george aloyce
JF-Expert Member
- Aug 22, 2017
- 1,177
- 1,825
SABABU 7 ZA NDOA NYINGI KUF*A KABLA YA KUFIKISHA MIAKA MIWILI!
Nimeongea na watu wengi sana kuhusu ndoa, nimesikiliza sababu nyingi za watu kuachana siku hizi ndoa nyingi hazivuki miaka 3, unasikia flani aliolewa hata mwaka bado unasikia yuko kwao, mara mwanaume kaondoka kamuacha na ujauzito, yaani kila kitu ni shaghala baghala. Sasa kama uko kwenye ndoa au ndiyo unakaribia kuingia basi nakupa siri hizi saba kwanini ndoa nyingi zinakufa.
(1) Haraka ya mwanamke kutaka kummiliki mwanaume; Umeingia kwenye ndoa, haina hata miezi miwili ushaanza kuulizia kuhusu mali zake, kutaka kushirikishwa kwenye kila kitu chake na mbaya zaidi unataka asishirikishe ndugu zake, unawakasirikia na kutaka mawazo yako yasikilizwe yawe kama amri.
(2) Mwanaume kushindwa kuweka mipaka ya ndugu na mke; Umeoa unaishi na ndugu zako, ni nadra sana kuelewana. Lakini unatumia muda mwingi kwa ndugu zako, unaruhusu ndugu zako kumtukana mke wako, akiongea unamjibu vibaya anakua kama mgeni. Kauli za ndugu zangu ndiyo kila kitu, kama huwezi kuishi nao basi.
(3) Kumlinganisha mke/mume wako na ma X wako. iwe ni kwa ubaya au mazuri lakini kama kila akifanya kosa unalinganisha na X wako, maisha ya nyuma bado yamekutawala, unahofu labda naye atakuacha kama X wako, umebeba maumivu ya nyuma na visirani vya nyuma basi utaharibu na sasa.
(4) Kupotea kwa mawasiliano; Wanaume wakishaoa wanahisi wameshamaliza, mambo ya simu kama zamani hayapo, meseji hazipo, ukiondoka asubuhi ni mpaka jioni. Mwanaume unaongea na mke wako kama takataka na mwanamke unaongea na mume wako kama shoga yako, kama mtoto unaanza kumpangia, sitaki urudi saa ngapi, sitaki hiki na kile basi mnatibuana.
(5) Mategemeo makubwa sana kuhusu ndoa; Mwanamke ulikua huna furaha ukaamini ukiolewa ndiyo mume atakupa furaha, ataacha marafiki zake, ndugu na kila mtu kukusikiliza wewe. Unadhani atakuhudumia kila kitu, maisha yatakua mazuri. Mwanaume ulijua ukioa mambo yatakua rahisi, uko kwenye ndoa ila unataka kuwa kama kijana, urudi muda unaotaka, unataka mwanamke kunyenyekea kama kipindi cha uchumba, na kutaka mwanamke kufanya kila kitu ili tu kukufurahisha.
(6) Ubinafsi kuleta umimi katika ndoa; Mmeshaingia kwenye ndoa kila mtu anataka kufanya vitu kivyake, mnanunua kiwanja kila mmoja anataka kiwe na majina yake, hela yako ni yako hutaki mwenzako kuiona. Mwanaume unamuambia mimi ndiyo mwanaume kila kitu kiwe na majina yangu na mwanamke unasema kama wewe mwanaume basi fanya kila kitu kama mwanaume unajiweka pembeni na kuanza kufanya mambo yako kivyako.
(7) Kubeba mawazo ya watu wa nje; mama yako ndiyo anaamua namna unavyoishi na mke wako, dada yako anakupangia kila kitu na mke wako, kwakua ulishawazoea unawaamini hivyo unaamini kila kitu chako. Mwanamke Mama yako anakupangia kuhusu ndoa yako, anakuambia namna ya kuishi na mume wako, anakushauri kuficha vitu kwa mume wako. Mnaendeshwa na marafiki na unaonesha kuwajali wao kuliko mume/mke wako!
Nimeongea na watu wengi sana kuhusu ndoa, nimesikiliza sababu nyingi za watu kuachana siku hizi ndoa nyingi hazivuki miaka 3, unasikia flani aliolewa hata mwaka bado unasikia yuko kwao, mara mwanaume kaondoka kamuacha na ujauzito, yaani kila kitu ni shaghala baghala. Sasa kama uko kwenye ndoa au ndiyo unakaribia kuingia basi nakupa siri hizi saba kwanini ndoa nyingi zinakufa.
(1) Haraka ya mwanamke kutaka kummiliki mwanaume; Umeingia kwenye ndoa, haina hata miezi miwili ushaanza kuulizia kuhusu mali zake, kutaka kushirikishwa kwenye kila kitu chake na mbaya zaidi unataka asishirikishe ndugu zake, unawakasirikia na kutaka mawazo yako yasikilizwe yawe kama amri.
(2) Mwanaume kushindwa kuweka mipaka ya ndugu na mke; Umeoa unaishi na ndugu zako, ni nadra sana kuelewana. Lakini unatumia muda mwingi kwa ndugu zako, unaruhusu ndugu zako kumtukana mke wako, akiongea unamjibu vibaya anakua kama mgeni. Kauli za ndugu zangu ndiyo kila kitu, kama huwezi kuishi nao basi.
(3) Kumlinganisha mke/mume wako na ma X wako. iwe ni kwa ubaya au mazuri lakini kama kila akifanya kosa unalinganisha na X wako, maisha ya nyuma bado yamekutawala, unahofu labda naye atakuacha kama X wako, umebeba maumivu ya nyuma na visirani vya nyuma basi utaharibu na sasa.
(4) Kupotea kwa mawasiliano; Wanaume wakishaoa wanahisi wameshamaliza, mambo ya simu kama zamani hayapo, meseji hazipo, ukiondoka asubuhi ni mpaka jioni. Mwanaume unaongea na mke wako kama takataka na mwanamke unaongea na mume wako kama shoga yako, kama mtoto unaanza kumpangia, sitaki urudi saa ngapi, sitaki hiki na kile basi mnatibuana.
(5) Mategemeo makubwa sana kuhusu ndoa; Mwanamke ulikua huna furaha ukaamini ukiolewa ndiyo mume atakupa furaha, ataacha marafiki zake, ndugu na kila mtu kukusikiliza wewe. Unadhani atakuhudumia kila kitu, maisha yatakua mazuri. Mwanaume ulijua ukioa mambo yatakua rahisi, uko kwenye ndoa ila unataka kuwa kama kijana, urudi muda unaotaka, unataka mwanamke kunyenyekea kama kipindi cha uchumba, na kutaka mwanamke kufanya kila kitu ili tu kukufurahisha.
(6) Ubinafsi kuleta umimi katika ndoa; Mmeshaingia kwenye ndoa kila mtu anataka kufanya vitu kivyake, mnanunua kiwanja kila mmoja anataka kiwe na majina yake, hela yako ni yako hutaki mwenzako kuiona. Mwanaume unamuambia mimi ndiyo mwanaume kila kitu kiwe na majina yangu na mwanamke unasema kama wewe mwanaume basi fanya kila kitu kama mwanaume unajiweka pembeni na kuanza kufanya mambo yako kivyako.
(7) Kubeba mawazo ya watu wa nje; mama yako ndiyo anaamua namna unavyoishi na mke wako, dada yako anakupangia kila kitu na mke wako, kwakua ulishawazoea unawaamini hivyo unaamini kila kitu chako. Mwanamke Mama yako anakupangia kuhusu ndoa yako, anakuambia namna ya kuishi na mume wako, anakushauri kuficha vitu kwa mume wako. Mnaendeshwa na marafiki na unaonesha kuwajali wao kuliko mume/mke wako!