kbm
JF-Expert Member
- Oct 5, 2012
- 5,222
- 1,670
Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, amesema karibu nusu ya watumishi wa Taasisi ya Bunge ni mzigo.
Aliyasema hayo jana wakati akichangia katika semina ya wabunge ya Mfumo Mpya wa Usimamizi na Ufuatiliaji wa Miradi ya maendeleo ili kupata matokeo makubwa sasa.
Lengo la semina hiyo lilikuwa ni kuongeza uelewa kwa wabunge juuya Taasisi ya Rais inayojulikana kwa lugha ya Kiingereza kama Presidential Delivery Bureau (PDB).
"Tatizo kwenye halmashauri kumejaa wazembe, hata hapa (Bunge) tuna karibu nusu ya watumishi mzigo, mtupe namna ya kuwaondoa wazembe," alisema. Ndugai alisema si kwamba watumishi wanaonekana katika Bunge wote ni wazuri.
Alisema suala la uwajibikaji ni dogo nchini na kutaka Tume ya Mipango kutoa njia mbadala ili watumishi waserikali wazembe waweze kuwajibishwa. "Uwajibikaji ni mdogo, tuna watumishi wa kawaida hakuna kazi wanayoifanya, mwalimu wa sekondari unakuta kwa miaka mitano mfululizo anafelisha anaachwa tu, hakuna wa kumuandikia onyo wala kumwajibisha," alisema.
"Kwa kadri tunavyoendelea hivi hatuna namna ya kuchukuliana hatua hatutakwenda popote pale." Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Makamo Rais (Mazingira), Terezya Huviza, alitaka watumishi watakaochaguliwa kuunda PDB, wawe waaminifu wasiopenda kujilimbikizia mali.
Alisema bila kufanywa kwa ukaguzi mzuri kabla ya kuwaweka katika PDB, mfumo huo utakufa.
"Sisi wenyewe (wabunge), tumejichanganya, sisi ndio wafanyabiashara hatutaki kulipa kodi lazima tuchague kitu kimoja kama uongozi ama biashara," alisema.
Mbunge wa Mwibara (CCM), Kangi Lugola, alisema tatizo la kupanda kwa bei ya sukari linaletwa na serikali.
Alisema wenye viwanda wanazalisha kidogo ili wapate vibalivya kuagiza sukari kwa msamaha wa kodi. Mbunge wa Longido (CCM), Lekule Laizer, alisema uzalendo nchini umepotea na kwamba miradi mbalimbali inayotekelezwa imejaa rushwa.
"Rushwa wakati mnaanza utekelezaji hadi mnapomalizia mradi hauna kiwango cha ubora, unakutaka mradi mzima umejaa rushwa," alisema. Alilitaja tatizo jingine ni ukiritimba katika fedha zinazotolewa katika kukuza uchumi almaarufu kama mabilioni ya JK kwamba zimekuwa zikitolewa kwa ukiritimba.
Alitoa mfano wa halmashauri ya Longido ambayo ilipangiwa Sh. milioni 250, ni Sh. milioni 40 tu ambazo zimeshatolewa hadi sasa huku nyingine zikishikiliwa katika mabenki.
Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA), Tundu Lissu, alisikitishwa na mada zote katika semina kuandaliwa kwa lugha ya Kiingereza wakati walio wengi ni wazungumzaji wa lugha ya Kiswahili.
"Mada zote zimeandaliwa kwa lugha ya Kiingereza ni kwa ajili ya mfadhili yupi? Huu ni ugonjwa mkubwa, tatizo ni kuwa ombaomba," alisema. Mbunge wa Ngara (CCM), Deogratius Ntukamazina, alitaka uteuzi wa nafasi mbalimbali za uongozi kuzingatia uwezo wa watu.
"Kama appointment (uteuzi) zetu zitaendelea kuwa na misingi ya udini, urafiki na ukabila, uwajibikaji na kuwajibishana hautawezekana,"alisema. Mbunge wa Muhambwe (NCCR-Mageuzi), Felix Mkosamali, alisema lazima kuwa na watu wenye upeo mkubwa na wenye kujiwekea malengo makubwa.
Alisema iwapo watu kama hao hawapo wajue kabisa ni kupoteza muda kwa kuwa mfumo huo hautafanikiwa. Alihoji taasisi hiyo si ya kwanza na kwamba ipo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imefanikiwa katika mambo gani.
Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Dk. Philip Mpango, alisema kujikosoa na kubadilika kwa kujifunza kutokana na uzoefu wa siku za nyuma au nchi nyingine zilizofanikiwa ni hatua ya unyenyekevu na ya kimaendeleo.
"Vivyo vivyo kukosoa kunakoambatana na mapendekezo ya njia mbadala zinazotekelezeka nikitendo cha uzalendo na muhimu wamaendeleo na ustawi wa Taifa,"alisema hayo wakati akiwasilisha mada yake ya Mfumo Mpya wa Usimamizi na Ufuatiliaji wa Miradi ya Maendeleo ili Kupata Matokeo Makubwa Sasa.
CHANZO: NIPASHE
Aliyasema hayo jana wakati akichangia katika semina ya wabunge ya Mfumo Mpya wa Usimamizi na Ufuatiliaji wa Miradi ya maendeleo ili kupata matokeo makubwa sasa.
Lengo la semina hiyo lilikuwa ni kuongeza uelewa kwa wabunge juuya Taasisi ya Rais inayojulikana kwa lugha ya Kiingereza kama Presidential Delivery Bureau (PDB).
"Tatizo kwenye halmashauri kumejaa wazembe, hata hapa (Bunge) tuna karibu nusu ya watumishi mzigo, mtupe namna ya kuwaondoa wazembe," alisema. Ndugai alisema si kwamba watumishi wanaonekana katika Bunge wote ni wazuri.
Alisema suala la uwajibikaji ni dogo nchini na kutaka Tume ya Mipango kutoa njia mbadala ili watumishi waserikali wazembe waweze kuwajibishwa. "Uwajibikaji ni mdogo, tuna watumishi wa kawaida hakuna kazi wanayoifanya, mwalimu wa sekondari unakuta kwa miaka mitano mfululizo anafelisha anaachwa tu, hakuna wa kumuandikia onyo wala kumwajibisha," alisema.
"Kwa kadri tunavyoendelea hivi hatuna namna ya kuchukuliana hatua hatutakwenda popote pale." Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Makamo Rais (Mazingira), Terezya Huviza, alitaka watumishi watakaochaguliwa kuunda PDB, wawe waaminifu wasiopenda kujilimbikizia mali.
Alisema bila kufanywa kwa ukaguzi mzuri kabla ya kuwaweka katika PDB, mfumo huo utakufa.
"Sisi wenyewe (wabunge), tumejichanganya, sisi ndio wafanyabiashara hatutaki kulipa kodi lazima tuchague kitu kimoja kama uongozi ama biashara," alisema.
Mbunge wa Mwibara (CCM), Kangi Lugola, alisema tatizo la kupanda kwa bei ya sukari linaletwa na serikali.
Alisema wenye viwanda wanazalisha kidogo ili wapate vibalivya kuagiza sukari kwa msamaha wa kodi. Mbunge wa Longido (CCM), Lekule Laizer, alisema uzalendo nchini umepotea na kwamba miradi mbalimbali inayotekelezwa imejaa rushwa.
"Rushwa wakati mnaanza utekelezaji hadi mnapomalizia mradi hauna kiwango cha ubora, unakutaka mradi mzima umejaa rushwa," alisema. Alilitaja tatizo jingine ni ukiritimba katika fedha zinazotolewa katika kukuza uchumi almaarufu kama mabilioni ya JK kwamba zimekuwa zikitolewa kwa ukiritimba.
Alitoa mfano wa halmashauri ya Longido ambayo ilipangiwa Sh. milioni 250, ni Sh. milioni 40 tu ambazo zimeshatolewa hadi sasa huku nyingine zikishikiliwa katika mabenki.
Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA), Tundu Lissu, alisikitishwa na mada zote katika semina kuandaliwa kwa lugha ya Kiingereza wakati walio wengi ni wazungumzaji wa lugha ya Kiswahili.
"Mada zote zimeandaliwa kwa lugha ya Kiingereza ni kwa ajili ya mfadhili yupi? Huu ni ugonjwa mkubwa, tatizo ni kuwa ombaomba," alisema. Mbunge wa Ngara (CCM), Deogratius Ntukamazina, alitaka uteuzi wa nafasi mbalimbali za uongozi kuzingatia uwezo wa watu.
"Kama appointment (uteuzi) zetu zitaendelea kuwa na misingi ya udini, urafiki na ukabila, uwajibikaji na kuwajibishana hautawezekana,"alisema. Mbunge wa Muhambwe (NCCR-Mageuzi), Felix Mkosamali, alisema lazima kuwa na watu wenye upeo mkubwa na wenye kujiwekea malengo makubwa.
Alisema iwapo watu kama hao hawapo wajue kabisa ni kupoteza muda kwa kuwa mfumo huo hautafanikiwa. Alihoji taasisi hiyo si ya kwanza na kwamba ipo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imefanikiwa katika mambo gani.
Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Dk. Philip Mpango, alisema kujikosoa na kubadilika kwa kujifunza kutokana na uzoefu wa siku za nyuma au nchi nyingine zilizofanikiwa ni hatua ya unyenyekevu na ya kimaendeleo.
"Vivyo vivyo kukosoa kunakoambatana na mapendekezo ya njia mbadala zinazotekelezeka nikitendo cha uzalendo na muhimu wamaendeleo na ustawi wa Taifa,"alisema hayo wakati akiwasilisha mada yake ya Mfumo Mpya wa Usimamizi na Ufuatiliaji wa Miradi ya Maendeleo ili Kupata Matokeo Makubwa Sasa.
CHANZO: NIPASHE