubaliani kwa hoja. Hivyo ni lazima tuwe na hofu ya Mungu maana Karma ni kweli!

Kitendo cha Polepole kumpakazia Tundu Lissu ushoga hadharani kwa kweli hakikubaliki. Alienda Ulaya kutibiwa baada ya kuumizwa na wasiopenda ushindani wa kisiasa! Kusema hivyo ni kukosa hoja mbadala za ushindani wa kisiasa na kutapelekea matatizo zaidi.

Nakuona unaongea kwa ukali kuhusu kada wenu aliyeuawa huko Njombe, kama wewe ulivyoumia basi kila mmoja wetu linapomfika tatizo anapata kipimo hicho hicho cha maumivu. Lazima tuheshimu uhai wa kila mmoja wetu! Nchi hii siyo ya bata na kuku! Ni ya watu wenye miili sawa, na kila mmoja wetu linapomfika tatizo huumia kwa kiwango kile kile kilichokuumiza wewe! Tafadhali sana!

Mtaanza kuja na ujinga wa kudhalilisha utu wa watu kwakuwa tu mnataka madaraka. Hilo kamwe halikubaliki. Tufanye siasa za hoja zikitolewa tuhuma zijibiwe bila kudhalilishana kwa kiwango unachopanga kufanya. Hiyo ndiyo maana halisi ya siasa.

Polepole, unakoelekea siko!
Siasa majitaka Chadema saccos mnazipenda, ila hamziwezi.
 
Huo muda aliokuwa anaongea upupu, bora TBC 1 wangeweka hata kipindi cha mziki wa zamani na Chacha Maginga.

Yaani siku zote hizo wamekaa ndani wakijadili hoja za kumjibu Lisu, vichwa vyote ndivyo vimemtuma aongee ujinga?

Kwa mwelekeo wa mazungumzo yake, hizo tarehe 7 za mwisho anajiandaa kumtangaza Lisu kama shoga, rejea kauli yake baada ya kusema anasubiri siku saba za mwisho.
Pole pole ni mpinzani mkuu usiumize kichwa.
 
Huo muda aliokuwa anaongea upupu, bora TBC 1 wangeweka hata kipindi cha mziki wa zamani na Chacha Maginga.

Yaani siku zote hizo wamekaa ndani wakijadili hoja za kumjibu Lisu, vichwa vyote ndivyo vimemtuma aongee ujinga?
Pole pole ni mpinzani mkuu usiumize kichwa.
Kashindwa hata kusema Chadema, kaishia kusema chama Cha Mbowe.
 
Back
Top Bottom