NAMBA MOJA AJAYE NCHINI
JF-Expert Member
- Oct 29, 2019
- 8,610
- 17,657
Wanabodi za asubuhi! Leo nakuja na malalamiko ya walimu wa shule za msingi katika Wilaya ya Uyui kumhusu huyu Karugutu.
Wanaanza kwa kueleza kuwa kwenye zoezi la kuboresha daftari la wapiga kura mwaka jana Karugutu aliwalazimisha walimu wa saini hela ya chakula 15,000/= kwa maana ya kifungua kinywa na chakula cha mchana. Walimu hao waliumizwa na kitendo hicho cha kuwapiga hela ya chakula kwenye semina.
Fedha ambayo wangelipwa kwenye semina ilikatwa kwa huduma mbovu ya chakula chenye thamani ya Sh. 4000/= ikafanywa 15000/=. Walimu walilia na kulalamika lakini Karugutu hukusikia.
Tena uliwatisha kuwa watachukuliwa hatua ya kinidhamu wasiposaini. Walimu wamekuwa wakilalamika kwa tabia yako ya kuwakejeli na kuwakemea wakija halmashauri kwa matatizo mbalimbali, umekuwa ukiwatisha na kuwakemea kwa kutaka kuwaandikia barua za kinidhamu wakidai haki zao.
Tatizo kubwa la halmashauri ya Uyui ni rushwa na kubebana hata kutoa vyeo kwa rushwa mbalimbali za fedha na ngono. Ubadhirifu ni mwingi sana hapo wilayani.
Hadi sasa kuna wakuu wa shule wa sekondari wenye elimu ndogo wametoa rushwa ili kuendelea na ukuu huo wakati wengine wakiondolewa kwa ukuu ule ule.
Masijala ya mkurugenzi na elimu za Uyui!, watumishi wake wanaomba rushwa kwa watumishi hasa walimu wanapokuwa na shida mbalimbali hasa kutafutiwa faili zao na kupokea barua za likizo.
Namuomba Seleman Jafo aitazame Uyui (Isikizya hapo ofisini Wilaya ilipo) Aondoe uozo uliopo!!
Watumishi wa umma tena walimu wananyanyaswa sana na watumishi wa Halmashauri hiyo.
Wenye dhamana Chukueni hatua!
Wanaanza kwa kueleza kuwa kwenye zoezi la kuboresha daftari la wapiga kura mwaka jana Karugutu aliwalazimisha walimu wa saini hela ya chakula 15,000/= kwa maana ya kifungua kinywa na chakula cha mchana. Walimu hao waliumizwa na kitendo hicho cha kuwapiga hela ya chakula kwenye semina.
Fedha ambayo wangelipwa kwenye semina ilikatwa kwa huduma mbovu ya chakula chenye thamani ya Sh. 4000/= ikafanywa 15000/=. Walimu walilia na kulalamika lakini Karugutu hukusikia.
Tena uliwatisha kuwa watachukuliwa hatua ya kinidhamu wasiposaini. Walimu wamekuwa wakilalamika kwa tabia yako ya kuwakejeli na kuwakemea wakija halmashauri kwa matatizo mbalimbali, umekuwa ukiwatisha na kuwakemea kwa kutaka kuwaandikia barua za kinidhamu wakidai haki zao.
Tatizo kubwa la halmashauri ya Uyui ni rushwa na kubebana hata kutoa vyeo kwa rushwa mbalimbali za fedha na ngono. Ubadhirifu ni mwingi sana hapo wilayani.
Hadi sasa kuna wakuu wa shule wa sekondari wenye elimu ndogo wametoa rushwa ili kuendelea na ukuu huo wakati wengine wakiondolewa kwa ukuu ule ule.
Masijala ya mkurugenzi na elimu za Uyui!, watumishi wake wanaomba rushwa kwa watumishi hasa walimu wanapokuwa na shida mbalimbali hasa kutafutiwa faili zao na kupokea barua za likizo.
Namuomba Seleman Jafo aitazame Uyui (Isikizya hapo ofisini Wilaya ilipo) Aondoe uozo uliopo!!
Watumishi wa umma tena walimu wananyanyaswa sana na watumishi wa Halmashauri hiyo.
Wenye dhamana Chukueni hatua!