Ndoa zenye Utata..

MwanajamiiOne

Platinum Member
Jul 24, 2008
10,470
6,563
Salamu ndugu zanguni.... jamani naomba nisaidieni, je kuna ndoa kweli hapa iwapo................

1. Pesa za mume hazieleweki zinapokwenda na ukiuliza ni ugomvi ila za mke anataka ajue ametumiaje na anataka mshahara ukitoka tu basi akabidhiwe na yeye ndie awe anayepanga matumizi. Na mke haruhusiwa kununua hata handkerchief ataambiwa yuko extravagant ila mume anauwezo wa kutumia laki tano au sita within a week ikaisha na asiulizwe matumizi.

2. Mke hatakiwi kusaidia ndugu zake na akiomba pesa kwa ajili ya ndugu zake (mke) basi mume hukasirika hadi mke anajuta...

3. Mume siku zote yuko negative about chochote anachokifanya mkewe ingawaje pesa zikipatikana yeye ndie wa kwanza kuzidai

4. Kila siku mume anatafuta makosa kwa mkewe hata kama ni kwenda na kufukua ya nyuma kabla hawajaoana

5. Mume anapenda aabudiwa hata na wakwe zake. kwake yeye wakwe zake si kama wazazi bali watumwa ambao wanastahili kumnyenyekea yeye.

Kwa upande wangu mimi nahisi kama huyu mume anamtumia tu huyu mdada na hana mapenzi ya kweli nae hivyo si ajabu akamwaga huko mbeleni mambo yake yakishakuwa mazuri....

Nini mtazamo wako katika ndoa za aina hii?
 
hii ndoa imetawaliwa na uoga kwa mwanamke, kwanini mwanaume kipato chake kisikihusu chako kimuhusu? jamai kila leo wanaambiaga wadada wenzangu mwanaume ni siku ya kwanza umuonyeshe wewe ni wa aina gani otherwic ndio kama hivi unakuja kutesekea ndoa, angekuwa mkali kidogo kwake tangu siku ya kwanza ya hiyo tabia atleast kungekuwa na changes kidogo kwasasa ni too late, mimi wa hivyo kila mtu aqshike lake.
 
Dada nyamayao this is what I thought as a wise decision. Kwa kweli sometimes huwa nashindwa kuelewa yaani the man anakuwa kama vile mkoloni and yet anajidai anampenda sana mkewe... yaani anazo loose ends kibao ambazo hazieleweki namkewe mara nyingi huwa hapendi kumfukunyuafukunyua mumewe akiamini kuwa anampatia space - mume hataki simu yake iguswe na wala aulizwe uko wapi kama akipifga simu but yeye simu ya mkewe ni yake na asikute namba ya mtu asiyemfahamu basi atampigia na kuanza kumwuliza kwa hasira-- its very sad.
 
Dada nyamayao this is what I thought as a wise decision. Kwa kweli sometimes huwa nashindwa kuelewa yaani the man anakuwa kama vile mkoloni and yet anajidai anampenda sana mkewe... yaani anazo loose ends kibao ambazo hazieleweki namkewe mara nyingi huwa hapendi kumfukunyuafukunyua mumewe akiamini kuwa anampatia space - mume hataki simu yake iguswe na wala aulizwe uko wapi kama akipifga simu but yeye simu ya mkewe ni yake na asikute namba ya mtu asiyemfahamu basi atampigia na kuanza kumwuliza kwa hasira-- its very sad.



yani umpatie mtu space wakati yeye kakufuga funga kila idara? ujinga mtupu, uwoga wake tu, anahofu akijitetea ndoa itakufa kibudu! mbaya sana.
 
Mwanamke analipa gharama za kumg'ang'ania mwanamume na kumfanya ndiye Mungu wake hapa duniani. Kama angekuwa hana kazi na kwa hiyo hana kipato angalau ningemsamehe. Ila kwa haya anayovumilia sina shaka ni mjinga tu. Hata hivyo hajachelewa. Kama angepata mtu wa kumpa usahauri mzuri basi angemwambia aamue kuachana na huyo mume wake angalau kwa miezi 2-3 ili mwanamume aweze kupata nafasi ya kuichanganua vizuri thamani ya mke wake. Lakini kwa kuendelea kuufyata mkia kwa kila jambo analofanyiwa kama mbwa koko, atakuja kuchofolewa hata koromeo (ukizingatia kuwa hata ndugu wa mwanamke ni kama nyau mbele ya mwanamume). Amemruhusu amchezee anavyotaka kama doli lake. Kwa hiyo akimua kulichoma moto hakuna maneno!!! After all, to him (the husband) she is just a toy and sex object, let him use it to the maximum!!
 
We mwana J 1, Hii aina ya ndoa uliyoileta hapa ni ya jirani yako, or ndugu yako or ya kwako? If you don't mind liweke wazi hili, ili tuweze kuichangia vizuri!

Cheers
NL
 
Hii ndoa utadhani ni hadithi ya kubuni kumbe kweli. Mimi ushauri wangu kwa huyu Dada awe jasiri aache kumpa pesa huyo mumewe.
 
Salamu ndugu zanguni.... jamani naomba nisaidieni, je kuna ndoa kweli hapa iwapo................

1. Pesa za mume hazieleweki zinapokwenda na ukiuliza ni ugomvi ila za mke anataka ajue ametumiaje na anataka mshahara ukitoka tu basi akabidhiwe na yeye ndie awe anayepanga matumizi. Na mke haruhusiwa kununua hata handkerchief ataambiwa yuko extravagant ila mume anauwezo wa kutumia laki tano au sita within a week ikaisha na asiulizwe matumizi.

2. Mke hatakiwi kusaidia ndugu zake na akiomba pesa kwa ajili ya ndugu zake (mke) basi mume hukasirika hadi mke anajuta...

3. Mume siku zote yuko negative about chochote anachokifanya mkewe ingawaje pesa zikipatikana yeye ndie wa kwanza kuzidai

4. Kila siku mume anatafuta makosa kwa mkewe hata kama ni kwenda na kufukua ya nyuma kabla hawajaoana

5. Mume anapenda aabudiwa hata na wakwe zake. kwake yeye wakwe zake si kama wazazi bali watumwa ambao wanastahili kumnyenyekea yeye.

Kwa upande wangu mimi nahisi kama huyu mume anamtumia tu huyu mdada na hana mapenzi ya kweli nae hivyo si ajabu akamwaga huko mbeleni mambo yake yakishakuwa mazuri....

Nini mtazamo wako katika ndoa za aina hii?

...Mke anaonewa na mumewe.


je kuna ndoa kweli hapa iwapo................

1. Pesa za mke hazieleweki zinapokwenda na ukiuliza ni ugomvi ila za mume anataka ajue ametumiaje na anataka mshahara ukitoka tu basi akabidhiwe na yeye ndie awe anayepanga matumizi. Na mume haruhusiwa kununua hata handkerchief ataambiwa yuko extravagant ila mke anauwezo wa kutumia laki tano au sita within a week ikaisha na asiulizwe matumizi.

2. Mume hatakiwi kusaidia ndugu zake na akiomba pesa kwa ajili ya ndugu zake (mume) basi mke hukasirika hadi Mume anajuta...

3. Mke siku zote yuko negative about chochote anachokifanya Mumewe ingawaje pesa zikipatikana yeye ndie wa kwanza kuzidai

4. Kila siku Mke anatafuta makosa kwa Mumewe hata kama ni kwenda na kufukua ya nyuma kabla hawajaoana

5. Mke anapenda aabudiwa hata na wakwe zake. kwake yeye wakwe zake si kama wazazi bali watumwa ambao wanastahili kumnyenyekea yeye.

Nini mtazamo wako katika ndoa za aina hii?

...Mume anampenda sana Mkewe!


...yote inategemeana na bilauri unaiangaliaje, ...maji yamejaa nusu, au yamepungua nusu!
 
Hii ndoa utadhani ni hadithi ya kubuni kumbe kweli. Mimi ushauri wangu kwa huyu Dada awe jasiri aache kumpa pesa huyo mumewe.

Sawa ataacha kumpa pesa je unadhani hii itakuwa suluhisho au ndo itamfungua kifungoni? Maana the way it seems ni kuwa bwana hana mapenzi ya kweli kwa mkewe otherwise asingekuwa anakasirikakasirika hata kwa sababu za kuchekesha- eti housegirl kaitwa hajaitika (bila kujua kama amesikia au la) tayari basi kosa ni la mke!!

Mimi nadhani hapa mapeenzi yameelemea upande mmoja tu kwa mke masikini
 


...Mke anaonewa na mumewe.




...Mume anampenda sana Mkewe!


...yote inategemeana na bilauri unaiangaliaje, ...maji yamejaa nusu, au yamepungua nusu!


Nimekupata mkuu hili nalo jambo ila kwa kusema kweli kwa tafsiri ya kweli hii snerio B ni kuwa Mke ni mwonevu kwa mume na mume hatakiwi (kama ilivyo kwa mke) kukubaliana na hali hii. Wote ni binadamu ambao tuna haki ya kuishi kwa furaha katika muda tuliopewa na mwenyezi MUNGU kwa nini umnyanyase mwenzio kisa umemuoa/amekuoa?.. Huoni dhambi?
 
Namshauri huyo dada aamke huu sio wakati wa kulala na wala hajachelewa. Aongee na mume amueleze anavyofanya sio vizuri. Akiendelea kuwa goigoi ataishia kuumia wakati mwenzake wala hamjali.

Je wana watoto?
 
matatizo mengine tunaayanza sisi wenyewe mara tu mnapooana ile biashara ya kujitia mmekua kitu kimoja so you share nearly everything. baadae ndoa ikianza kuchujuka sasa unaanza kuona tabu wakati ulikubali mwenyewe wakati ndoa changa. niulize swali, hii biashara ya kumpa mwanamme mshahara ilianzaje? maana hapa sielewi, kazi nifanye mimi, mshahara nimpe bwana, hainiingii akilini.
huyu mwanamme ni kabila gani, kama ni kutoka musoma nitaelewa, kama ni kutoka maeneo mengine ya bongo nitajiuliza tena katoa wapi hii tabia.
sioni kwa nini ufanye wewe kazi, ushindwe kumsaidia hata mama au baba yako kwa sababu you have to ask from your hubby for your salary... wake up!
 
Sal
Kwa kweli sijui how it come to that but naamini ni mojawapo ya stupid things tunazozifanya pale mapenzi yanapokuwa kileleni/moto. How alikubali kuwa anampa mume mshahara yeye na mumewe ndio wanaojua ila nataka kuuliza kwani kuna ubaya mtu kufanya vitu pamoja? unless from the beginning muwe na shaka juu ya ndoa si wanadai mkishaoana huwa kila kitu ni cha wote? .. (mimi sijui coz I dont have experience ya ndoa as I am not married).

kama ni ndio why utumie upendo wa mwenzio kumwadhibu kwa sababu naamini kama ni yeye mwenyewe aliamua kumkabidhi mume mshahara ni wazi kuwa alifanya hivyo kwa mapenzi kitu ambacho sasa naona kinamtokea puani.

Ni kweli haiingii akilini eti kazi ufanye wewe afu mshahara atumie yeye.... kwa kweli ni pagumu
 
Namshauri huyo dada aamke huu sio wakati wa kulala na wala hajachelewa. Aongee na mume amueleze anavyofanya sio vizuri. Akiendelea kuwa goigoi ataishia kuumia wakati mwenzake wala hamjali.

Je wana watoto?

gnasha aksante kwa ushauri wako... ni kweli katika ndoa yao wamebarikiwa watoto mapacha wa kiume wenye unmri wa mwaka mmoja sasa.
 
Sawa ataacha kumpa pesa je unadhani hii itakuwa suluhisho au ndo itamfungua kifungoni? Maana the way it seems ni kuwa bwana hana mapenzi ya kweli kwa mkewe otherwise asingekuwa anakasirikakasirika hata kwa sababu za kuchekesha- eti housegirl kaitwa hajaitika (bila kujua kama amesikia au la) tayari basi kosa ni la mke!!

Mimi nadhani hapa mapeenzi yameelemea upande mmoja tu kwa mke masikini

sijajua unatafsiri vp neno mapenzi, kwangu mimi naona kuwa mume ndiye anayempenda zaidi Mke ndio maana anampelekesha puta katika kila jambo na hampi nafasi ya kutumia hela vibaya wala kutumia nje ya familia yao na kupeleka kwa ndugu zake. huyu mume anampenda sana mkewe ndio ajili yuko naye hadi sasa.
 
Salamu ndugu zanguni.... jamani naomba nisaidieni, je kuna ndoa kweli hapa iwapo................

1. Pesa za mume hazieleweki zinapokwenda na ukiuliza ni ugomvi ila za mke anataka ajue ametumiaje na anataka mshahara ukitoka tu basi akabidhiwe na yeye ndie awe anayepanga matumizi. Na mke haruhusiwa kununua hata handkerchief ataambiwa yuko extravagant ila mume anauwezo wa kutumia laki tano au sita within a week ikaisha na asiulizwe matumizi.
2. Mke hatakiwi kusaidia ndugu zake na akiomba pesa kwa ajili ya ndugu zake (mke) basi mume hukasirika hadi mke anajuta...

3. Mume siku zote yuko negative about chochote anachokifanya mkewe ingawaje pesa zikipatikana yeye ndie wa kwanza kuzidai

4. Kila siku mume anatafuta makosa kwa mkewe hata kama ni kwenda na kufukua ya nyuma kabla hawajaoana

5. Mume anapenda aabudiwa hata na wakwe zake. kwake yeye wakwe zake si kama wazazi bali watumwa ambao wanastahili kumnyenyekea yeye.
Nasikia Guantanamo inafungwa, kumbe ziko nyingine? Tobah!
 
mimi nikifika nyumbani mshahara wote anapokea mke wangu na bajeti nzima anafanya yeye, na hata nikitaka hela za kutuma kwetu inanibidi kumuomba yeye, huo ni mfumo tu wa maisha. Mama yangu aliwahi kulalamika ati yeye akitaka hela hata ya kununua soda lazima mke wangu ajue kwanini, nilichomwambia huo ni mfumo wetu wa maisha.
Hivyo sioni sababu ya mtu mwingine kumzungumzia huyu Dada ati anateseka wakati huo ni mfumo wao wameamua wao kuishi hivyo.
 
mimi nikifika nyumbani mshahara wote anapokea mke wangu na bajeti nzima anafanya yeye, na hata nikitaka hela za kutuma kwetu inanibidi kumuomba yeye, huo ni mfumo tu wa maisha. Mama yangu aliwahi kulalamika ati yeye akitaka hela hata ya kununua soda lazima mke wangu ajue kwanini, nilichomwambia huo ni mfumo wetu wa maisha.
Hivyo sioni sababu ya mtu mwingine kumzungumzia huyu Dada ati anateseka wakati huo ni mfumo wao wameamua wao kuishi hivyo.

Mahmoud aksante kwa ushauri wako ila sidhani kama kuna sehemu yoyote ambayo nimesema huo ni utaratibu wao waliojiwekea wenyewe.. sijui ila nafikiri ingekuwa ni utaratibu wao sidhani kama angekuwa analalamika na kutaka ushauri kwa watu nje ya familia. inawezekana ukweli akaujua yeye mwenyewe ila mimi nimewakilisha kile nilichokiona kwa macho- face value of the story.

Aksante tena kwa mtazamo wako.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom