Ndugai alipompiga mkwara Halima Mdee Bungeni Leo

Ndugai alipompiga mkwara Halima Mdee Bungeni Leo

MTAZAMO,Siasa ni mchezo na mnapokuwa wengi ni advantage. Naamini wabunge wa ccm na spika/naibu spika hawajatumwa na wananchi hayo wanayoyafanya. Maadamu tunaona, tuchukue hatua. Cdm kwa uchache wao hawana la kufanya zaidi ya kuwashitaki kwetu na hasa kwa wale ambao hawakuona au hawakuelewa kilichotokea ili maamuzi yetu yazingatie mambo hayo. Tuwahukumu hao wanaowadhalilisha viongozi tuliowachagua maana wanatudhalilisha hata sisi kwa manufaa ya chama chao badala ya wananchi waliowapigia kura!
Nimekupata mkuu lakini hii ni vita na ushindi ndani na nje ya bunge ni muhimu sana.binafsi bado naona ccm wanatumia mbinu dhaifu kuzima hoja nyingi ila cdm haijajipanga kulazimisha hoja za msingi zipewe majibu na wahusika hata kama ni majibu mabovu na si kuzimwa na spika.yule mama spika mwanzo alikuwa anawaogopa waziwazi wabunge wa cdm hadi hofu yake ulikuwa unaweza kuisoma usoni kwake lakini sasa hv anajiamini haswa hata akivurunda!tukumbuke majimbo ya wapinzani hayatapewa kipaumbele kupewa miradi na fedha za kutosha na huku mtaani wananchi wameanza kusema tumechagua upinzani mbona mambo yale yale hakuna hata nukta ya mabadiliko? Lazima tulazimishe kufanyiwa kazi hoja za wabunge wetu na waheshimiwe lakini nao wajipange ili waweze kutimiza malengo yote kwa ufasaha lakini haswa wasigeuzwe walalamikaji tu alafu mwisho kuja kulalamika mitaani bila juhudi za makusudi bungeni.tunataka moto mkubwa zaidi ya huu bungeni maana yapo mengi sana yanayoangamiza taifa.
 
Hao ni panya ambao wanamdhihaki paka kwa sababu wako karibu na shimo (wamekalia viti vya enzi) nje ya viti hivyo watanyakuliwa kwa supersonic speed na paka. Time will tell, tumhurumie kwani taaluma yake ni kushirikiana na wanyama pori he lacks soft skills.
 
leo nina kupuuza duh, ina maana halima mpuuzi?
yeye kama naibu spika anaposema wanaopinga ni wanafiki ina maana hajui hao hao anao waita wanafiki ni kina nani?
ina kuwaje hivyo vipaza sauti lakini kila mtu anaweza kuongea tu anavyotaka bila kuchukuliwa hatua.
hivi ili suhala la posho kwa nini wana ccm wanaita wabunge wa chadema majina ya kijinga?
kama wanataka kujua msimamo wa wananchi wafanye POLL moja kwa wananchi wapate message wananchi wako upande gani, kama hawajakuta na sisi wananchi wanatuita wanafiki ya kwamba walikuwa wanalipwa toka zamani na sasa tunapingwa kwa nini hatukupinga zamani?

dunia ni mabadiliko mbona na wao wanatumia pc leo na wasibaki na mambo ya zamani?
sasa ni wakati wa mabadiliko ndio maana mambo yanaibuka na ccm wanapaswa kuheshimu hilo
Kwa ninavyo jua kiswahili, Anayepuuza ndiye MPUUZI, kama ilivyo kwa anayejenga ni mjenzi na hapa aliye puuza ni naibu spika. Hao anaowaita wanafiki ni wananchi ambao hoja zao zimewakilishwa na wabiunge wao. Upungufu wa naibu spika ni kuiona hoja kuwa ni ya mbunge kama mtu binafsi na siyo ya wananchi anaowawakilisha. hata hivyo hayo yana mwisho na yatakuja kumtokea puani siku moja.
 
Ndugai ni Kilaza tena sana Maana ameshindwa kukemea Sauti za Mipasho yaani amemu attack Halima Personally
 
Hivi ni mimi sielewi kuhusu hii BIMA ya afya. kwa uelewa wangu BIMA ya afya inakatwa au kutolewa kwenye mshahara. Sasa kwa nini wabunge hiyo BIMA yao ishughulikiwe na bunge?

Alafu sijaelewa

  • msistizo wa ndugai anapotaja safari za nje ya nchi za wabunge kama ndo kigezo cha kuwa na bima ya afya.
  • Ndugai anapotumia maneno kama ".....leo unapiga kelele mambo ya posho......" au ".....kwa leo Nakuupuza......." , Hivi ni kikao official au wako pub
  • Kutokuwa mbunge kipindi fulani inamuondolea mbunge haki ya kushauri au kuhoji mambo fulani. Nimesikia ndugai akisem "......Mambo haya yalipitishwa kikao cha bunge la tisa na bahati nzuri mhh mbunge hakuwepo.........."
  • Na katika hoja na majibu anasema kama wanadaoi mambo ya posho wako serious basi warudishe posho za tangia mwanzo. Mbona serikali ikifuta kodi fulani hairudishi pesa ilizokusanya kutokana na odi hiyo.
Kweli CCM ni Janga la taifaa. Ndugai kanyesha dharau ya hali ya juu kwa mbunge na wananchi. kauli zake zinazalilisha wabunge uliko ile ya wivu wa kike

CDM should make a move ndugai avuliwe cheo chake. Matamshi yake na hiyo positin haviendani. Otherwise ombe msamaha wanchi na halima mdee. Badala ya kufanya kazi ya kiti ameoeyshayuko kichama zaidi.
 
Nilikuwa nafuatilia Bunge na nikakuta sehemu ambayo walikuwa wanazungumzia suala la Bima za Wabunge - wakijadili kauli ya Kafulila kuwa Wabunge ni "privileged class" kuwa wanapata huduma ya afya wao na watoto wao. Ndugai alipokuwa akijaribu kutoa ufafanuzi alidokeza kitu kuwa wabunge hawana bima ya afya na Bungeni linawafanyia utaratibu. Akatumia muda pia kurusha vidonge vya mwisho na kama utakavyosikia Halima Mdee akataka kupata "taarifa"... well listen .

View attachment 33772
Hata mimi nilisikitika sana namna Naibu spika alivyofanya uharaka na kutumia nguvu sana katika kutisha kwa kutumia kitabu cha kanuni za Bunge kuzima hoja za Bi Halima. na vile vile kulikuwa na mipasho ya chini chini ndani ya bunge.
 
mimi sijasikitika, nimefurahi kwakuwa wananchi wanazidi kupata uelewa dhidi ya serikali yao, faida ya kauli ile ya ndugai itaonekana 2015
 
Kweli hizi ni akili za wabunge wa CCM. Upumbavu mtupu kuanzia kwa kiongozi (sijui spika) mwenyewe. Unatetea posho.... what a hell is this. Kwa kuwa zamani wapinzani walikuwa wanachukua posho, na imebainika kuwa ni wizi.... kwa kuwa hawawezi kurudisha basi hili linahalalisha wizi. @"""f$/=@n CCM
 
Kati ya watu wachache waliobakia ndani ya ccm niliokuwa bado nawaheshimu ni pamoja na huyu Agwe Ndugai Job. Bahati nzuri namfahamu huyu bwana kwani tulisoma naye Old Moshi. Alionyesha uwezo wa uongozi tangu enzi zile.

Ndiyo maana alipopata ubunge na sasa U-Naibu spika mimi sikushangaa. Lakini kwa jinsi alivyopeleka mambo jana: tukianzia na hoja ya Mch Mh Msigwa kuomba mwongozo, yaani badala ya kutoa mwongozo akarudia makosa yale yale ya Sitta kuwaita wapinzani eti Wanafiki. Hiki kibri kakitoa wapi Job Mbaruka??

Tukirudi kwenye issue ya Mh Mdee, alitumia ubabe wa hali ya juu, anamtisha Mh mbunge mwenzake anaruhusu wabunge kuropoka ovyo bila utaratibu. Alimtisha kwa kushika kile kitabu, sijui ndicho chenye kanuni, anamwambia asicheze na kiti, sijui anaweza kufanya maamuzi ambayo wapiga kura wake hawatamuelewa, na maneno ya namna hiyo.

Kwa kifupi Job kubali "mate" wangu uliteleza. Ingawa mtu mzima huona aibu kusema samahani (na hasa kwa mwanamke), naomba uwe wa kwanza kumwomba samahani mbunge mwenzako wa Kawe - Halima Mdee.

Vinginevyo sisi wapiga kura wako hatukuelewi. Au ni kaulevi fulani mnako wabunge wa ccm?? Au mnadhani 2015 ni mbali sana?? Au hapatakuwa na maisha tena baaba ya hili bunge?? Au mnadhani mtaendelea kuishi humo mjengoni baada ya mwezi wa 9??

Kama majibu ya maswali yangu hapo juu ni SIYO mnategemea tuangaliane vipi huku uraiani na hasa utakapofika ule msimu wa kuomba kura kurudi Mjengoni?? Kwa sababu naamini kabisa hata wewe Job bado unahitaji kurudi mjengoni 2015, au imetosha??

Na kwa ninavyokuona unakinyemelea kiti cha Makinda, kama sivyo kataa na ukanushe.

Mimi niseme tu kwamba CCM wanajimaliza wenyewe, yatakayotokea 2015 wala wasitafute mchawi, watajifanya kusahau lakini sisi waathirika wa wanayoyasema na kuyatenda sasa hivi tutawakumbusha, kwani waswahili walisema" Mla ndizi husahau lakini mtupa maganda hasahau kamwe".
 
mamamaa weeeee!!!!! Kumbe kwa sasa bunge lishakua sehemu ya mipasho kama lango la jiji??
Jamani huo utengenezaji wa katiba mpya unaanza lini?? Kuna mambo ningependa na kufurahia kuyaona yakitimia kabla sijafa.

Hizo posho na mishahara wanayolipwa kutoka kwenye hela za walipa kodi ndo wanazitumia kuimbia mipasho bungeni!!!

Na sisi watanzania jamani tubadilike tusisubiri mpaka wapinzani waje watuambie tuandamane!!!
Jambo kama hili wangetakiwa kesho yake wabunge watukute pale nje ya bunge na mabango yetu yakisema ndugai kazalilisha wabunge na wananchi kwa ujumla ajiuzulu.......na si lazima tuwe wengi hata wananchi 100 tu inatosha kufikisha ujumbe.
Ndugu zangu hii kauli imenipa haisra sana nitazilipizia kwa nani!!
 
Tukirudi kwenye issue ya Mh Mdee, alitumia ubabe wa hali ya juu, anamtisha Mh mbunge mwenzake anaruhusu wabunge kuropoka ovyo bila utaratibu. Alimtisha kwa kushika kile kitabu, sijui ndicho chenye kanuni, anamwambia asicheze na kiti, sijui anaweza kufanya maamuzi ambayo wapiga kura wake hawatamuelewa, na maneno ya namna hiyo.

Kwa wanaofuatilia Bunge hili, mtakubaliana nami kuwa Mh. Halima Mdee amekuwa na mtindo wa kuingilia mijadala kwa namna ambayo ni 'provocative' kiasi kwamba hata wanaomtazama huwa wanabaki wakijiuliza? Hii imetokea mara nyingi na mara zote huishia kubishana na Spika au Mwenyekiti kwa lugha ambayo; kwa maoni yangu, haimjengei taswira nzuri mbele ya wapigakura wake.
 
Mheshimiwa Sitta nilikua namheshimu sana kwa sababu umri wake ni sawa na Babu yangu lakini kutokana na kujidhalilisha kwake jana Bungeni kuwaita wabunge wenzie waliochaguliwa na wananchi kua ni Wanafiki na mimi sina Budi kumuita yeye ni Ms%**&Nge. anatetea nini wakati ukienda Jimbo la Urambo lina dhiki kama nini?
Huyu Naibu spika ndo kilaza kweli ile hoja ya mbunge wangu mpendwa Mch Msigwa ilitakiwa aijibu kama kweli ni halali kuwaita wenzio wanafiki au sio halali? yeye akaenda moja kwa moja kwenye mipasho. Wananchi wa Iringa tumekasirishwa sana na usikanyage Iringa kwenye Ngome ya mkwawa kitakachokupata utajutia maisha yako yote
 
mimi sijasikitika, nimefurahi kwakuwa wananchi wanazidi kupata uelewa dhidi ya serikali yao, faida ya kauli ile ya ndugai itaonekana 2015
Zumbe, 2015 ni mbali sana kusubiri katika hali hii. Hatua lazima zichukuliwe mapema. Naanza kupata mantiki ya yule mbunge aliyesema "Tufunge mlango zipigwe"
Wakati mwingine heshima haipatikani kwa kuiomba, bali kuipigania. Hata mnyonge unayemwonea kwa kumtwanga ngumi akiamua kila ukipita anakutungua kwa mawe utaacha kumwonea.
Wananchi ndio wanaotakiwa kukasirika na udhalilishaji kama huu na kuchukua hatua sio kuwaachia wabunge wa upinzani pekee.
 
Baada ya kusikiliza hiyo clip, nimeamini kuwa wabunge wa ccm, hasa msemaji hayupo pale kwa manufaa ya Watanzania. Kweli hawa wabunge ni 'manyang'au'.
 
TBC haikumuønyesha Mdee alichofanya mpaka Ndugai alipotamka maneno hayo kuwa anampuuza.
 
Mkuu nahisi wabunge wetu wa cdm kama wameishiwa mbinu za kupambana na mbinu za ccm kuzima hoja nyingi mle ndani.hoja nyingi kuzimwa ni ushindi kwa ccm hasa tukiangalia namna wananchi wengi wakiwa bado hawajakomaa na elimu ya democrasia na uwajibikaji wa viongozi.siku zinakwenda na hoja zinazimwa kwa mbinu zile zile huku wabunge wetu wakionekana kama walalamikaji tu bila hatua zozote.cdm tunapaswa kuwa wamoja mle ndani kiitikadi na ki mbinu.inabidi utumike mtindo wa kijeshi wa collective responsibility kulazimisha kusikilizwa na kufanyiwa kazi hoja zao.wabunge wanadhalilishwa mno kama kuambiwa kaa chini! Nakupuuza na kukamatwa kama vibaka tena kwa kejeli!binafsi sitaki kumlaumu spika wala wabunge wa ccm maana wanafanya kazi waliyotumwa! Lakini wabunge wa cdm wanakabiliana vp na uhuni huu? Uhuni umezidi bungeni hakuna hatua na matamko yametuchosha inabidi kutumia sheria zilizopo na za kimataifa kulazimisha demokrasia kuchukua nafasi.tusiwalaumu ccm wanafanya waliyotumwa,cdm wanafanya nini mle kabla hawajarudi kwetu mitaani?

Bunge la Makinda likiisha, CHADEMA wazindue bunge la mtaani (mikutano ya hadhara) waanze kupitia bajeti nzima na kueleza wananchi madudu yote ya serikali, wakumbushe mapendekezo/mawazo mbadala waliyotoa bungeni na namna yalivyokataliwa na 'wabunge wa ccm'. Wasikae kimya CHADEMA leteni hoja zenu zooooote huku mtaani maana sisi wananchi ndio tumewatuma wabunge wote DODOMA, na huku mtaani wananchi ni wengi milioni 40 na ushee.
 
Kwa ninavyo jua kiswahili, Anayepuuza ndiye MPUUZI, kama ilivyo kwa anayejenga ni mjenzi na hapa aliye puuza ni naibu spika. Hao anaowaita wanafiki ni wananchi ambao hoja zao zimewakilishwa na wabiunge wao. Upungufu wa naibu spika ni kuiona hoja kuwa ni ya mbunge kama mtu binafsi na siyo ya wananchi anaowawakilisha. hata hivyo hayo yana mwisho na yatakuja kumtokea puani siku moja.

duh yeah kweli sikuiangalia kiivyo,
nimekupata kabisa kwa maana hiyo tuna naibu spika mpuuzi
 
Ndugai ni zuzu,juha na ***** mkubwa.

Huu UNAFIKI uliozungumzwa na Sitta na Ndugai kuhusu wabunge wa UPINZANI kukataa sitting allowance hauna mashiko hata kidogo!!!!!!
Kuhusu kuondoa au kupunguza Posho hasa sitting ALLOWANCE serikali ya CCM wenyewe wamesema NI MPANGO ambao upo kwenye programu yao ya miaka 5 ijayo!!!

Sasa tuwaulize Sitta na Ndugai wao wamesharudisha hizo posho za Bunge lililopita kwasababu swala la Posho liko kwenye programu yao ya Chama?CCM ndiyo wanafiki wakubwa na hasa Sitta ambaye kwa sasa amekuwa ni kigeugeu hasa baada ya kunyang'anywa USPIKA kwa visingizio vya KINAFIKI vya wana-CCM kwamba ati walitaka Spika MWANAMKE-Makinda wakti huohuo SS akiwa naye amechukua fomu.

SItta anatakiwa aeleze UNAFIKI wake wa kuanzisha chama cha CCJ ndani ya chama cha CCM. Huo ndio unafiki mkubwa kabisa wa SS. KITENDO CHA WAPINZANI KUKATAA POSHO ZA SITTING ALLOWANCE NI UZALENDO NA UKOMAVU WA KISIASA WAKTI KITENDO CHA KUANZISHA CCJ NDANI YA CCM NDIYO UNAFIKI NA UHAINI ndani ya CCM NA SERIKALI YAKE.
 
Kwanza nikushukuru sana MM kwa kutu-keep us posted kwani watu wengine hatukubahatika kufuatilia shughuli za Bunge kutokana mgao wa umeme. Jamani hoja ya CHADEMA si kurudisha posho bali kufuta posho za vikao (sitting allowance) katika mfumo wetu wa malipo. Na muongozo ulioombwa ni kuhusu kauli iliyotolewa na Sitta ya kuwaita Wabunge wa upinzani WANAFIKI.

Sasa muongozo unaotolewa ni mwingine kabis! wala haiitaji kwenda shule kujua kuwa Mh. Ndugai hakuwa IMPARTIAL kabisa, yaan warudishe posho!? Ndugai Vipi tena? Toa muongozo unaostahili. Vice President wa Tanzania Visiwani ameshasema hii ni HOJA YA MSINGI na inapaswa kupatiwa majibu ya MSINGI, sasa hizi kebehi zinatoka wapi? Na huyu Sitta sasa ameanza kulewa madaraka, binafsi nilikuwa ninamtunzia heshima sana, but kauli zake zimeanza kunipa wasiwasi


Yani huyu NDUNGAI namchukia kupita maelezo, anajiona yeye ndio yeye na anaona Tanzania nzima hakuna anejua sheria kama yeye.Huwa ana ubabe sana kwa wapinzani na ushabiki wa wazi wazi na usiokuwa na maana kwa CCM.Yani ni afadhali makinda kuliko huyu kibaraka anaejiskia na kujiona ni mbabe.Kuna siku huko mitaani watampiga mawe
 
Back
Top Bottom